Kutomsikiliza KIKWETE bungeni ni uhaini ama ujasiri?

nimefuatilia matamko na matamshi mbalimbali yaliyotolewa na viongozi wa kisiasa,dini,wanataaluma. Nilichoona ni kuwa watanzania hawaijui katiba wala sheria za nchi yao..?

Pia wengi wanaogopa kukabiliana na changamoto zenye ukweli, ila pia hawapendi kuona viongozi wakielezwa ukweli hadharani kwa kisingizio kuwa ni kuwavunjia heshima .

Yafaa sasa wakajua kuwa hata kwenye mikutano ya un wapo viongozi kama mugabe na rais wa i ran waliwahi kukimbiwa na viongozi wenzao pindi walipoanza kuhutubia,hivyo chilighati na wenzake yafaa wajifunze ukweli huu.

Natoa changamoto -

ni demokrasia..
 
Chiligati hakuna jina lingine la kumtaja zaidi ya Kibaka wa katiba ya nchi yetu, maana ameikumbatia halafu haisomi. Wana ccm wanadanganywa sana. lakini siku wakigundua kuwa wanadanganywa sijui itakuwaje!
 
Nadhani ungebadilisha kichwa cha habari, kina mislead, wale wabunge wa Chadema walitoka bungeni na haina maana ni "Kutomsikiliza KIKWETE", mimi naamini walimsikiliza kupitia luninga.

Walikujulisha kwamba waliangalia runinga?
 
ujasiri wa ajabu,tena kwa nchi km bongo hasa bara kwetu huku ambapo kila ki2 ni ndiyo mzee
 
Nimefuatilia matamko na matamshi mbalimbali yaliyotolewa na viongozi wa kisiasa,dini,wanataaluma. Nilichoona ni kuwa watanzania hawaijui katiba wala sheria za nchi yao..?

PIA wengi wanaogopa kukabiliana na changamoto zenye ukweli, ila pia hawapendi kuona viongozi wakielezwa ukweli hadharani kwa kisingizio kuwa ni kuwavunjia heshima .

Yafaa sasa wakajua kuwa hata kwenye mikutano ya UN wapo viongozi kama mugabe na rais wa I RAN waliwahi kukimbiwa na viongozi wenzao pindi walipoanza kuhutubia,hivyo CHILIGHATI na wenzake yafaa wajifunze ukweli huu.

Natoa changamoto -

Ni wazi chiligati amekosea kuliongelea hili kwani hata kwa maslahi ya CCM ilikuwa vyemawakalidharau kwa kunyamaza kimya...

Kuhusu jumuiya ya kimataifa (UN) ni wazi kama hiyo ni strategy wamepotoka kwani wengi wao hasa wale wenye sauti zenye kusikika hawako upande wa Chadema na wanawaona irresponsible............

Lakini pia Chadema wameonyesha ujasiri uliopotoka kwa maslahi yao na maslahi ya Taifa kwa ujumla...........hasa ukichukulia hali ya mgawanyiko wa kijamii unaotokota hivi sasa......
 
si uhaini,hakuna mahali popote pale panapo mlazimisha mtu yeyote yule kumsikiliza raisi pindi anapohutubia,na tambuwa kuwa unahaki ya kutomsikiliza raisi akiongea ilimradi tu usifunje haki ya mtu mwingine kumsikiliza mkuu wa nchi

nadhani kwa wabunge wa chadema lengo lilikuwa ni kufikisha ujumbe

mapinduziiiii daimaaaa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom