Kuumbeee, hata magazeti ni mafisadi...!!

BabaDesi

JF-Expert Member
Jun 30, 2007
6,033
3,944
Naombeni Msaada. Siku ya Jumanne kuna Mbunge wa Upinzani alisimama na kutoa hoja akihoji juu ya Kampuni ya Simu ya VodaCom kupewa likizo nyingine kulipa kodi. Kwa bahati mbaya sikusikia jina la Mbunge mwenyewe wala tarakimu za Mabilioni yaliyotajwa. sikuwa na wasiwasi, nikasubiri kesho yake ili kuisoma kwa undani taarifa ile. Kwa Mshangao wangu, hakuna hata gazeti moja lililoandika kuhusu habari ile ambayo mimi nilidhani kuwa ingekuwa 'front page news'!! Mpaka leo Jumamosi ninapoandika habari hii, hakuna hata gazeti moja ambalo limeiandika habari ile. Wakati nikiomba mtu mwenye uwezo wa kupata Hansard za Bunge atuwekee hapa hoja ile tuisome vizuri, bado nimeshangazwa na unafiki wa magazeti ya Tanzania wa kupigia kelele mafisadi lakini yenyewe kwa kuogopa kupewa matangazo ya Vodacom yameacha kuandika habari ile muhimu...!!HUU SI UFISADI???
 
Last edited:
sasa mpaka leo ni haujafahamu kama ni bora kusoma magazeti ya udaku kuliko haya yanayojifanya yako mstari wa mbele kuandika habari za kitaifa yatakupoteza na kukufanya mwendawazimu ,kwani yanayosemwa siyo yanayoandikwa na yanavyoandikwa sivyo habari zenyewe zilivyo ,utasikia sijui linataka kushitakiwa ,sijui niombeeni razi ,yaani yanatumika kuwapa umaarufu watu wasio na faida na Taifa hili ukiyachunguza kwa ndani yana watu wao ambao huandika habari na kupamba kila aina ya mijisifa japo haistahiki wala hakionekani kikubwa alichokifanya ,zaidi haya magazeti ni maarufu kwa kueneza fitna na majungu ,ndio maana ukaona huandika pale wanapoona patavuruga na kutoleta maelewano ila mambo ya haki hawayaandiki ,wewe tazama tu habari za vyama vya upinzani kama zinaandikwa na zikifikia kuandikwa basi kuna ujumbe utafikiri hotuba za Bin Laden wanaelewana wenyewe wahusika tu.
 
Naombeni Msaada. Siku ya Jumanne kuna Mbunge wa Upinzani alisimama na kutoa hoja akihoji juu ya Kampuni ya Simu ya VodaCom kupewa likizo nyingine kulipa kodi. Kwa bahati mbaya sikusikia jina la Mbunge mwenyewe wala tarakimu za Mabilioni yaliyotajwa. sikuwa na wasiwasi, nikasubiri kesho yake ili kuisoma kwa undani taarifa ile. Kwa Mshangao wangu, hakuna hata gazeti moja lililoandika kuhusu habari ile ambayo mimi nilidhani kuwa ingekuwa 'front page news'!! Mpaka leo Jumamosi ninapoandika habari hii, hakuna hata gazeti moja ambalo limeiandika habari ile. Wakati nikiomba mtu mwenye uwezo wa kupata Hansard za Bunge atuwekee hapa hoja ile tuisome vizuri, bado nimeshangazwa na unafiki wa magazeti ya Tanzania wa kupigia kelele mafisadi lakini yenyewe kwa kuogopa kupewa matangazo ya Vodacom yameacha kuandika habari ile muhimu...!!HUU SI UFISADI???

Mkuu hii habari iliandikwa na Daily News.....si unajua tena wahusika wa Vodacom Tanzania ni akina nani? Ukishapata jawabu unaweza ukaelewa kwanini habari haikupewa kipambaule.

http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=5442

THE Legislator for Gando(CUF), Mr Khalifa Suleiman Khalifa, has questioned the criteria used and basis for granting a mobile phone company, Vodacom Tanzania Limited, tax holiday of 10 years.

