Kuunga kwetu Zimbabwe hakuna mjadala - Kikwete,

Mugishagwe

JF-Expert Member
Apr 28, 2006
300
58
Je JK alishauriwa vyema na kualingalia swala la Zimbabwe kwa undani kabla hajaanza kumwa sifa na support kwa Mugambe badala ya wananchi wa Zimbabwe ? Je katika hotuba yake aliwaacha wapi wananchi wa Zimbabwe ambao wanateseka hadi wanatamani mkoloni kuwepo tena ??





2006-04-29 10:26:00
Na Maura Mwingira, Bulawayo


Rais Jakaya Kikwete amesisitiza kuwa uhuru wa kisiasa unakuwa na maana tu pale nchi inapokuwa na uwezo wa kujiamulia mambo yake bila ya kusukumwa au kuingiliwa na mataifa ya nje.

Alisema kama nchi haina uwezo wa kufanya hivyo basi maisha na watu waliojitolea mhanga kwa ajili ya uhuru wa nchi yao kama vile walivyojitolea wapigania uhuru wa Zimbabwe hayatakuwa na maana yoyote.

Alikuwa akizungumza wakati wa chakula cha usiku alichoandaliwa na mwenyeji wake, Rais Robert Mugabe, katika Ikulu ya Bulawayo.

Rais Kikwete alikuwa nchini hapa kwa ziara ya siku mbili ya kikazi.

’’Tunakuhakikishia kuwa, tutaendelea kupigia debe falsafa hii kwamba uhuru wa kisiasa utakuwa na maana kama tutaweza kujiamulia hatima yetu bila ya kusukumwa au kuingiliwa na mataifa ya nje,’’ alisema Rais na kushangiliwa na wageni waliohudhuria dhifa hiyo.

Rais ambaye mara baada ya kukanyaga ardhi ya Zimbabwe alipokewa na mwenyeji wake kwa kupigiwa mizinga 21, alisema Tanzania inatambua kipindi kigumu na ambacho wananchi wa nchi hiyo wanakipitia na kuongeza Tanzania inaunga mkono juhudi za nchi hiyo na kulijenga upya taifa lao na kuondokana na udhalimu wa kikoloni.

’’Nakupongeza kwa moyo wangu wote komrade Rais kwa kukataa kukubali mahangaiko na machungu mliyoyapata wakati wa vita vya kupigania uhuru wenu yaonekane kuwa hayana maana yoyote.

Changamoto yetu sote ni kuhakikisha kuwa matumaini waliyonayo wananchi hasa wale waliopoteza maisha yao wakipigania uhuru yanatekelezwa kikamilifu’’.

Alimhakikishia Rais Mugabe kuwa serikali yake imedhamiria kuendeleza na kudumisha uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizo mbili.

’’Nina uthamini na kuuendeleza uhusiano huu wa kidugu ambao Watanzania wameendelea kuuenzi tangu siku ile walipoona umuhimu wa kuungana mkono na kaka na dada zao wa Zimbabwe katika harakati za Chimurenga,’’ alisema Rais, kauli iliyoshangiliwa na wenyeji wake.

Alisema kuwa leo Waafrika wanatembea kifua mbele na wanazungumzia hatma ya bara lao kwa kujiamini kwa sababu wananchi wa Zimbabwe wamethubutu kuzungumza na kutenda katika maana ile inayotafsiri kuwa dhahama na udhalimu wa kikoloni ulikuwa na mwanzo wake kwa hiyo lazima utakuwa na mwisho wake.

’’Leo hii Komrade Rais, tunaweza kutangaza kwa ufahari na imani kubwa kuwa wale wote waliotoa mhanga maisha yao katika Chimurenga na harakati za ukombozi, hawakujitoa bure,’’ alisema.

