Shayu
Platinum Member
- May 24, 2011
- 608
- 1,653
Kila Taifa ni lazima liwe na maono yake. Kila Taifa ni lazima lijue linapoelekea. Kila Taifa ni lazima liwe na muongozo na Dira. Matumaini ya Taifa lolote huwa mikononi mwa Viongozi wao ndio wanaamua baadae na historia ya Taifa.
Tatizo tulilonalo ni viongozi walikosa ambition kwa Taifa hili. Hao ndio wanakwamisha juhudi za kuleta maendeleo kwa Taifa hili. Wanachukulia madaraka kama ni sehemu kupata pride ya uongozi na nafasi ya kula lakini sio kuleta mabadiliko kwa watu wa Taifa hili. Hilo ndilo Tatizo tulilonalo.
Viongozi wetu wameridhika na hali iliyopo. Mimi binafsi ningependa tutafakari ni jinsi gani tutalitoa Taifa hili kutoka hapa lilipo.Changamoto hii ya kimawazo ni lazima iwepo kwenye kila kichwa cha mtazania.
Nimeandika mawazo yangu mengi kuongelea jinsi gani tunaweza kuliondoa Taifa hili kutoka hapa lilipo na ninaendelea kutafakari ili kupata majibu sahihi kwa matatizo yetu. Natambua Taifa hili litajengwa na sisi wenyewe kwa nguvu zetu pamoja na akili zetu.
Kitu cha muhimu ni kwamba ni lazima tuunganishe nguvu zetu kukabiliana na changamoto tulizo nazo kama Taifa. Ni lazima tuangalie upya siasa zetu ziwe ni za kujenga nchi na sio siasa maslahi binafsi. Embu turudishe akili zetu pamoja tutafakari kuhusu mustakabali wa nchi hii.
Nchi hii itajengwa na watu wanaotafakari na italindwa na watu wanaotafakari. Kitu gani kinasababisha kuendelea kuwa maskini kama sio tatizo letu la kukataa kuwa wamoja ili tutafakari kwa pamoja matatizo yanayo tukabili? Kuna vitu ambavyo ni muhimu kutafakri ili kuleta nchi yetu katika mstari ulionyooka.
Sitachoka kuwalaumu watawala waliopo kwa kushindwa kuleta utawala wa haki na kusababisha disorder katika jamii yetu. kuruhusu ufisadi na wizi na kusababisha umoja wa Taifa hili kumomonyoka kisha taifa kuwa la watu wabinafsi, la watu wanajifikiria wenyewe na sio baadae yetu.
Ni ukweli usiopingika kwamba CCM wameshindwa kuongoza Taifa hili kuelekea kwenye tija. Nchi inaendelea kuwa tegemezi kwa wahisani na ndoto yetu ya kuwa Taifa lenye kujitegemea haimo miongoni mwa viongozi. Tumetengeneza Taifa la watu wanaoamini katika misaada na sio katika juhudi zetu wenyewe ili kujiletea maendeleo.
Umoja wetu umepotea hili ni lazima tuwalaumu CCM kwa kuondosha umoja na uzalendo wa nchi. Dhambi hii haiwezi kuwatoka. Wameshindwa kuongoza nchi katika utawala wa sheria na maadili kila kitu kimevurugika.
Matumaini ya Taifa hili yamemomonyoka watu wamekata tamaa juu ya maisha na juu ya baadae ya Taifa letu. Viongozi wa CCM , taifa linaharibika wao wanaendelea kustarahe. Taifa limekosa dira sababu ya uongozi wao mbovu.
Hakuna kitu kingine kilichosababisha Taifa hili kuyumba na kukosa mwelekeo zaidi ya uongozi mbovu wa CCM hili halina ubishi. Mtu yeyote mwenye macho anaona. Hili liko dhahiri.
Taifa hili linahitaji mwelekeo na Dira. CCM wameshindwa kuonyesha uongozi katika kila nyanja. Hata kuwapa matumaini watu wa Taifa hili wameshindwa. Hili liko dhahiri hata ukipita barabarani na kuangalia nyuso za watu, hakuna matumaini.
Kuna kutoridhika kwa watu juu ya CCM na uongozi wake, wameshindwa kukidhi matarajio ya wananchi ya Elimu bora, huduma bora za afya na kuleta umoja wa watu wa Taifa hili. Hakuna order makazini watu wamekuwa wezi, wananchi maskini wanateseka.
Watu wowote pale duniani sehemu yeyote ile wana haki ya kuitoa serikali yeyote isiyokidhi matarajio ya watu na kuiweka serikali nyingine itakayoleta tija na matumaini kwa watu.
Na ikiwa serikali yeyoye inawazuia watu wenye kiu ya kuleta maendeleo yao wenyewe kwa ufisadi na wizi watu wao wana haki ya kuiondoa serikali hiyo, serikali ni lazima iwajibike kwa watu wake na si vinginevyo, ni lazima itoe huduma kwa watu wake na si vinginevyo. Kwahiyo watu wakiona serikali imeshindwa kutoa majibu kwa matatizo yao wana haki ya kuitoa serikali hiyo.
Hii ni haki ya kimsingi kabisa kwa raia wowote huru. Watu wa TAIFA hili wasikubali uhuru wao uwekwe rehani na wezi. Taasisi zote zilizoundwa katika Taifa hili ni kwaajili ya kuhudumia wananchi ni taasisi zao, wananchi wana haki nazo. Wana uhuru wa kuhoji uendeshaji wake.
Wana haki ya kupewa majibu sahihi wanapohoji. Wana haki ya kuwaadabisha viongozi wao kama hawako sawasawa. Nguvu hii iko mikononi mwao.
Msipo kemea na kuwaadabisha mapema viongozi mafisadi uhuru wenu utapokonywa na baadae ya Taifa hili itakuwa gizani. Hatua ya kwanza kwa serikali yeyote kuwa ya kiimla ni pale inapokuwa ya kifisadi ni lazima itaanza kuua tu raia wake.
Itawafanya raia watwana. Uhuru wao utapotea. Utawala wowote wa ukandamizaji unaanzia kwenye ufisadi. Kamwe hatutaweza kujenga TAIFA hili kwa siasa za ulaghai hata kidogo. Hatutaweza kujenga Taifa hili katika misingi ya ubinafsi bali katika nguvu ya umoja.
Tunahitaji viongozi wakweli na wazalendo ili kuongoza Taifa hili. Viongozi wenye msimamo watakaoleta dira katika Taifa hili. Tunahitaji viongozi wanaojua wanasimamia nini. Ndipo Taifa hili litakapo pata mwelekeo na matumaini kurudi kwa watanzania. Ni hili tumaini tu litakalo tupa nguvu ya kufanya kazi na kulitumikia Taifa letu.
Wengi wetu matumaini ya Taifa hili kukua yamepotea au kupungua kutokana na viongozi waliopo. Ndoto ya Taifa lazima inyanyuke upya na kutambua kwamba Taifa hili linauwezo wa kukua na kuwa Taifa kubwa kama mengine. Viongozi ambao wamekosa nguvu na courage ya kuliondoa Taifa hili kutoka hapa lilipo ni lazima waondolewa na tuingize nguvu mpya. Ni lazima tujenge elimu bora yenye misingi imara itakayoleta mageuzi katika Taifa hili, ni lazima tujenge uzalendo kwa watu wetu. Hii misingi yote hii CCM wameivunja. Akili zao ziko kwenye kuuibia nchi. Sio umoja wa watu wa Taifa hili wala maendeleo yake.
Kampeni ya kuiondoa CCM madarakani lazima iwe ''reasonable''. Wananchi lazima waelezwe matatizo yaliyosababishwa na CCM na uwezekano wa Taifa hili kubadilika na kuwa bora zaidi bila ya CCM Kuwepo madarakani. Wananchi lazima waambiwe aina ya Taifa tutakalolijenga baada ya kuiondoa CCM lazima wajengewe matumaini ya maisha.
Inaonekana CCM wameshindwa kabisa ku reform chama chao. wangekuwa na hamu ya ku reform chama chao wangemtoa mwenyekiti wa chama chao ambaye nae pia amesemwa sana katika tuhuma mbali mbali lakini pia ameshindwa kukileta chama chake pamoja kuwa chenye nidhamu na maadili. Kwa kukosa mwelekeo kwa CCM na nchi pia imekosa mwelekeo kama Baba wa Taifa alivyosema bila CCM imara nchi yetu itayumba.