Debating the Prime Minister's Office 2008/09 budget estimates, Mr Khalifa said by exempting the company from income and corporate tax the government was losing billions of shillings.

He told the House that when it started operations the company was granted a tax holiday of five years and that it received an extension of another five years upon the expiry of the earlier term.

The MP said it was estimated that the company which was paying between 6bn/- and 8bn/- in Value Added Tax a month had an annual turnover of over 350bn/-. "That means this company collects over 300bn/- a year and yet does not pay tax," he said.

Mr Khalifa wanted to know who made that decision and why on that particular company while there were four other firms that provided mobile phone services in the country.

He said since tax being one of the main sources of the government's revenue the move was detrimental to the country's economy and national development.

Worse still, he said mobile phone tariffs remained high among all companies making Tanzania the second country in the world with exorbitant rates after Turkey.
 
Mkuu hii habari iliandikwa na Daily News.....si unajua tena wahusika wa Vodacom Tanzania ni akina nani? Ukishapata jawabu unaweza ukaelewa kwanini habari haikupewa kipambaule.

http://dailynews.habarileo.co.tz/home/index.php?id=5442

THE Legislator for Gando(CUF), Mr Khalifa Suleiman Khalifa, has questioned the criteria used and basis for granting a mobile phone company, Vodacom Tanzania Limited, tax holiday of 10 years.

Debating the Prime Minister's Office 2008/09 budget estimates, Mr Khalifa said by exempting the company from income and corporate tax the government was losing billions of shillings.

He told the House that when it started operations the company was granted a tax holiday of five years and that it received an extension of another five years upon the expiry of the earlier term.

The MP said it was estimated that the company which was paying between 6bn/- and 8bn/- in Value Added Tax a month had an annual turnover of over 350bn/-. "That means this company collects over 300bn/- a year and yet does not pay tax," he said.

Mr Khalifa wanted to know who made that decision and why on that particular company while there were four other firms that provided mobile phone services in the country.

He said since tax being one of the main sources of the government's revenue the move was detrimental to the country's economy and national development.

Worse still, he said mobile phone tariffs remained high among all companies making Tanzania the second country in the world with exorbitant rates after Turkey.

Duh! Tax Exemption for 10 years!!! Kweli Rostam Azizi ameshika utamu!!! Wakati Watanzania wenye kipato kidogo wanahenyeka kulipa kodi kila kukicha!!!
 
Kwa hiyo manataka kuniambia Tanzania Daima nalo ni gazeti la kifisadi au linamilikiwa na mafisadi?
 
Duh! Tax Exemption for 10 years!!! Kweli Rostam Azizi ameshika utamu!!! Wakati Watanzania wenye kipato kidogo wanahenyeka kulipa kodi kila kukicha!!!

Bubu ataka kusema,
Hivi kweli watu wenye kipato kidogo wanalipa kodi Tanzania? Naomba uziorodheshe kodi wanazolipa na viwango ili tuanze kuzipigania hapa.
Halafu kuna jambo jingine hapa inabidi tuwe wazi, unapokuwa mfanyabishara lengo lako kubwa ni kupunguza gharama na kuongeza kipato. Kama umeweza kupunguza gharama kama Vodacom basi wewe ni mfanyabishara mzuri. Kwa mawazo yangu hapa wa kulaumiwa ni aliyotoa msamaha huo. Jambo jingine la kuangalia ni faida gani taifa limepata kutokana na msamaha huo wa kodi. Kama Vodacom isingekuwepo taifa lingepata faida gani au hasara gani. Lazima tukumbuke ili kuendelea kiuchumi "communication" is no.1 factor.
 