Alisisitiza ’’komrade Rais, na kaka mpendwa nataka nikusisitize tena kwamba kukuunga kwetu mkono katika juhudi za kuleta mageuzi katika Zimbabwe, hauna mjadala wala masharti kama ambavyo imekuwa siku zote’’.

Rais Kikwete ambaye pia akiwa nchini hapa alifungua rasmi maonyesho ya biashara ya kimataifa, alisema kuwa ziara yake hiyo licha ya kujitambulisha kuwa yeye ndiye rais mpya wa Tanzania, lakini ilikuwa pia ni ya kujifunza namna ambayo nchi hiyo imeweza kupita hatua kubwa kiuchumi.

Kwa upande wake Rais Robert Mugabe alisema kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo imeendelea kuiunga mkono serikali yake kwa hatua yake ya kuwapatia wazawa ardhi na akashukuru kwa hatua hiyo.

’’Tanzania mmeendelea kuwa nasi katika harakati zetu za kuwapatia watu wetu ardhi. Mmekuwa nasi hata pale mataifa makubwa walipotuwekea vikwazo kwa uamuzi wetu, tunawashukuru sana kwa upendo wenu,’’ alisema.

SOURCE: Nipashe
 
Mzee Mugishagwe,

Hashima yako mkuu, naona hapo unachanganya mambo mawili mazito wazungu hawampigii kelele Mugabe kwa sababu ya wananchi kuwa na shida kwani si hata bongo wapo wananchi kwa mamillioni ambao wangependa mkoloni arudi! kwani tofauti yetu na Zimbabwe ni nini?

The issue hapa ni ardhi! Mugabe baada ya miaka mingi katika power alikuja kugundua kuwa asilimia 95% ya wananchi wake hawana ardhi au wanamiliki only 5% ya ardhi ya Zimbabwe nchi yao, wakati wazungu ambao ni asilimia 5% ya zimbabwe wana own 95% tu ardhi ya zimbabwe, kabla hajaanza pokonya pokonya ya ardhi hiyo aliwaomba wazungu yaani the West wamsaidie kulitatua tatizo hilo la Aedhi ya zimbabwe inlcuding The Commonwealth, wota wakaanza kujiuma uma, akamuomba Mbeki na Madiba, waote hawana jawabu, ndipo akaamua kuanza kuchukua ardhi hiyo na sio kwa faida yake bali kuwapa wananchi wa Zimbabwe, sio kama kina fulani hapa bongo ambao wamezichukua na kujenga majumba ya kupanga, sasa wewe mzee Mugishagwe hapa ni kipi usichoelewa? Hamna sababu ya kuwa Intellectual au professor, au genius kuelewa kuwa some where au somehow something had to be done! Na hata hawa wazungu wa Zimbabwe ni wapumbavu wakubwa kwani hata wao walipaswa kuelewa
kuwa it was coming kwa hiyo wangeanza mapema kutafuta njia za ku-reconcile au kutafuta njia za kubalance hii issue!

Mbeki, Madiba, na the whole OAU katika hili wako na Mugabe, kwani aliwauliza wote wamsaidie kumpa maarifa ya kuweza kuchukua hiyo ardhi bila kutumia nguvu none had an answerr for him, Mwalimu alimwambia achukue ardhi hiyo pale tu walipopata uhuru yeye akaamua kuheshimu makubaliona ya Lacanster, ambayo yalitengenezwa na wazungu kwa ujanja wa kujua kuwa ardhi yote ya Zimbabwe imo mikononi mwa wazungu, jamani tuache kusikiliza hawa the West waongo wakubwa na wanafiki wakubwa hawa, ndio wanatupa misaada lakini uhusiano uishie kwenye misaada tu sio mpaka waingilie siasa zetu,

Wewe mkuu Mugishagwe na the West mlitaka mugabe afanye nini?
 
