1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 6,255
- 7,930
Chenge mbona haguswi?? Jibu swali
Hana mgogoro wa kimadaraka na wenye nchi. Ni sehemu ya kujenga mfumo CCM .
Sio tishio kwa walioko madarakani na wale wanasaka madaraka.
Ukiangalia kwa haraka Kashfa za Escrow na Lugumi kashfa nyingi za miaka kumi ya utawala wa JK iligusa watu wachache wa ukanda mkubwa. Na hii ilikua ni maandalizi ya uchaguzi ili fedha hizo zitumile kwenye kampeni na kuhakikisha ukanda mkubwa unaipa CCM ushindi.
Hii nchi ina mafisadi wakubwa sana lakini hawaguswi kwa sababu hawana mvuto wa kisiasa na sio wanasiasa.
Ukitaka Chenge ashambuliwe kama mpira wa kona basi aonyeshe nia ya kugombea kwenye nafasi ya urais au uspika.
Hata Kwenye nafasi ya spika wa bunge amekua akijiweka pembeni ili tu asiingie kwenye migogoro ya kuchafuana na kuwhughulikiwa japo Chenge ndiye mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuongoza bunge.
Pia Chenge hakuna mahali alipoiba yeye kama yeye zaidi ya kupewa fungu lake kama mshauri wa kisheria sasa utamshitaki kwa lipi!
Magufuli kama kweli anataka ajue nani ametumia mali za umma kujilimbikizia mali basi afanye sensa ya kuzitambua mali zote zilizopo Tanzania ndani na nje ya nchi ili ijulikane nani anamiliki nini na amevipataje wakati aliku sio mfanyabiashara na hakulipa kodi popote. Hapo atakua ametenda haki.