Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mabingwa wa nchi ya Tanzania Simba Sports Club leo Agosti 4, 2018 imechapa bila huruma F.C.E. Ksaifa mabao 3-1 katika mchezo safi wa kirafiki uliofanyika kwenye dimba la Kartepe Green Park.
Simba ikionyesha kandanda safi na la kuvutia kwenye mchezo huo, ilikuwa ya kwanza kuandika bao kupitia kwa Emmanuel Okwi katika dakika ya 16' kipindi cha kwanza bao lililodumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Emmanuel Okwi aliipatia tena bao Simba dakika ya 50' ambapo lilidumu kwa dakika 4 tu baada ya F.C.E. Ksaifa kuandika bao lao la kwanza katika dakika 54 kupitia kwa mchezaji Nader Al-krinsui.
Mshambuliaji matata Meddie Kagere alihitimisha ukurasa wa mabao katika dakika ya 87' akifunga bao la tatu, hivyo mchezo huo kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi huo mnono wa mabao 3 dhidi ya bao 1 la F.C.E. Ksaifa.
Simba ikionyesha kandanda safi na la kuvutia kwenye mchezo huo, ilikuwa ya kwanza kuandika bao kupitia kwa Emmanuel Okwi katika dakika ya 16' kipindi cha kwanza bao lililodumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Emmanuel Okwi aliipatia tena bao Simba dakika ya 50' ambapo lilidumu kwa dakika 4 tu baada ya F.C.E. Ksaifa kuandika bao lao la kwanza katika dakika 54 kupitia kwa mchezaji Nader Al-krinsui.
Mshambuliaji matata Meddie Kagere alihitimisha ukurasa wa mabao katika dakika ya 87' akifunga bao la tatu, hivyo mchezo huo kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi huo mnono wa mabao 3 dhidi ya bao 1 la F.C.E. Ksaifa.