Mkuu ES
Mimi nasema ardhi kuchukuliwa ama kugawanywa was the right decision ila njia zilizo tumika ndiyo mbaya.Mimi nasema Mzungu hawezi kumuona mweusi anahamia na kuwa own mali nyingi wachilia mbali ardhi.Nimekaa sana hapa Uingereza nimeona mifano micvhache ikiwemo wa kusumbuliwa Al Fayeed Baba yake Dodi kila mapesa yake.Mimi nalalamika ukatili wa Mugabe kwa watu wake na kutumia mabavu kuiba kura na kuwanyima haki Wazimbabwe na kuwatesa kama hali ilivyo sasa .Ardhi ni sahihi kuwa mkononi mwa Wazimba lakini je wangapa wameipata ? Waliyo pata ni wale walo mzunguka Mugabe na koo zao Zimbabwe na Wazimbabwe wana hali ngumu .Mim na ma Western hakuna ninacho kubaliana nao ni wabaya sana when it comes to we blacks interests amd rights
 
Mzee Es said:
Mzee Moshi,
Kumbe mambo yako mazito, lakini na yule muhindi pale Drive in cinema si naye alinyang'anywa ardhi na rais wetu aliyepita ili kuwapa Us wajemge ubalozi, au?
Sidhani km ni hasara km unavyoweza dhani.Iwapo hata taifa km German na Italy viongozi wao wa hivi karibuni wamewabwaga vigogo kwa vile tuu wameahidi kujenga uhusiano na US.Sijui sisi tutajidai nini hatutaki kutoka US.Hata vibosile wetu Russia na China wanabeep,wanang`ta na kupuliza kwani bado nao mwisho wa siku wanagonga kuunga mstari km sisi kuomba namna ya kwenda choo.Huyo mhindi sanasana ageishia kukwepa kodi na kwenda jenga Canada.
US wana mengi mabaya tena kwa taifa km Tanzania ambalo lilikuwa na mitazamo ya kijamaa na kuunga mkono siasa za mugabe,ndio mbaya zaidi.Ila sidhani km ni lazima adui aangamizwe,mara nyingine anaweza tumika vizuri zaidi km tutakuwa na sera nzuri.Us walijifanya kutukomoa kwa kuwapa kudai uchaguzi haukuwa huru na wa haki ila baadaye wakaja jua wanachopanda kitawatokea puani na pia ujasiri na busara za viongozi wetu viliwafanya wafikirie mara mbili na baadaye ikabidi waachane na ujinga.
Ninachoweza sema kwa watanzania ni kujiamini na kujenga uzalendo kwani tuna kila nafasi ya kujiandaa kuingia ktk ushindani na wageni.Hii haikuwepo kwa watu wa Zimbabwe kwani tayari kila kitu kilikuwa mikoni kwa matajiri wachache wa kizungu na hakuna aliyeweza kupata pa kuanzia kirahisi na akipata,asingeweza kupata ardhi kwani hela ya kununua au kukubaliwa kununua haikuwa rahisi kupatikana.
Mungu ibariki Tanzania,wabariki watanzania.Sasa hivi mzungu atapata ardhi kwa kufuata kanuni na si kupora na kupeana urithi wao kwa wao.Bado kuna watakopata kutokana na upuuzi wa wenzetu wachache wenye kuendeshwa kwa tamaa,ila bado hatuwezi kataa kuwa si wote tutakuwa wema ktk familia zetu na nchi yetu na kila afanyaye hivyo kuna nafsi ya kuhoji na kutmia sheria.
 
Mara yangu ya kwnaza kumuona ndugu yangu Augustino Moshi akiandika namna hii yaani ni mzalendo mwafrika wa hali ya juu na aliyoandika kwenye reply yake ni sawa kabisa na vile vile hata mimi nimekaa sana Zimbabwe na ninafahamu vizuri sana system inavyofanya kazi na hatua za Mzee RObert MUgabe ni sawa kabisa ,hawa watu kwanini wang'ang'anie ardhi ambayo hawakuilipia hata cent moja?.JK kafanya kitu chaa maana kuonyesha mapenzi yetu kwa ndugu zetu watu wa Zimbabwe na kumbukeni hizo ni nyayo za mzee Kambarage anazozifuata JK ,sio kitu kigeni kwa mtanzania kuwa upande wa mwafrika mwenzake hatukuanza leo wala jana hatua kama hizo ,tuliupigania uhuru na damu ya mtanzania nayo ilimwagika katika nchi hiyo.
UHuru???...kazi ya chama
Willo
 
Hivi Kikwete ni visionary kweli. je wakati anaongea haya alikuwa na akili timamu? je kauli zake bado ni sahihi hadi leo? watu visionary maneno yao hubaki kuwa kweli kwa muda mrefu sana.
 
I always have problem with giving my total confidence to people pleaser like JK. They are not their own people. Their firmness and confidence of decision making must all ways being questionable... Huwezi kuamini kweli alichoamua ndicho anachokiona moyoni au ni kufurahisha upande fulani au woga wa namna fulani wa kimalezi!!! Ni taabu tupu!! huoni hapa nyumbani...kakemea nini kwa moyo na dhati kabisa? ... si timing timing tuuu!

Kiongozi gani kujificha kwenye kuwa neutral almost kwenye kila kitu na kuachia mambo yajipeleke peleke tu?

Lazima Kukemea...Kuonya..kuelimisha na kupinga hadharani tena kwa dhati where is appropriate na Must... sio kupiga piga chenga ili kutokuudhi watu..au kufurahisha pande fulani... au woga wa kizembe.

Hivi ni kweli hakuna tolarable limit ya kudeal na mtu kama R Mugabe? Hivi kweli hakuna kiwango cha mwisho cha kuumiza wananchi wa taifa fulani ...simply Watu wa nchi hiyo walipigania Uhuru...!?

Ni mpaka Rais Kichaa aangamize Taifa lote..ndio hatua za dhati zichukuliwe?
 
Akiandaliwa chakula na Gordon Brown utaona atakavyoiponda Zimbabwe na kuunga mkono juhudi za serikali ya ushirikiano. What is all this: unafiki. Anaongea asiyoyawaza na anayoyawaza hayaongei. Hao ndio viongozi wetu!
 
SISHANGAI kinachoonekana hapa ni kuwa bado tuna kizazi cha wanaodai 'walileta uhuru' kama vile kwamba wasingelizawaliwa wao basi kusingekuwa na watu wengine wa kuleta uhuru na kutawala. No, way, katu isingelikuwa hivyo na pengine Afrika ingeliweza kuwa na kizazi kingine cha viongozi bora kabisa kuliko kizazi hiki cha viongozi kilichopotea na kilichotupoteza.

Afrika yote viongozi wake chali isipokuwa labda Botswana, Namibia, Angola na Rwanda ambako kweli tuna wanaume wanaofanya kazi. Na kazi inaoanekana. Waliobakia ni wapenda kujionesha kote duniani lakini hawana cha kujivunia kutokana na aibu ya umasikini na kubaki mno nyuma kimaendeleo kwa watu wao.
Muulize aliyeko madarakani mwaka mmoja, miwili, mitatu, kumi kafanya nini cha maana kama sio kuirudisha nyuma nchi yake.... na utaambulia porojo na takwimu mbichi za kupikwa kwa mkaa wa mkorosho!

Tatizo la viongozi wa Afrika ni kuwa wana fikra kwamba wao ni bora kuliko wananchi wao wote wakiwekwa pamoja na kwamba ni kazi yao kuteteana na kulindana wakiwa madarakani kwa kisingizio kuwa jambo hili ni kwa faida yangu na yako.

