YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,909
- 51,904
umepigilia msumari penyeweItawaletea shida ya kubaguliwa wanafunzi huko mbele. Syllubus ni moja tu. Labda useme pia kuwa na syllabuses nyingi. Kama ilivyo sasa wale wa intentional schools walivyo na syllabus tofauti na mitihani/watahini tofauti. Localy italeta confusion!
Kama unakubali hoja ya kuwa na syllabus moja kwa nchi, then huwezi kuwa na mitihani zaidi ya mmoja.
Maana lengo la mitihani ni kupima kama kile mwanafunzi anachotakiwa kujua kwa level fulani (syllabus) je anakijua kwa kiwango gani!?
Kama kwa syllabus yetu tunataka mtoto anayemaliza drs 7 ajue kuhesabu na kuandika mpaka 10, huwezi kuwa na vipimo tofauti kwa shule tofauti kwa lengo hilo hilo. Huwezi kupima shule moja kuona kama wanahesabu vizuri mpaka 5 tu na nyingine mpaka 10, halafu wakifuzu wote uwape cheti cha kufuzu darasa la 7. Akija huku kwenye ajira, nianze kumfundisha kuhesabu kuanzia 6-10? Kwa nini nisimchukue ambaye tayari anajua kuhesabu mpaka 10?