Ni lazima tuwe serious katika masuala ya nchi. Ni lazima tuwe serious na ujenzi wa vyama vya kisiasa imara kwakuwa viongozi wetu hutoka humo. Tukiwa na vyama vya siasa ambavyo sio madhubuti nchi yetu itayumba. Ni lazima tujenge vyama vyetu vya siasa katika uzalendo na maadili. Katika masuala ya nchi tusioneane huruma wala kucheka na mtu. Wananchi wana haki ya kuwadhibiti wabunge na serikali yao kwakuwa wao ni watumishi wao na si vinginevyo.
Matatizo yote ya elimu ambayo haijajengwa katika misingi ya kizalendo ambayo itawafanya vijana walitumikie taifa lao, na matatizo mengine ya kiuchumi na kijamii CCM, haiwezi kuepuka lawama kwa nchi yetu kukukosa mwelekeo na kukosa ORDER. Wameshindwa kuonyesha uongozi. Uamuzi ni wa wananchi kuona hali iliyopo na kuchukua hatua.
Kama nilivyosema hatu ya kwanza kwa Taifa lolote kuendelea ni pale raia wanapobadilisha fikra zao kutoka kwenye ubinafsi kuja kwenye Utaifa na uzalendo, na kuijenga nchi yetu kwa pamoja Tofali baada ya tofali.
Katika matumaini haya ya Taifa la watu wamoja na wenye nia moja ni lazima tuishi, tutembee na tukuzwe katika fikra hizi, ya kwamba tunauwezo wa kujenga Taifa hili na kuwa kubwa, na ya kwamba funguo za maendeleo ya Taifa hili ziko mikononi mwetu ni wajibu wetu kufungua au kufunga mlango wa maendeleo. Ni lazima tuamini hivi ama sivyo tutakuwa hatuna nguvu ya kulijenga Taifa hili na ni wajibu wetu kuwekeza nguvu zetu na akili zetu katika kujenga Taifa hili.
Naliona Taifa hili katika macho ya uwezekano, naona tija, Taifa hili linauwezo wa kuwa kama Taifa lolote kubwa ikiwa viongozi na wananchi wakiwa wamoja katika kuleta maendeleo yao wenyewe. Ikiwa tutajenga vyama vyetu vya kisiasa katika maadili na uzalendo. Katika matumaini haya ni lazima tuishi.
Tatizo tulilonalo ni viongozi walikosa ambition kwa Taifa hili. Hao ndio wanakwamisha juhudi za kuleta maendeleo kwa Taifa hili. Wanachukulia madaraka kama ni sehemu kupata pride ya uongozi na nafasi ya kula lakini sio kuleta mabadiliko kwa watu wa Taifa hili. Hilo ndilo Tatizo tulilonalo.
Viongozi wetu wameridhika na hali iliyopo. Mimi binafsi ningependa tutafakari ni jinsi gani tutalitoa Taifa hili kutoka hapa lilipo.Changamoto hii ya kimawazo ni lazima iwepo kwenye kila kichwa cha mtazania.
Nimeandika mawazo yangu mengi kuongelea jinsi gani tunaweza kuliondoa Taifa hili kutoka hapa lilipo na ninaendelea kutafakari ili kupata majibu sahihi kwa matatizo yetu. Natambua Taifa hili litajengwa na sisi wenyewe kwa nguvu zetu pamoja na akili zetu.
Kitu cha muhimu ni kwamba ni lazima tuunganishe nguvu zetu kukabiliana na changamoto tulizo nazo kama Taifa. Ni lazima tuangalie upya siasa zetu ziwe ni za kujenga nchi na sio siasa maslahi binafsi. Embu turudishe akili zetu pamoja tutafakari kuhusu mustakabali wa nchi hii.
Nchi hii itajengwa na watu wanaotafakari na italindwa na watu wanaotafakari. Kitu gani kinasababisha kuendelea kuwa maskini kama sio tatizo letu la kukataa kuwa wamoja ili tutafakari kwa pamoja matatizo yanayo tukabili? Kuna vitu ambavyo ni muhimu kutafakri ili kuleta nchi yetu katika mstari ulionyooka.