Guinea inatuonesha huu ni uzushi mtupu! Na kilichotokea Guinea kitarajiwe kwingineko Afrika kama tutandelea kuwa na akili fupi kama tulizo nazo sasa, kuwa na masikio tusisikie, kuwa na macho tusione, na kuwa pua tushindwe kunusa harufu ya vita na damau inayotunyemelea kila pembe hapa Afrika kutokana na viongozi wabovu na waliochoka kama kina Mugabe-ambaye kwangu hana tofauti na Hitler Mweusi, kiongozi aliye tayari watu wake wote wafe ili yeye aendelee tu kutawala. What a myopic view my deceived leader, what selfishness, what a crime to the silent humanity we call Zimbabweans! Whom, anyway, have no sympathy for at all, since they have been such unbelievable cowards!
 
Hivi Kikwete ni visionary kweli. je wakati anaongea haya alikuwa na akili timamu? je kauli zake bado ni sahihi hadi leo? watu visionary maneno yao hubaki kuwa kweli kwa muda mrefu sana.

mimi sio mwanadiplomasia na inawezekana sijui inavyofanya kazi, kikwete akaribishwe dinner, alafu hapo hapo aanza criticism ooooh mugabe achai madaraka, eeeh wewe hufai atarudi mzima huyu handsome wenu?

alichosema ni kuwa nchi iachiwe ifanye maamunzi na SIO MAANGAMIZI pasipokuingiliwa na watu wa nje, binafsi sidhani kama ni kuwa alipmpa support. I AM TRYING TO LEARN FROM SOMEBODY.
 
mimi sio mwanadiplomasia na inawezekana sijui inavyofanya kazi, kikwete akaribishwe dinner, alafu hapo hapo aanza criticism ooooh mugabe achai madaraka, eeeh wewe hufai atarudi mzima huyu handsome wenu?

alichosema ni kuwa nchi iachiwe ifanye maamunzi na SIO MAANGAMIZI pasipokuingiliwa na watu wa nje, binafsi sidhani kama ni kuwa alipmpa support. I AM TRYING TO LEARN FROM SOMEBODY.


Unalosema ni sawa.

Tatizo ninaloona mimi kuhusu kauli za Kikwete kwenye dinner hii ni kuwa:

Kwa vile alishakuwa waziri wa mambo ya nje kwa miaka kumi; alitakiwa awe ameshajua kuwa hali ya kisiasa Zimbabwe ni tete sana, na hasa kuwa huyo mwenyeji wake robati alikuwa anang'ang'ania madaraka kiasi kuwa alikuwa hataki kumpisha mtu mwingine hata ndani ya chama chake cha ZANU-PF. Kwa hali hiyo haikuwa sahihi kwake kutoa kauli kavu kuwa "kuunga mkono kwetu utawala wako mzee robati si jambo la mjadala." Ni afadhali angetumia lugha ya kidiplomasia kuwa "Tanzania tutaendelea kuwaunga mkono watu wa Zimbabwe katika jitihadi zao za kujienga demkrasi" Statement ya namna hiyo ingekuwa haimpi kiburi Robati binafsi kuwa anaungwa mkono na serikali nyingine, bali ingekuwa inaonyesha kuwa Tanzania tupo bega kwa bega na chaguo la wazimbabwe bila kujali ni mtu gani wanayemweka madarakani.
 
Mkuu ES, heshima mbele nadhani ni muhimu kutopotosha historia ya mahusiano kati ya Zimbabwe na Tanzania. Wakati wa mazungumzo ya Lancaster kuhusu uhuru wa Zimbabwe the most contetious issue was the LAND question; kitu ambacho karibu kilete kuvunjika kwa mazungumzo.Wazimbabwe walitaka swala la ardhi lipatiwe ufumbuzi kwenye mazungumzo yale na hiyo ikaleta stalemate kwenye mazungumzo kwani wazungu hawakuafiki; hapo ndipo mwalimu Nyerere alipointervene na kumshauri Mugabe akubali kuahirisha utatuzi wa swala hilo as a way of saving the negotiations ama sivyo uhuru wa Zimbabwe ungechelewa!! Ndio maana Tanzania has always had a moral obligation to support Mugabe wakati wa land seizure kule Zimbabwe.
 
