Kutorushwa kwa hotuba ya Dr. Slaa - TBC yaomba radhi

Selous

JF-Expert Member
Jan 13, 2008
1,325
144
na Amana Nyembo - Tanzania Daima



SHIRIKA la Utangazaji Tanzania (TBC), limeomba radhi kwa kushindwa kurusha matangazo ya moja kwa moja ya kikao cha Bunge la Bajeti, Juni 23, wakati Waziri Kivuli, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Dk. Willibrod Slaa, akisoma hotuba yake.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa TBC, Tido Mhando, alisema, hali hiyo ilisababishwa na matatizo ya kiufundi.

Mhando alisema baada ya tatizo hilo kutokea mafundi walijitahidi kufanya marekebisho kwa muda mrefu lakini hawakufanikiwa, hivyo mitambo ya TBC ilishindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa na kuwakosesha watazamaji wa televisheni hiyo kuangali kikao cha Bunge cha jioni ya siku hiyo wakati kinaanza.

“Juhudi za mafundi zilifanikiwa muda mrefu baadaye, ingawa bado kikao cha Bunge kilikuwa kikiendelea, tuliona si busara kurejesha matangazo hayo kikao kikiwa katikati,” alisema Mhando.

Alisema baada ya tatizo hilo kutatuliwa na mafundi, TBC ilimualika Dk. Slaa katika kipindi cha asubuhi cha Jambo Afrika Jambo Tanzania, ambako aliyazungumzia masuala ya hotuba yake kwa kirefu, pamoja na hotuba yake kutumiwa katika taarifa ya habari ya usiku.

Alisema siku moja kabla ya tukio hilo, matangazo yalikuwa yakikatika lakini hali hiyo ilidhibitiwa mapema na mafundi wa shirika hilo.

Mhando aliwaomba radhi watazamaji wa TBC kwa usumbufu uliojitokeza siku hiyo na siku iliyofuata baada ya kumalizika kwa kikao cha asubuhi, wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokuwa akitoa hotuba yake ya bajeti.

“Matatizo ya kiufundi kwenye mitambo yetu ya kurushia matangazo ya moja kwa moja yameendelea kwa muda mrefu sasa, tuliwajibika kupeleka kifaa kingine cha akiba Dodoma ili kuinusuru hali hiyo na wakati huo huo tumelazimika kumtuma haraka fundi wetu, Kabisi nchini Uingereza ili kukifanyia marekebisho kifaa hicho, hata hivyo kilionekana hakifai na hivyo tukalazimika kununua kipya,” alisema Mhando.

Alisema hawakuwataarifu mapema watazamaji wa TBC kuhusu tatizo hilo kwa sababu walikuwa na matumaini ya kulimaliza tatizo hilo mapema.

Aliwatoa wasiwasi wananchi na wabunge kwa taswira yoyote mbaya iliyojengeka na kuwahakikishia kuwa chombo hicho kiko kwa ajili ya umma wote wa Watanzania na mipango inazidi kufanywa ili kufikisha matangazo yake sehemu zote nchini.
 
Kwa vile kesho ni siku ya haotuba ya habari wanajua fika kuwa swali hilo lingeulizwa , kwa nini siku zote hizo hawakuomba radhi?

Mwezi mzima sasa leo ndio wanakumbuka kwa sababu walijua kuwa kesho watabanwa mbavu na bajeti yao ya habari?
 
Nilikuwa najiuliza imekuwa ni ngumu sana kuomba radhi au hata kutoa maelezo ya nini kilipelekea mpaka hawakuonyesha live? Kumbe kesho wapo kikaangioni!!!!
 
Tido Mhando wacha mambo ya ukerekrtwa huu ni wakati wa uwazi jikubalishe na kazi ya uwana habari jiweke mwaninifu tushachoka kudanganywa.
 
Utengwe tena muda maalumu wajioni na ile hotuba wairushe tena, nzima nzima. Sio kuikata kata. Lakini wapinzani/independent radio nazo ziko wapi?
 
Naambiwa kuwa hotuba ya habari imebadilishwa tuu ghafla kwani kesho ilipaswa kuwa haotuba ya wanawake jinsia na watoto ila ikabadilishwa juzi na kuwekwa hii ya habari sasa sijui ndio kuwafanyia umafia wanahabari na MOAT wasianze kutia presha na kujipanga wanachotaka ama laa , huko mimi sijui.
 
Tido Mhando, pollester wa Mtandao kutoka BBC mchango wake kwa mtandao, ilikuwa kila siku kutoa polls zinazo onyesha kuwa Mtandao na Kikwete ndio wanaotakiwa na wananchi kushika power, baada ya Mkapa,

Zawadi yake kuwa mkurugenzi wa TBC, tukaambiwa sana hapa na wapambe wake jinsi alivyo kichwa na babu kubwa sana na hii fani, sasa leo siku ya hotuba ya shujaa wa taifa Dr. Slaa haipo kwenye luninga, kisa eti sababu za kiufundi, really?

Na hakuna yeyote wa kumuwajibisha si alikuwa anawaridhisha walkiompa kula

Only in Tanzania!
 
Hivi ni kwanini sisi wadanganyika tunyenyekea sana watu kuliko profession zetu? Ukiona kama unatabia hii basi achana na haya mambo, unarudi za BBC au unakaa kama sisi. Hatumo lakini tunavuma.

Huwezi kuwa na mchango kwa taifa kama huwezi kufanya kazi na maamuzi kwa manufaa ya taifa. Na sio lazima umfurahishe Kichwangumu wakati unafanya maamuzi au kazi kwa manufaa ya taifa.

C'mon
 
Hii ni dhambi ya pili Tido anaifanya, baada ya kutukosesha hotuba ile tamu ya Dk. Slaa sasa anatudanganya. Ni uwongo mkubwa!!!! Kwani tetesi zilikuwepo hata kabla ya hotuba kuwa kuna zengwe linatengenezwa ili wasirushe hotuba hiyo. Atuombe radhi kwa kutudanganya
 
Bw. Tido Mhando, pamoja na juhudi zake za kuboresha TBC nafikiri ana wakati mgumu sana kwani nadhani tunakumbuka namna TBC(TvT) ilivyokuwa inahujumiwa huko nyuma mpaka ikaondolewa kwenye ofisi ya PM na kuwa shirika.
Pamoja na hii misukosuko iliyopo (ya kifisadi) lakini bado tumeona TBC wakitupa "live" mambo mbalimbali ya kuumbuana wakubwa. wanajitahidi kwa namna fulani. Kwani pamoja na hivyo hivi vyombo vingine wanazuiwa kuonyesha hayo matangazo?
 
Naambiwa kuwa hotuba ya habari imebadilishwa tuu ghafla kwani kesho ilipaswa kuwa haotuba ya wanawake jinsia na watoto ila ikabadilishwa juzi na kuwekwa hii ya habari sasa sijui ndio kuwafanyia umafia wanahabari na MOAT wasianze kutia presha na kujipanga wanachotaka ama laa , huko mimi sijui.

Kama walitaka kuwakwepa MOAT wamenoa kwa sababu nasikia wameshatia timu Dom.
Nasikia Mkuchika anataka kuwahi China kwenye olympic ndo maana akaomba awahi kusoma hotuba yake
 
janja yao ilikua hajajulikana. sasa hivi waeushe wasirushe chama linasonga kama kawa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom