Kutuma sms zaidi ya 100 inawezekana?

teac kapex

JF-Expert Member
Jan 23, 2011
470
136
Wadau nauliza hivi, nahitaji kuwa natuma sms za matukio ya Kanisa kwa washiriki kama 500 hivi je hii kitu ina gharama zingine tofauti na kifurushi changu cha sms?
Lakini pia nataka nikituma sms iende ikiwa na jina la Kanisa na iwe no reply. Nifanyeje?
 
kwa hivyo haiwezekan mkuu. lazima ukituma meseji itaonesha reply kwa ulio watumia, pia ukituma meseji zikafika mia laini itafungiwa kwa kutokutuma sms.hivyo kama utakuwa maeneo ya karibu ya shop za hii mitandao ungefika ili upate msaada zaidi.
nawasilisha mkuu Mungu awe nanyi katika jambo Leno la kheri
 
Msaada zaidi unahitajika kuhusu hiyo bulk sms bado niko gizani nimejaribu kuingia na kuregister lkn nilipojaribu kutuma msg ikagoma na kusemema insufficient credit
 
Nipe namba PM mtu akucheck sasa hivi, ndio kazi zao.
Bulk SMS, wewe kama wewe huwezi maana ni huduma nyingine tofauti kidogo
 
Kuna watu wanaitwa Bongo live wana package mbalimbali za sms unapewa na portal kabisa ya kutuma meseji.. ukijisajili utaona bei za sms zao kadri unavyonunua sms nyingi ndiyo bei ya sms inavyozidi kushuka. Portal yao ni rahisi kutumia ukitaka ina feature nyingi kama utakavyo wewe unless utake tofauti na hapo.
 
Mkuu mimi natoa hii huduma nimekutumia message na link ya website yangu unaweza kujisajiri na kutuma trial sms km 100
 
Kuna watu wanaitwa Bongo live wana package mbalimbali za sms unapewa na portal kabisa ya kutuma meseji.. ukijisajili utaona bei za sms zao kadri unavyonunua sms nyingi ndiyo bei ya sms inavyozidi kushuka. Portal yao ni rahisi kutumia ukitaka ina feature nyingi kama utakavyo wewe unless utake tofauti na hapo.
Mbona hamuwezi kumuelekeza mtu kitu akaelewa?
Bongo live Ni wapi Ofisi zao ziko wapi ni kitu gani hichi
Je ni app inapatikana wapi unajiungaje na hiyo app ili uweze kupata huduma unayoitaka
Ukitoa maelekezo kwa mtu toa maelezo mtu akuelewe sio unaelejeza juu juu tu mtu hata haelewi
 
Mbona hamuwezi kumuelekeza mtu kitu akaelewa?
Bongo live Ni wapi Ofisi zao ziko wapi ni kitu gani hichi
Je ni app inapatikana wapi unajiungaje na hiyo app ili uweze kupata huduma unayoitaka
Ukitoa maelekezo kwa mtu toa maelezo mtu akuelewe sio unaelejeza juu juu tu mtu hata haelewi
Kama mtumiaji mzuri wa google ukiandika "bongo live" maelekezo yote yapo pale wameweka details zao mkuu, akiona shida apite hapa www.bongolive.co.tz
 
Nilileta hapa jf system ya kusimamia taarifa za kanisa ambayo inaruhusu kutuma bulk SMS, lakini haikupata mwitikio. Nikaamua kuifungia store tuu.
 
Nilileta hapa jf system ya kusimamia taarifa za kanisa ambayo inaruhusu kutuma bulk SMS, lakini haikupata mwitikio. Nikaamua kuifungia store tuu.
Haikupata mwitikio kiaje?..ulikua unaiuza au vp yan?
 
Sikuwa nauza, niliweka free kwa miezi 6, then unalipia kwa mwezi 15,000 tuu.
Okay..ila nadhani ilitakiwa ujue soko lako liko wapi kisha uwekeze nguvu kubwa huko.So ungepata wateja tu kuliko ulivyoamua kuifunga
 
Back
Top Bottom