Sitachoka kuwalaumu watawala waliopo kwa kushindwa kuleta utawala wa haki na kusababisha disorder katika jamii yetu. kuruhusu ufisadi na wizi na kusababisha umoja wa Taifa hili kumomonyoka kisha taifa kuwa la watu wabinafsi, la watu wanajifikiria wenyewe na sio baadae yetu.
Ni ukweli usiopingika kwamba CCM wameshindwa kuongoza Taifa hili kuelekea kwenye tija. Nchi inaendelea kuwa tegemezi kwa wahisani na ndoto yetu ya kuwa Taifa lenye kujitegemea haimo miongoni mwa viongozi. Tumetengeneza Taifa la watu wanaoamini katika misaada na sio katika juhudi zetu wenyewe ili kujiletea maendeleo.
Umoja wetu umepotea hili ni lazima tuwalaumu CCM kwa kuondosha umoja na uzalendo wa nchi. Dhambi hii haiwezi kuwatoka. Wameshindwa kuongoza nchi katika utawala wa sheria na maadili kila kitu kimevurugika.
Matumaini ya Taifa hili yamemomonyoka watu wamekata tamaa juu ya maisha na juu ya baadae ya Taifa letu. Viongozi wa CCM , taifa linaharibika wao wanaendelea kustarahe. Taifa limekosa dira sababu ya uongozi wao mbovu.
Hakuna kitu kingine kilichosababisha Taifa hili kuyumba na kukosa mwelekeo zaidi ya uongozi mbovu wa CCM hili halina ubishi. Mtu yeyote mwenye macho anaona. Hili liko dhahiri.
Taifa hili linahitaji mwelekeo na Dira. CCM wameshindwa kuonyesha uongozi katika kila nyanja. Hata kuwapa matumaini watu wa Taifa hili wameshindwa. Hili liko dhahiri hata ukipita barabarani na kuangalia nyuso za watu, hakuna matumaini.
Kuna kutoridhika kwa watu juu ya CCM na uongozi wake, wameshindwa kukidhi matarajio ya wananchi ya Elimu bora, huduma bora za afya na kuleta umoja wa watu wa Taifa hili. Hakuna order makazini watu wamekuwa wezi, wananchi maskini wanateseka.
Watu wowote pale duniani sehemu yeyote ile wana haki ya kuitoa serikali yeyote isiyokidhi matarajio ya watu na kuiweka serikali nyingine itakayoleta tija na matumaini kwa watu.
Na ikiwa serikali yeyoye inawazuia watu wenye kiu ya kuleta maendeleo yao wenyewe kwa ufisadi na wizi watu wao wana haki ya kuiondoa serikali hiyo, serikali ni lazima iwajibike kwa watu wake na si vinginevyo, ni lazima itoe huduma kwa watu wake na si vinginevyo. Kwahiyo watu wakiona serikali imeshindwa kutoa majibu kwa matatizo yao wana haki ya kuitoa serikali hiyo.
Hii ni haki ya kimsingi kabisa kwa raia wowote huru. Watu wa TAIFA hili wasikubali uhuru wao uwekwe rehani na wezi. Taasisi zote zilizoundwa katika Taifa hili ni kwaajili ya kuhudumia wananchi ni taasisi zao, wananchi wana haki nazo. Wana uhuru wa kuhoji uendeshaji wake.
Wana haki ya kupewa majibu sahihi wanapohoji. Wana haki ya kuwaadabisha viongozi wao kama hawako sawasawa. Nguvu hii iko mikononi mwao.
Msipo kemea na kuwaadabisha mapema viongozi mafisadi uhuru wenu utapokonywa na baadae ya Taifa hili itakuwa gizani. Hatua ya kwanza kwa serikali yeyote kuwa ya kiimla ni pale inapokuwa ya kifisadi ni lazima itaanza kuua tu raia wake.
Itawafanya raia watwana. Uhuru wao utapotea. Utawala wowote wa ukandamizaji unaanzia kwenye ufisadi. Kamwe hatutaweza kujenga TAIFA hili kwa siasa za ulaghai hata kidogo. Hatutaweza kujenga Taifa hili katika misingi ya ubinafsi bali katika nguvu ya umoja.
Tunahitaji viongozi wakweli na wazalendo ili kuongoza Taifa hili. Viongozi wenye msimamo watakaoleta dira katika Taifa hili. Tunahitaji viongozi wanaojua wanasimamia nini. Ndipo Taifa hili litakapo pata mwelekeo na matumaini kurudi kwa watanzania. Ni hili tumaini tu litakalo tupa nguvu ya kufanya kazi na kulitumikia Taifa letu.
