Kuundwa upya tawi la asasi ya kupambana na rushwa

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,604
1,704
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KONGAMANO la siku mbili lililoandaliwa na asasi ya Concern for Development Initiative in Africa (ForDIA) lilimalizika jana (Ijumaa 8 Mei 2009) jijini Dar es Salaam kwa mafanikio katika maeneo mawili makuu kitaifa na kimataifa:

1. Wadau waliamua kuunda upya tawi la asasi ya kimataifa ya kupigania uwazi na kupambana na rushwa – Transparency International (TI) – kwa kuipa sura ya kitaasisi na hadhi ya kisheria.

Jina la Tawi la Tanzania litakuwa Tanzania Transparency Forum (TRAFO).

Katika muktadha huu, wadau walichagua Kamati ya Muda ya Utekelezaji ya kusimamia mchakato hadi kusajiliwa kwa tawi katika kipindi kisichozidi miezi sita.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ni Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; Makamu Nape Mnauye wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Bubelwa Kaiza anayekuwa Katibu Mtendaji. Kaiza ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa ForDIA.

2. Wadau walipokea na kujadili Ripoti ya ForDIA juu ya mtazamo wa wananchi kuhusu rushwa (Mtazamo-rushwa) katika wilaya 35 za Tanzania Bara ambayo ilizinduliwa rasmi jana katika hotel ya Giraffe Ocean View. Ripoti inachambua ifuatavyo:

(i) Halmashauri ambazo hazina kiwango kikubwa cha matukio ya rushwa: Tandahimba (asilimia 95), Mtwara Vijijini (89.55), Ulanga (87.5), Nachingwea (85.2), Liwale (84.9), Shinyanga mjini ( 84.4), Mbinga (83.3) na Ruangwa (77.05).

Nyingine zilizo juu ya asilimia 50 ni Tunduru (76.6), Mbeya Vijijini (75), Rungwe (73.3), Kilosa (66.65), Morogoro Mjini (61.4), Kilwa (60.4.), Kyela (58.35) na Lindo Mjini ( 50.35).


(ii) Halmashauri zinazoongoza kwa kiwango kikubwa cha matukio ya rushwa: Mbozi (asilimia 93.75)), Muleba (93.5), Bukoba Vijijini (87.85), Bariadi (80), Miseny (7, na Newala (70.85), Kishapu (70.1), Meatu (68.35), Mtwara Mjini (65.2), Bukoba Mjini (64.6).

Nyingine zinazoongoza kwa matukio ya rushwa juu ya asilimia 50 ni Kahama (63., Mbeya Mjini (62.5), Namtumbo (61.05), Bukombe (60.4), Mbarali (60.15), Ileje 59.65), Lindi Vijijini (56), Mvomero (55), na Chunya (52.1).

Akizindua Ripoti ya Mtazamo-rushwa, Mkurugenzi Mtendaji wa TAKUKURU, Dk. Edward G. Hosea alisema kazi iliyofanywa na ForDIA ni kubwa na muhimu; na kwamba kazi za aina hiyo huwapa watunga sera ushahidi mwanana wa tatizo husika ili wapate upenyo wa kuanzia katika kukabiliana na tatizo.

Aliwapa changamoto wadau katika eneo hili, wasomi, wanataaluma katika medani ya maendeleo, watafiti na wananchi kwa ujumla, kusoma, kujadili na kutoa maoni juu ya ripoti hiyo yenye kurasa 135.


Bubelwa Kaiza
Mkurugenzi Mtendaji


--------------
Executive Director
Concern for Development Initiatives in Africa (ForDIA)
Secretariat of the Great Lakes Peace and Security Network (PeSeNet)
Off University Road, Survey Area, Kawe/Mlalakuwa Plot # 301-304, House # 250
P.O. Box 32505,
Dar es Salaam -TANZANIA
Tel: +255 22 2701890
+255 22 2701895-6
Cell: +255 784 410 939
Fax: +255 22 2701890
E-mail: bubelwa.kaiza@fordia.org
Website: www.fordia.org

 
Last edited:
Kama Takukuru ambayo inaongozwa na Hosea bado iko juu ya hiki chombo kipya kimamlaka basi hakuna jipya tutakalolitegemea sisi Watanzania zaidi ya kubebeshwa mzigo wa kulipia gharama za uendeshaji wa chombo hiki kipya.
 
