PMNBuko
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 967
- 154
Katika hali isyo ya kawaida, jamaa fulani hapa mtaani kaamua kutoroka familia yake na kukimbilia kusikojulikana kwa sababu ya ugomvi usioisha ndani ya familia yake, yeye na mke wake wa ndoa. Ameacha nyumba, shamba, biashara yake, mali na watoto. Ameahidi kutorudi kamwe. Aidha, amepoteza laini zake zote. Hataki tena mawasiliano kati yake na familia yake. Tatizo kubwa ni ugomvi wa zaidi ya miaka mitatu hivi kati yake na mke wake. Wote wanatuhumiana kutokuwa waaminifu ndani ya ndoa yao. Mwanamke ni mkali sana, mwanaume ni mkimya kiasi. Anadai siku nyingine mwanamke humtusi usiku kucha. Hugombana kila mara, lakini ugomvi (matusi) haukomi. Mwanamke licha ya kumnyima unyumba mumewe mara kadhaa, hata chakula alikuwa akimpa kwa taabu na saa nyingine kukosa kabisa. Siku moja mwanaume aliamka usiku wa manane, kashika panga ili amchinje mkewe, lakini aliahirisha kwa kuhofia wote kufariki au kufungwa na kuwaacha watoto wakitaabika, aliahirisha azma yake hiyo. Sasa juzi Ijumaa, kaamua kuondoka. Hapatikani. Baba yake, Mama yake na sisi marafiki, tumemshauri asiondoke bila mafanikio.
Je, hiyo ni busara, amelogwa au ni tatizo la kisaikolojia???
Je, hiyo ni busara, amelogwa au ni tatizo la kisaikolojia???