Bubu ataka kusema,Hivi kweli watu wenye kipato kidogo wanalipa kodi Tanzania? Naomba uziorodheshe kodi wanazolipa na viwango ili tuanze kuzipigania hapa.
Halafu kuna jambo jingine hapa inabidi tuwe wazi, unapokuwa mfanyabishara lengo lako kubwa ni kupunguza gharama na kuongeza kipato. Kama umeweza kupunguza gharama kama Vodacom basi wewe ni mfanyabishara mzuri. Kwa mawazo yangu hapa wa kulaumiwa ni aliyotoa msamaha huo. Jambo jingine la kuangalia ni faida gani taifa limepata kutokana na msamaha huo wa kodi. Kama Vodacom isingekuwepo taifa lingepata faida gani au hasara gani. Lazima tukumbuke ili kuendelea kiuchumi "communication" is no.1 factor.

Ukisoma bajeti ya serikali unaweza kuona mshahara wa kuanzia 120,000 unalipiwa kodi. Sasa jiulize ni Watanzania wangapi wanapata hicho kipato na wanalipia kodi serikalini. Kama wao wanalipia vipi Vodacom na 'wawekezaji' wengine wasilipie au wapewe tax holiday 'milele'? suala la Vodacom kuwapo na kuishi bila kodi, ingekuwa bora zaidi kama isingekuwapo ili wananchi wajue hakuna mtu anayejichotea mapesa bila ya kulipia kodi.
 
HUU SI UFISADI???

Sio ufisadi, ni ujuzi mdogo tu, wa Uandishi Habari nchini kwetu.

Mpaka leo sijaona gazeti lilioandika kwamba Zimbabwe wameita balozi wake nyumbani. Wakati hii ni major story.
 
cha kushangaza ni gazeti la serikali ndio liliandika mengine ya binafsi kwanini hawakuinyaka?

Magazeti yetu yanaandika habari kwa muangalia aliyesema nani na si habari yenyewe, hilo swala lingesemwa na zito au siraa magazeti yote yangeandika lakini kwasababu kasema mtu asiyejulikana waliacha hapo hapo.
 
Mwanakijiji,
gazeti la serikali linaishi kwa kodi za waathirika wa ufisadi, lakini magazeti binafsi yanaishi kwa matangazo ya makampuni kama hayo ya Vodacom. Hivi ulishamuona nani anakata mkono unaomlisha, hata kama ndio mapenzi na maadili ya uandishi?
 
Ukisoma bajeti ya serikali unaweza kuona mshahara wa kuanzia 120,000 unalipiwa kodi. Sasa jiulize ni Watanzania wangapi wanapata hicho kipato na wanalipia kodi serikalini. Kama wao wanalipia vipi Vodacom na 'wawekezaji' wengine wasilipie au wapewe tax holiday 'milele'? suala la Vodacom kuwapo na kuishi bila kodi, ingekuwa bora zaidi kama isingekuwapo ili wananchi wajue hakuna mtu anayejichotea mapesa bila ya kulipia kodi.
Sidhani kama huyo mbunge amesema makampuni mengine ya simu yanalipa kodi. Najua kampuni kama Tigo inastahili kuwemo kwenye "tax holiday". Mbunge amezungumzia urefu wa tax holiday. Hoja yake ameijenga vizuri baada ya kuweka figures ambazo zinaonyesha ni kiasi gani Vodacom wanapata kutokana na tax holiday. Kama faida wanayopata ni kubwa kuliko kiasi cha fedha wanachopata basi hawastahili extension ya tax holiday. Kwa upande wangu bila kuangalia ni kiasi gani cha faida wanachopata au uhusiano wao wa kibiashara na RA, leo hii kama Vodacom ikifa, sehemu nyingi za nchi yetu huko vijijini zitakosa mawasiliano ya simu na niwajibu wa serikali kuilinda kwa sababu ina cover moja ya wajibu wake wa kuhakikisha kuna mawasiliano sehemu yote ya nchi. Ningependa sana kujua mawazo ya Mnyika wa CHADEMA kwenye hili kwa maana yeye anatumia Voda for years.
 