Tanzania kumuunga mkono Mugabe siyo habari mpya.Mbona hata Mkapa alikuwa akifanya hivyo waziwazi kabisa.
 
Bulesi,
Mkuu umezungumza maneno mazito ambayo ndio kitu kikubwa sana.. isipokuwa umeacha kitu kimoja kuwa makubaliano ya Lancaster waliafikiana kuwa Muingereza angelipa fidia ya ardhi kwa wazungu ktk kipindi cha miaka 20.. Na ilipofikia mwisho mwa miaka 20 Muingereza alikuwa hajatoa zaidi ya asilimia 20 kwa sababu kaburu hakutaka kuporwa ardhi ile kisha kulazimishwa kuishi jirani na mtu mweusi..
Mhhhhn!Sisi tunawaona wao binadamu kama sisi wakati wao wanatuona sisi wanyama..

Wanabodi,
Swala la Zimbabwe kusema kweli wazee wangu ni zito kuliko sote tunavyofikiria... Mugabe nitamhukumu kwa mabaya yake kutokana na jinsi anavyotumia nguvu zake zote kuwaadhibu wananchi wake, yet nashindwa kusema zaidi kwa sababu Zimbabwe ni nchi iliyofungiwa milango yote ya biashara.. Kilimo cha Zimbabwe bila mbolea huwezi kustawisha kitu hata kidogo na mbolea haingii nchini humo. Mugabe has to go lakini ni muhimu atakaye chukua utawala lazima akubalike ktk ufumbuzi wa swala la ardhi kulinda uhuru na maslahi ya Wazimbabwe weusi.

Miezi michache iliyopita kuna meli toka China iliyokuwa ikitaka kutia namga South Afrika ilizuiwa wakisema ina vifaa vya kivita lakini ukweli ni kwamba meli ile ilikuwa na mbolea..Nakumbuka vizuri nilipata kusoma mahojiano kati ya mtangazaji mmoja wa South Afrika akimhoji nahodha wa meli ile wa kichina.. lakini sikuwahi kusoma wala kusikia ukweli huo mahala popote na wala ktk gazeti lolote zaidi ya meli ile kuwa imebeba silaha..

Sasa ebu tujiweke sisi ktk nafasi ya Zimbabwe..let's look on the other side pamoja na kwamba ni kinyume cha hali halisi ya Zimbabwe..Hivi kweli sisi Watanzania tunaweza kukubali leo hii ardhi iporwe na kupewa wazungu iwe kwa kilimo ama madini bila wananchi wake kupata fidia!..Tanzania kweli patakalika!..Yes, kutakuwepo na watu watakaounga mkono kwa sababu wanaishi Dar au miji mingine mikubwa lakini ushindani wake utatugawa vibaya sana..
Kwa hiyo pamoja na kwamba nimetumia fidia kwa misingi tofauti na ile ya Zimbabwe isipokuwa nachukulia hali halisi ya wananchi ambao wamepigana miaka yote kutafuta Uhuru wa kumiliki ardhi..wakiamini kuwa ardhi ile imeporwa leo uwambie wakubali matokeo yaishe!
Na kibaya zaidi ni kwamba hata Mugabe alipojaribu kutangaza kwamba ardhi ile haitakuwa mali ya weusi isipokuwa serikali kwa hiyo wazungu warudi watapewa kipimo cha ardhi kutokana na matumizi ya ardhi ile.. Makaburu wamekataa kata kata, wanataka kurudishiwa ardhi yao kwa sababu wao ni raia wa Zimbabwe na wana haki sawa na mtu mweusi ktk kumiliki ardhi kulingana na uwezo wako...Kwa nchi za magharibi hawaoni kabisa tofauti ya haki kati ya Mzimbabwe mweusi na mweupe ikiwa wote ni raia wa nchi hiyo..