Wengi wetu matumaini ya Taifa hili kukua yamepotea au kupungua kutokana na viongozi waliopo. Ndoto ya Taifa lazima inyanyuke upya na kutambua kwamba Taifa hili linauwezo wa kukua na kuwa Taifa kubwa kama mengine. Viongozi ambao wamekosa nguvu na courage ya kuliondoa Taifa hili kutoka hapa lilipo ni lazima waondolewa na tuingize nguvu mpya. Ni lazima tujenge elimu bora yenye misingi imara itakayoleta mageuzi katika Taifa hili, ni lazima tujenge uzalendo kwa watu wetu. Hii misingi yote hii CCM wameivunja. Akili zao ziko kwenye kuuibia nchi. Sio umoja wa watu wa Taifa hili wala maendeleo yake.
Kampeni ya kuiondoa CCM madarakani lazima iwe ''reasonable''. Wananchi lazima waelezwe matatizo yaliyosababishwa na CCM na uwezekano wa Taifa hili kubadilika na kuwa bora zaidi bila ya CCM Kuwepo madarakani. Wananchi lazima waambiwe aina ya Taifa tutakalolijenga baada ya kuiondoa CCM lazima wajengewe matumaini ya maisha.
Inaonekana CCM wameshindwa kabisa ku reform chama chao. wangekuwa na hamu ya ku reform chama chao wangemtoa mwenyekiti wa chama chao ambaye nae pia amesemwa sana katika tuhuma mbali mbali lakini pia ameshindwa kukileta chama chake pamoja kuwa chenye nidhamu na maadili. Kwa kukosa mwelekeo kwa CCM na nchi pia imekosa mwelekeo kama Baba wa Taifa alivyosema bila CCM imara nchi yetu itayumba.
Ni lazima tuwe serious katika masuala ya nchi. Ni lazima tuwe serious na ujenzi wa vyama vya kisiasa imara kwakuwa viongozi wetu hutoka humo. Tukiwa na vyama vya siasa ambavyo sio madhubuti nchi yetu itayumba. Ni lazima tujenge vyama vyetu vya siasa katika uzalendo na maadili. Katika masuala ya nchi tusioneane huruma wala kucheka na mtu. Wananchi wana haki ya kuwadhibiti wabunge na serikali yao kwakuwa wao ni watumishi wao na si vinginevyo.
Matatizo yote ya elimu ambayo haijajengwa katika misingi ya kizalendo ambayo itawafanya vijana walitumikie taifa lao, na matatizo mengine ya kiuchumi na kijamii CCM, haiwezi kuepuka lawama kwa nchi yetu kukukosa mwelekeo na kukosa ORDER. Wameshindwa kuonyesha uongozi. Uamuzi ni wa wananchi kuona hali iliyopo na kuchukua hatua.
Kama nilivyosema hatu ya kwanza kwa Taifa lolote kuendelea ni pale raia wanapobadilisha fikra zao kutoka kwenye ubinafsi kuja kwenye Utaifa na uzalendo, na kuijenga nchi yetu kwa pamoja Tofali baada ya tofali.
Katika matumaini haya ya Taifa la watu wamoja na wenye nia moja ni lazima tuishi, tutembee na tukuzwe katika fikra hizi, ya kwamba tunauwezo wa kujenga Taifa hili na kuwa kubwa, na ya kwamba funguo za maendeleo ya Taifa hili ziko mikononi mwetu ni wajibu wetu kufungua au kufunga mlango wa maendeleo. Ni lazima tuamini hivi ama sivyo tutakuwa hatuna nguvu ya kulijenga Taifa hili na ni wajibu wetu kuwekeza nguvu zetu na akili zetu katika kujenga Taifa hili.
Naliona Taifa hili katika macho ya uwezekano, naona tija, Taifa hili linauwezo wa kuwa kama Taifa lolote kubwa ikiwa viongozi na wananchi wakiwa wamoja katika kuleta maendeleo yao wenyewe. Ikiwa tutajenga vyama vyetu vya kisiasa katika maadili na uzalendo. Katika matumaini haya ni lazima tuishi.