Kutomchagua,kutofika kumwapisha waziri mkuu,sasa chadema mmekomaa kisiasa.

Gsana

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
4,383
1,321
Ndugu wapenda demokrasia,sasa wawakilishi wa watanzania bungeni wameanza kuonekana kutumia haki ya kidemokrasia kukataa kuburuzwa,bali kwa msimamo wa pamoja wa kutokubaliana na udikteta. Ni jambo linalompa fahari mnyonge wa nchi hii aliyekaa juani siku ya kupiga kura alafu akatangazia kile ninachokiita udikteta. Naona msimamo wa watanzania umeanza kuwa wa ukomavu wala si unafiki wa kuwa wapinzani wakati mnasubiri kupeana5 baada ya watanzania kusumbuka kupiga kura. Kwa kitendo cha Cuf kuingia ikulu wakati wafuasi wake walidhani ndo mkombozi wa wanyonge ni usaliti wa hali ya juu. Kumbuka mpaka leo kuna watanzia waliowekwa mahabusu eti walileta fujo wakati wa uchaguzi wakikitetea CUF lakini leo Seif anakaa kupiga picha na ccm akikenua meno na kubadilishana BMW,ni usaliti. Chadema kaeni mkijua mpo bungeni kutuwakilisha wanyonge,dai haki mpaka mwisho. Jioni pia kaeni nje ya bunge mbele ya luninga mkisikiliza Mwenyekiti wa Ccm akihutubia kikao cha bunge cha ccm. Hamna mapigano,vita wala vurugu kufanyika ila peaceful democracy should be unveiled. Waache mafisadi na wendawazimu wawashangae ila wanademokrasia wanaelewa. Hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
Back
Top Bottom