Kutokuwa na Civil War kumesababisha wa-Tanzania kuwa watu wenye amani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,267
Jana nilikuwa ninasafiri nilikaa kiti kimoja na mkaka wa ki-Nigeria katika maongezi aliniambia alikuja Tanzania kwa shughuli za biashara. Ukarimu aliokutana nao Tanzania anasema hata usahau. Kila aliyekutana nae alikuwa mcheshi na mkarimu.

Anasema gharama za hoteli alizojipigia kwa wiki mbili hakulipa kwani wenyeji wake walimkaribisha nyumbani kula na kulala bure kwa wiki mbili.

Mwisho alisema nyinyi mna amani kwakuwa hamjapigana vita ya wenyewe kwa wenyewe. Je kuna ukweli hapa?
 
Ukweli ndio huo ila amani kwenye njaa haitadumu kila miaka
Ninadhani hizi taarifa za ubadhirifu na ufisadi zinazifikia watu kwa njia ya mass communication hazitaiacha amani hii salama ukizingatia watu wameshakata tamaa ya maisha
 
Ninadhani hizi taarifa za ubadhirifu na ufisadi zinazifikia watu kwa njia ya mass communication hairatyacha salama ukizingatia watu wameshakata tamaa ya maisha
Ukweli ndio huo mkuu watu washachoka ila wanavuta muda tu
 
Kupigana wenyewe kwa wenyewe inaweza kuwa kiashirio cha kuchukiana. Upendo baina yetu, tunauonesha hata kwa wageni.
 
Kitu kinachoweza kusababisha watu kupigana ni aidha DINI au KABILA, Kwa kabila Tanzania haiwezekani labda mtu atumie dini ingawa pia siyo rahisi kulingana na misingi iliyowekwa
 
Jana nilikuwa ninasafiri nilikaa kiti kimoja na mkaka wa ki-Nigeria katika maongezi aliniambia alikuja Tanzania kwa shughuli za biashara. Ukarimu aliokutana nao Tanzania anasema hata usahau. Kila aliyekutana nae alikuwa mcheshi na mkarimu.

Anasema gharama za hoteli alizojipigia kwa wiki mbili hakulipa kwani wenyeji wake walimkaribisha nyumbani kula na kulala bure kwa wiki mbili.

Mwisho alisema nyinyi mna amani kwakuwa hamjapigana vita ya wenyewe kwa wenyewe. Je kuna ukweli hapa?
Naona ulisahau kumwambia kwamba si Tanzania yote yenye amani
Mkuranga na Rufiji ni kama Maiduguri (Northern Nigeria) kuna snipers wa hatari hadi raia kulazimika kulala saa kumi na mbili
Teh! Teh! Teh!
 
Tumshukuru Mungu kwa kutopigana wenyewe kwa wenyewe.
Lakini vita tuliyonayo haiwezi kutuacha salama.
 
Kutokupigana ndio amani yenyewe kwa sababu tuliishi kwa amani na upendo toka zamani na hatukupenda kusuluhisha matatizo yetu kwa vita. Ndio maana tuna amani hadi leo
 
Jana nilikuwa ninasafiri nilikaa kiti kimoja na mkaka wa ki-Nigeria katika maongezi aliniambia alikuja Tanzania kwa shughuli za biashara. Ukarimu aliokutana nao Tanzania anasema hata usahau. Kila aliyekutana nae alikuwa mcheshi na mkarimu.

Anasema gharama za hoteli alizojipigia kwa wiki mbili hakulipa kwani wenyeji wake walimkaribisha nyumbani kula na kulala bure kwa wiki mbili.

Mwisho alisema nyinyi mna amani kwakuwa hamjapigana vita ya wenyewe kwa wenyewe. Je kuna ukweli hapa?

ni kweli, hata kuto endelea pia ni kwa sababu hatujawahi kupigana!!

huwezi kukuta mahali lichama lina tuhuma zote zote zote za nchi hii, bado wakaendelea kutembea mtaani na nguo za kijani na njano!! nakuambia hata Yanga wangebadili rangi ya jezi yao
 
ni kweli, hata kuto endelea pia ni kwa sababu hatujawahi kupigana!!

huwezi kukuta mahali lichama lina tuhuma zote zote zote za nchi hii, bado wakaendelea kutembea mtaani na nguo za kijani na njano!! nakuambia hata Yanga wangebadili rangi ya jezi yao
Na wezi wana guts ya kutuita wapumbavu na malofa
 
Kitu kinachoweza kusababisha watu kupigana ni aidha DINI au KABILA, Kwa kabila Tanzania haiwezekani labda mtu atumie dini ingawa pia siyo rahisi kulingana na misingi iliyowekwa
Mkaruka,

Kuna kabila baya sana Tanzania sasa hivi, hili lina uhai wa miaka kama miaka 40 hivi hapa Tanzania . .

Hila kabila ndio linalotawala sasa, na haliamini mtu yeyote nje ya kabila lao kuwa anaweza kuongozaTanzania . . KABILA HILI NDIO LIMEJIFANYA KATIBA YA NCHI . . !

Lakini pia kabila hili ndilo linalochochea utengano, udini, na ukabila.
Hila kabila kwa kufikiri Tanzania ni mali yao, limegawa kwa wageni (wao wanawaita WAWEKEZAJI) bure (dhahabu, gesi, chuma, mafuta etc) rasilimali za watanzania . .

Nakwambieni wana JF, bila kuling'oa hili kabila ktk kutawala, MACHAFUKO HAYAEPUKIKI . . !
 
Back
Top Bottom