Kwa Mugabe na wapiganaji Makaburu ni wahamiaji, waliopora ardhi kutokana na mfumo wa Kikoloni hivyo uraia wao ni wa karatasi..Ardhi ni mali ya Mzimbabwe mweusi ambaye alipokonywa na Mkoloni.. Yale yale ya Palestina!
Tunarudi pale pale swala la Uzawa..Mzawa ni mtu gani?.. 1. Mtu aliyezaliwa nchi hiyo, 2. Mtu aliye na asili ya nchi hiyo (Makabila), 3. Mtu mwenye wazazi au mzazi mzawa wa nchi hiyo!
 
Tatizo letu waafrika tunatumia njia nyingi na ndefu za kuchambua na kutathmini matatizo yetu hadi tunachanganyikiwa. Tukiambiwa umasikini wetu umeletwa na viongozi wetu wenyewe tunaanza kuchambua na ku-analyse mambo tunarudi hadi historia ya kikoloni na kulaumu kila mtu anayeonekana na ngozi nyeupe as if ni sisi tu hapa duniani tulitawaliwa na kunyang'anywa ardhi ndio maana tumekuwa mafukara kiasi hiki.

Mimi nasema tatizo letu ni akina Mugabe, Banda, Mobutu, nk. It is obvious that viongozi wetu hususan waliotuletea uhuru wa kisiasa ndio waliotufikisha hapa tulipo. Inaniuma sana wasomi wetu wanalaumu matatizo ya Afrika kwa kutumia maneno kama neoliberalism, imperialism, globalization, nk. Hivi kuna haja ya kufanya uchambuzi kisomi ili kumjua mchawi wetu? kwa mfano mikataba feki ya madini Tanzania ni nani alaumiwe? Ni makampuni ya "kinyonyaji" au ni Mkapa na genge lake?

Kwa kifupi ni kwamba kuiokoa Zimbabwe kiuchumi na kijamii ni lazima Mugabe aondoke, ikibidi hata auawe kama ilivyofanyika kwa Savimbi! Na kuiokoa Africa ni lazima tuondokane na uchambuzi feki wa kisomi wa kulaumu ukoloni na mataifa ya magharibi. Haya mataifa yako na yataendelea kuwepo na kulinda na kupigania maslahi yao popote pale duniani. Hayako kwa ajili yetu ila kwa ajili yao na wananchi wao.

Lazima tuamke, viongozi wetu waige mfano wa nchi za Asia. Zimefanikiwa kujikwamua kiuchumi kwa kufanya kazi na mataifa hayo hayo tunayoyalaumu kwamba yanatudidimiza. Umaskini wetu unatafutiwa visingizio vya ajabu ajabu na wanasiasa na wasomi wetu waliofeli kifikra! Tusikubali!
 
Nurujamii,

Tafadhali rejea posts za hawa wafuatao ili uweze kulielewa tatizo la Zimbabwe vizuri: Bulesi, Augustine Moshi and Field Marshall ES.

N.B. Sidhani kama wazungu walifanya madudu kule Asia kama walivyofanya Zimbabwe. Kwa mfano, hawakuivamia China, Malyasia, Singapore, South Korea e.t.c na kupora ardhi yote yenye rutuba huku wakiwaacha wazawa bila ardhi. I think, there partnership has more to do with trade than otherwise.
 