sidhani Kama Huyo Mbunge Amesema Makampuni Mengine Ya Simu Yanalipa Kodi. Najua Kampuni Kama Tigo Inastahili Kuwemo Kwenye "tax Holiday". Mbunge Amezungumzia Urefu Wa Tax Holiday. Hoja Yake Ameijenga Vizuri Baada Ya Kuweka Figures Ambazo Zinaonyesha Ni Kiasi Gani Vodacom Wanapata Kutokana Na Tax Holiday. Kama Faida Wanayopata Ni Kubwa Kuliko Kiasi Cha Fedha Wanachopata Basi Hawastahili Extension Ya Tax Holiday. Kwa Upande Wangu Bila Kuangalia Ni Kiasi Gani Cha Faida Wanachopata Au Uhusiano Wao Wa Kibiashara Na Ra, Leo Hii Kama Vodacom Ikifa, Sehemu Nyingi Za Nchi Yetu Huko Vijijini Zitakosa Mawasiliano Ya Simu Na Niwajibu Wa Serikali Kuilinda Kwa Sababu Ina Cover Moja Ya Wajibu Wake Wa Kuhakikisha Kuna Mawasiliano Sehemu Yote Ya Nchi. Ningependa Sana Kujua Mawazo Ya Mnyika Wa Chadema Kwenye Hili Kwa Maana Yeye Anatumia Voda For Years.

Si Kweli Kati Ya Makampuni Yasiyo Taka Ku-invest Rural Areas Ni Vodacom. Huwa Hawajengi Mnara Mahali Ambapo Hakuna Umeme. Kampuni Inayoongoza Kujenga Minara Ya Mawasiliano Hasa Vijijini Ni Celtel. Vodacom Share Kwenye Telecommunication Industry Imeshuka Toka 51% Miezi Michache Iliyopita To 37%. Kwa Kuwa Wanavijiji Wengi Hawalazimiki Tena Kupanda Juu Ya Miti Kupata Matandao Hafifu Wa Voda, Kwani Celtel Wapo Huko Vijijini. Nitawapa Habari Zaidi Nakimbilia Kanisani
 
Kwa bahati mbaya sana, walipa Kodi wazuri wa nchi hii ni Wafanyakazi ambao wanalipa kupitia PAYE, na Wakulima, ambao wanalipa kodi zisizomoja kwa moja. haya m,akundi mawili hayana pa kukwepea. Hicho wanachokilipa ndicho kinachotunisha matumbo ya mafisadi na familia zao. Wakati hawa wanalipa kodi hadi utumbo, wengine ndiyo hawa wanapata likizo ya kutolipa kodi. Najiuliza hivi hii nchi yetu tuifanyeje jamani, tumekuwa kama kwamba wataanzania wote ni mataahira!
 
thanks to DAILY NEWS, HABARI LEO & TBC kwani zinadhihirisha ni for TANZANIA kisha wengine baadaye....!
TIDO KAIBADILI TBC, JE DAILY NEWS/HABARI LEO IMEBADILISHWA NA NANI.....?
 
Bubu ataka kusema,
Hivi kweli watu wenye kipato kidogo wanalipa kodi Tanzania? Naomba uziorodheshe kodi wanazolipa na viwango ili tuanze kuzipigania hapa.
Halafu kuna jambo jingine hapa inabidi tuwe wazi, unapokuwa mfanyabishara lengo lako kubwa ni kupunguza gharama na kuongeza kipato. Kama umeweza kupunguza gharama kama Vodacom basi wewe ni mfanyabishara mzuri. Kwa mawazo yangu hapa wa kulaumiwa ni aliyotoa msamaha huo. Jambo jingine la kuangalia ni faida gani taifa limepata kutokana na msamaha huo wa kodi. Kama Vodacom isingekuwepo taifa lingepata faida gani au hasara gani. Lazima tukumbuke ili kuendelea kiuchumi "communication" is no.1 factor.