Kama Takukuru ambayo inaongozwa na Hosea bado iko juu ya hiki chombo kipya kimamlaka basi hakuna jipya tutakalolitegemea sisi Watanzania zaidi ya kubebeshwa mzigo wa kulipia gharama za uendeshaji wa chombo hiki kipya.

Takukuru haiko juu yake. Hicho ni chombo huru. Hakifungamani na Serikali.
 
Ni vigezo gani wanatumia kujua Wilaya ina rushwa zaidi au la? CAG report? Au ni utafiti mwingine?

Walifanya utafiti wa kina katika ngazi ya Serikali za mitaa. Nikipata nakala ya utafiti huo nitaiwamba hapa. Unatofautiana sana na tafiti za Serikali.
 
Wanahusiana vipi na Transparency International?

Rejea hiyo taarifa yao hapo. Wao ni tawi la Transparency International. Liliwahi kuwepo hapo zamani. Likafungwa. Sasa ndio wanalifungua upya.
 
Rejea hiyo taarifa yao hapo. Wao ni tawi la Transparency International. Liliwahi kuwepo hapo zamani. Likafungwa. Sasa ndio wanalifungua upya.

Mlipo jichanganya ni kumuweka Hosea, Unajua watu wakisha ona yumo Hosea masfisha mafisadi wanajua ni yale yale.. na hivo kuichukulia ndivyo sivyo. May be kwa ushauri next time hakikisha mna jiweka mbali na TAKUKURU na hasa Bosi wao Hosea, kwani ataharibu sura ya kila kitu, jamaa hakubaliki tena mbele ya jamii period!
 
Mlipo jichanganya ni kumuweka Hosea, Unajua watu wakisha ona yumo Hosea masfisha mafisadi wanajua ni yale yale.. na hivo kuichukulia ndivyo sivyo. May be kwa ushauri next time hakikisha mna jiweka mbali na TAKUKURU na hasa Bosi wao Hosea, kwani ataharibu sura ya kila kitu, jamaa hakubaliki tena mbele ya jamii period!

Wamemuweka wapi?
 
Soma paragraph ya pili kutoka mwisho ya bandiko hili

Nilishasoma taarifa yote sijaona sehemu yoyote katika hiyo asasi alipowekwa mtu yoyote wa Takukuru - Mwenyekiti ni Prof. Mwesiga Baregu, Makamu wake ni Nape Nnauye na Katibu Mtendaji ni Bubelwa Kaiza.
 
Nilishasoma taarifa yote sijaona sehemu yoyote katika hiyo asasi alipowekwa mtu yoyote wa Takukuru - Mwenyekiti ni Prof. Mwesiga Baregu, Makamu wake ni Nape Nnauye na Katibu Mtendaji ni Bubelwa Kaiza.

Well naona tu tumepishana lugha, nina maana hapo walipo muweka katika inaugration
 
Just disband TAKUKURU altogether. The organisation can't quantify its work. The quality of its work is appaling, actually almost non-existent.

1.Hebu tujiulize budget ya kuendesha TAKUKURU ni kiasi gani kwa mwaka?

2.Tukishapata jibu hilo tujiulize returns za kazi wanayofanya inalingana na investment ya walipa kodi. Hawajawahi kufunga hata individual mmoja wa high profile.

3.Mwisho, hii TAKUKURU ipo kwa manufaa ya nani? Serikali ionekana inafanya kazi? Wajanja wachache wapate kujificha nyuma ya pazia hilo? Tunadanganyana tu, tunapotezeana muda. Hii fedha peleka mashuleni au hospitalini walalahoi wanufaike, lakini kusema mapambano ya rushwa nii DHAMBI TUPU!!!

Should we outsource kwa wageni kutoka nje waje kufanya kazi ya TAKUKURU? Sikia reaction ya watu hapo..........
 
Back
Top Bottom