Kutumia mtihani mmoja wa Taifa kupima wanafunzi wote sio sahihi, ni upotofu mkubwa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,581
46,176
Mazingira wanayosema wanafunzi wa Tanzania yanatofautiana sana. Wapo wanaosoma shule za huduma zote na wale ambao hata dawati la kukaa bado ni tatizo.

Wapo wanaokwenda shule na kidumu, ufagio, kuni, mbole, maji n.k na wenzao ambao hivyo vitu hawavigusi kabisa.

Wapo ambao shule zao zinahakikisha wanafika shuleni kwa wakati kwa magari ya shule na wengine ambao kufika shule ni juu yao wenye, hata wakitumia ungo ni sawa tu mradi wafike shule.

Kuna wanaokula shuleni na wanaoshinda na njaa, kuna wenye vyoo vya kutosha na wengine ambao vyoo ni vya kugombania.

Wapo ambo kumuona mwalimu wa somo ni sawa na kubeti na wale ambao walimu wa masomo wamejaa tele.

Tofauti ni nyingi sana, zaidi ya milioni moja na kwa namna hiyo hakuna mantiki wala sio sahihi kutumia mtihani mmoja kuwapima wanafunzi wote kwa kipimo kimoja.

Serikali ije na namna tofauti, mbadala ya kuwapima wanafunzi hawa wanaotofautiana mazingira ya kusomea kwa kiwango kikubwa sana ili kupata uhalisia wa uelewa wao na kujua jinsi ya kuwaandaa vyema kwa masomo ya juu zaidi. Tuwatendee haki katika elimu watoto wa maskini wanyonge wa nchi hii.
 
Hakuna haja ya kufanya hivyo. Ndio maana kufaulu kunaanzia divisheni 4. Ingekuwa kufaulu ni divisheni 1 pekee. Kungekuwa na haja ya kuangalia mfumo wa utahini ili jinsi ilivyo ibakie hivyo.

Muhimu serikali izidi kujitahidi kuboresha miundombinu ya kujisomea ili kufikia usawa kwa wote.
 
shule za Kata div 4.......98% , Private div 1=98% halafu unasema div 4 ni ufaulu... siasa hizo hawa watoto hawawezi kushindna kwend from five/ higher education.
Lakini kuna baadhi ya vitu atastahili kuvipata. Tofauti na akifeli kabisa. Io divisheni 4 nimeichukulia generally. Lakini mtu/ mwanafunzi akiwa serious hawezi kushindwa kupata hata divisheni 3 licha ya mazingira magumu.

Mara zingine kufaulu kunategemea na uwezo wa mwanafunzi husika. Kuna shule private ambazo atleast zina huduma za kukidhi baadhi ya mahitaji maalum lakini hazifaulishi kwa kiwango kikubwa.

Muhimu ni serikali kuweka mazingira wezeshi.
 
Hoja zako ni za msingi lakini ufumbuzi uliotoa ni questionable.

Kumbuka kipimo (mtihani) tofauti lazima kiendane na matokeo tofauti na hivyo shule lazima ziwe tofauti baada ya kufaulu mtihani, hivyo utajenga taifa lenye matabaka ya elimu na maisha pia, njia sahihi ya kuepuka jambo hilo ni kujitahidi kuondoa hizo changamoto ulizozitaja katika shule zetu.
 
Mfumo wa mtihani mmoja wa NECTA ufutwe na badala yake shule ziwekwe zinazofanana ziweke katika makundi yanayofanana na mitihani iwe kulingana na uhalisia wa makundi husika.
Taja taifa moja tu duniani linalotumia huo mfumo unaoota hewani?
 
Back
Top Bottom