Hivi ndivyo watanzania wanavyowajaza mapesa mafisadi

Viwango vilivyokuwa vinatumika
Mapato na kodi kwa mwezi

Shilingi 0 mpaka Shilingi 80,000 -Asilimia sifuri
Shilingi 80,001 mpaka Shilingi 180,000 -Asilimia 15 ya kiasi kinachozidi Shilingi 80,000
Shilingi 180,001 mpaka Shilingi 360,000 -Shilingi 15,000 kuongeza asilimia 20 ya kiasi kinachozidi Shilingi 180,000
Shilingi 360,001 mpaka Shilingi 540,000 - Shilingi 51,000 kuongeza asilimia 25ya kiasi kinachozidi Shilingi 360,000
Zaidi ya Shilingi 540,000 - Shilingi 96,000 kuongeza asilimia 30 ya kiasi kinachozidi Shilingi 540,000

Viwango Vipya
Mapato na kodi kwa mwezi

Shilingi 0 mpaka Shilingi 100,000 - Asilimia sifuri
Shilingi 100,001 mpaka Shilingi 360,000 - Asilimia 15 ya kiasi kinachozidi Shilingi 100,000
Shilingi 360,001 mpaka Shilingi 540,000 - Shilingi 39,000 kuongeza asilimia 20ya kiasi kinachozidi Shilingi 360,000
Shilingi 540,001 mpaka Shilingi 720,000 - Shilingi 75,000 kuongeza asilimia 25ya kiasi kinachozidi Shilingi 540,000
Zaidi ya Shilingi 720,000 - Shilingi 120,000 kuongeza asilimia 30 ya kiasi kinachozidi Shilingi 720,000

Wengine wetu tunalipa kodi mpaka laki tatu na zaidi mtu unashangaa kwa nini kampuni kubwa kama Voda isilipe kodi.
 
kupewa msamaha wakodi nikutokana na watu kuwa na mgongano wa kimaslahi kama utakumbuka kuna kigogo moja alikua bungeni kipindi kilichopita ni mmoja wa wakurugenzi wa voda alipoambiwa achague cheo chake au ukurugenzi alipiga kelele sana sasa mtu huyo ni mkubwa sana katika ccm,kuhusu magazeti angalia matangazo ya voda unaweza kukuta kurasa zaidi yatatu kwa siku moja hakuna mkurugenzi yoyote anaetaka kupoteza biashara hiyo bwana (BANIANI MBAYA LAKINI KIATU CHAKE NI DAWA)
 
Bubu ataka kusema,
Hivi kweli watu wenye kipato kidogo wanalipa kodi Tanzania? Naomba uziorodheshe kodi wanazolipa na viwango ili tuanze kuzipigania hapa.
Halafu kuna jambo jingine hapa inabidi tuwe wazi, unapokuwa mfanyabishara lengo lako kubwa ni kupunguza gharama na kuongeza kipato. Kama umeweza kupunguza gharama kama Vodacom basi wewe ni mfanyabishara mzuri. Kwa mawazo yangu hapa wa kulaumiwa ni aliyotoa msamaha huo. Jambo jingine la kuangalia ni faida gani taifa limepata kutokana na msamaha huo wa kodi. Kama Vodacom isingekuwepo taifa lingepata faida gani au hasara gani. Lazima tukumbuke ili kuendelea kiuchumi "communication" is no.1 factor.

Kwa taarifa yako bidhaa nyingi zinazouzwa kwenye duka la jirani yako huwa tayari zilishatozwa kodi kabla hazijafika hapo dukani. Kwa hiyo bei unayouziwa hapo kila siku is already tax-inclusive, japo wewe hulijui hilo. Sikulaumu sana kwani wewe ni miongoni mwa watanzania wengi wasiojua hilo!

Kwa hiyo watanzania wengi wenye kipato kidodo wakiwemo wazee wako waishio kijijini kwenu hulipa kodi kupitia kila bidhaa wanayonunua dukani na sehemu zinginezo wanunuako mahitaji yao ya kila siku.
 
Back
Top Bottom