kachumbari
Senior Member
- Nov 1, 2010
- 125
- 8
Mimi nina binti kaolewa na ana watoto 2 na wanakaa kwao kwenye nyumba ya yeye na mumewe,mama yuko mko mwingine na wao wako Mkoani lakini anamlalamika mama mkwe wake kila akienda kuwatembelea kwao,anajishughulisha sana,lakini kinachomkera huyu binti yangu ni kwamba imefikia mahali,binti akiwa amekwenda shule(chuoni) yeye anampeleka mtoto wake maji ya kuoga chumbani,anatandika kitanda na imefikia mpaka ana mfulia chupi huyu mume wa mwanangu(Mwanae),hata siku akiwa nyumbani wakipikwa kuku basi atahakikisha kwanza mwanae ndio anapata sehemu za kuku nzuri kuliko wajukuu zake na hizi taarifa anaambiwa na msaidizi wake hapo nyumbani hii inamaanisha nini?Nifanyeje kumsaidia Binti huyu?