Mara yangu ya kwnaza kumuona ndugu yangu Augustino Moshi akiandika namna hii yaani ni mzalendo mwafrika wa hali ya juu na aliyoandika kwenye reply yake ni sawa kabisa na vile vile hata mimi nimekaa sana Zimbabwe na ninafahamu vizuri sana system inavyofanya kazi na hatua za Mzee RObert MUgabe ni sawa kabisa ,hawa watu kwanini wang'ang'anie ardhi ambayo hawakuilipia hata cent moja?.JK kafanya kitu chaa maana kuonyesha mapenzi yetu kwa ndugu zetu watu wa Zimbabwe na kumbukeni hizo ni nyayo za mzee Kambarage anazozifuata JK ,sio kitu kigeni kwa mtanzania kuwa upande wa mwafrika mwenzake hatukuanza leo wala jana hatua kama hizo ,tuliupigania uhuru na damu ya mtanzania nayo ilimwagika katika nchi hiyo.
UHuru???...kazi ya chama
Willo
....jamani,mnazungumzia(willo&moshi) mambo ya ukoloni,....ardhi....kuna kipinduX2,njaa watu wanachemsha ngozi za wanyama kama kitoweo!! sasa hivi hiyo ardhi waliyonayo hawawezi hata kupanda dengu!! inamaana gani???sanasana watu wanachimba makaburi kila kukicha!! C'mon people!!
 
Nurujamii,
Lazima tuamke, viongozi wetu waige mfano wa nchi za Asia. Zimefanikiwa kujikwamua kiuchumi kwa kufanya kazi na mataifa hayo hayo tunayoyalaumu kwamba yanatudidimiza. Umaskini wetu unatafutiwa visingizio vya ajabu ajabu na wanasiasa na wasomi wetu waliofeli kifikra! Tusikubali!
Mkuu Zungu Pule amekujibu vizuri sana, hizo nchi za Asia zote hazina wazungu waliochukua ardhi yao na kama ingetokea hivyo hadithi ingekuwa tofauti kabisa..Ukalie ardhi ya Mchina au Mhindi weee umewasahau Mao Tse Tung na Indira Gandhi.
Ni nchi kama Australia, New Zealand, Marekani, Canada ambazo zimesimama dhidi ya Zimbabwe na histori ya nchi hizo inatuambia kwamba wazawa walinyang'anywa ardhi zao..Hivyo ni vigumu kwa nchi hizi kuelewa kwa mapana kitu gani Mugabe hataki kwani wao kumwondoa mzawa sii swala la mjadala...
Bila shjaka Mugabe has to go na nafikiri ingekuwa rahisi sana kumwondoa Wazimbabwe kama mataifa haya yasingeingilia sana na hasa kumsikiliza kibaraka wao. Mugabe alikwisha chemsha, alikwisha chemsha kabla ya uchaguzi uliopita 2000, kama sio mdomo wa Blair kuingilia kati maamuzi ya kuchukuliwa ardhi wananchi wa Zimbabwe wasingweza kuiona sababu ya kutomchagua Mugabe... Ukisikiliza kampeni nzima ya Mugabe wakati ule ilikuwa kuhusu Uingereza tu, utafikiri alikuwa anagombea Urais against Prime Minister Blair! na wananchi wakamsikia kwani kila Blair akibwabwaja Mugabe anaitoa ktk Luninga..Matokeo yake Mugabe alishinda kwa asilimia 120 of 150 seats wakati mwaka 2000 Mugabe alishinda viti 63 tu kati ya viti 120...kila mtu alijua Mugabe anaondoka uchaguzi unaofuata..
 
Hauxtable,
Mkuu wewe unafikiri wafanye nini? nimekwisha sema kumwondoa Mugabe will never change a thing kama ardhi haijarudishwa kwa wazungu..Kama Cuba madai yao yalikuwa Castro kaondoka bado yale yale, North Korea walisema haya haya alipokuwa Kim Il Sung baba yake na huyu rais wa sasa hivi Kim Jong Il lakini hakuna mabadiliko yoyote kudhihirisha kwamba tatizo ni mtu, isipokuwa Policy..
sasa kama tunataka kupata jawabu ya matatizo ya Zimbabwe ningeomba wenzangu mtoe ushauri Wazimbabwe wafanye nini hata kama Mugabe akiondoka.. ku surrender ardhi yao! au mna maoni gani kwa Wazimbabwe!
 
Back
Top Bottom