Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,235
Kwa wingi wao bungeni ilitarajiwa maslahi ya nchi yetu yaboreshwe na wabunge wa CCM, lakini badala yake wabunge wa upinzani walio wachache, ndiyo kila siku wanahangaika na hatima ya nchi yetu.
Hadi wakati mwingine najiuliza kama wingi wao ndiyo umewatia upofu wa fikra ama ni mahaba kwa chama chao ndiyo umewafanya wawe kama ndodocha kwa kila liletwalo na Serikali Bungeni.
Wabunge wa CCM Kila siku wakichangia mada bungeni, utawasikia wanalalamika kama vile nchi inasambaratika dakika inayofuatia, lakini muda kidogo baadaye wanaunga mkono kila jambo linaloletwa na serikali bungeni.
Kila siku wanauliza maendeleo yaliyoko kwenye majimbo ya wapinzani kama vile kwenye majimbo yao kuna maendeleo yaliyotukuka. Leo hii Livingstone Lusinde eti anahoji maendeleo ya Jimbo la Iringa mjini wakati jimboni mwake watu wanakunywa maji kwenye bwawa pamoja na Ng'ombe.
Wabunge wa CCM ni hasara kwa taifa kwa kuwa wanalipwa mishahara na posho kwa lengo la kuishauri na kuisimamia serikali, lakini wao kazi yao ni kuisifia na kuipamba hata kwa mambo yanayoumiza watanzania.
Ukitaka kujua uimara wa wabunge wa CCM, gusa chama chao!!
Hadi wakati mwingine najiuliza kama wingi wao ndiyo umewatia upofu wa fikra ama ni mahaba kwa chama chao ndiyo umewafanya wawe kama ndodocha kwa kila liletwalo na Serikali Bungeni.
Wabunge wa CCM Kila siku wakichangia mada bungeni, utawasikia wanalalamika kama vile nchi inasambaratika dakika inayofuatia, lakini muda kidogo baadaye wanaunga mkono kila jambo linaloletwa na serikali bungeni.
Kila siku wanauliza maendeleo yaliyoko kwenye majimbo ya wapinzani kama vile kwenye majimbo yao kuna maendeleo yaliyotukuka. Leo hii Livingstone Lusinde eti anahoji maendeleo ya Jimbo la Iringa mjini wakati jimboni mwake watu wanakunywa maji kwenye bwawa pamoja na Ng'ombe.
Wabunge wa CCM ni hasara kwa taifa kwa kuwa wanalipwa mishahara na posho kwa lengo la kuishauri na kuisimamia serikali, lakini wao kazi yao ni kuisifia na kuipamba hata kwa mambo yanayoumiza watanzania.
Ukitaka kujua uimara wa wabunge wa CCM, gusa chama chao!!