Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,089
Magufuli alitaka kuunda mkoa nyumbani kwake kwa utashi tu binafsi bila kujali vigezo vyenye mantiki vya kuunda mkoa huo.
Yaani katika muendelezo wake wa "unyumbani" akavunja protokali zote za kimantiki na kivigezo katika kuubda mkoa mpya.
Leo hii mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa michanga kabisa ambayo haina umri hata wa miaka 20, lakini cha ajabu yanaletwa mapendekezo ya kukata eneo kutoka mkoa huo kwenda kuunda mkoa mwingine—Ili iweje?
Lakini kibaya zaidi, Leo tunakwenda kukata eneo la mkoa ambao by all standards ni mkoa kongwe, wenye historia ndefu, Mkoa wa Kagera, uliobeba historia ya nchi hii kwa utamaduni wake mzuri, historia ya falme zake, lugha yake n. k tunakwenda kumegua eneo katika huo mkoa na kuunda mwingine tu ili kumpa mwendazake hitajio la moyo wake, bila kuangalia cultural-social dynamics za watu.
Tunajua Magufuli hakuwahi kuwapenda Wahaya, hata alipokuwa Waziri aliplay key role kwenye kuimega Chato kutoka mkoa wa Kagera.
Sasa hilo halikuishia hapo, leo tunakwenda kuimega Ngara na Biharamulo tena na kuiundia mkoa ili iweje?
Kama mnadhani kuunda mkoa ni kusogeza huduma kwa wananchi, basi uongezeeni bajeti mkoa wa Kagera na usogezeeni huduma ili huduma ziendelee kupatikana humohumo badala ya Kuumega mkoa huo.
Chato haina vigezo vya kuwa mkoa tunalazimisha mambo kumuenzi Marehemu bila kujali misingi ya utamaduni na historia za maingiliano ya watu wa maeneo husika.
Samia Iache Kagera kama ilivyo, ila Isogezee huduma zaidi!
Yaani katika muendelezo wake wa "unyumbani" akavunja protokali zote za kimantiki na kivigezo katika kuubda mkoa mpya.
Leo hii mkoa wa Geita ni miongoni mwa mikoa michanga kabisa ambayo haina umri hata wa miaka 20, lakini cha ajabu yanaletwa mapendekezo ya kukata eneo kutoka mkoa huo kwenda kuunda mkoa mwingine—Ili iweje?
Lakini kibaya zaidi, Leo tunakwenda kukata eneo la mkoa ambao by all standards ni mkoa kongwe, wenye historia ndefu, Mkoa wa Kagera, uliobeba historia ya nchi hii kwa utamaduni wake mzuri, historia ya falme zake, lugha yake n. k tunakwenda kumegua eneo katika huo mkoa na kuunda mwingine tu ili kumpa mwendazake hitajio la moyo wake, bila kuangalia cultural-social dynamics za watu.
Tunajua Magufuli hakuwahi kuwapenda Wahaya, hata alipokuwa Waziri aliplay key role kwenye kuimega Chato kutoka mkoa wa Kagera.
Sasa hilo halikuishia hapo, leo tunakwenda kuimega Ngara na Biharamulo tena na kuiundia mkoa ili iweje?
Kama mnadhani kuunda mkoa ni kusogeza huduma kwa wananchi, basi uongezeeni bajeti mkoa wa Kagera na usogezeeni huduma ili huduma ziendelee kupatikana humohumo badala ya Kuumega mkoa huo.
Chato haina vigezo vya kuwa mkoa tunalazimisha mambo kumuenzi Marehemu bila kujali misingi ya utamaduni na historia za maingiliano ya watu wa maeneo husika.
Samia Iache Kagera kama ilivyo, ila Isogezee huduma zaidi!