Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 58,998
- 103,383
Wakuu waungwana wa JF,
Kama kuna yeyote anayejua anisaidie na wengine wanaotaka kujua kama mimi.
Karibuni wajuzi wa mambo
Muktasari wa Ripoti ya Kamati ya Prof. Osoro unapatikana hapa:
https://www.ikulu.go.tz/files/publications/attachments/2_sw.pdf
Waione: JokaKuu, Mag3 Pascal Mayalla na wengineo
Hawajachukuliwa hatua yoyote na hawatokaa wachukuliwe hatua yoyote maana awamu hii hawapambani na ufisadi, bali wanakomesha matumizi ya neni fisadi. Hujawahi kusikia wanaccm kila wakichangia majukwaani na huku social media wakisema wapinzani wanaendesha siasa za kutukana. Kutukana wanayoiongelea ni hiyo watu kuwaita mafisadi. Kichekesho nilikiona wiki ile ya rais akiwa huko Mara eti alituhumiwa mtendaji wa kata kwamba katumia pesa za kijiji, basi rais na waziri Kange wakaagiza akamatwe eti ndio hayo mafisadi rais anayatafuta!! Halafu wananchi (wanaccm) waliokuwepo wakashangilia kwa nguvu kwamba mafisadi yanashugulikiwa. Ukiona mtu kakamatwa kwa kisingizo cha ufisadi kama sio mpinzani basi jua huko nyuma alikosana na jiwe hivyo anakomolewa.