Kutoka TANESCO: Taarifa kwa vyombo vya habari

...watu ambao baada ya kukatiwa umeme kwa kile walichoona ni uonevu wameamua kutafuta njia mbadala kama solar n.k.

Watanzania ambao bado wanahangaika kutawala nishati ya mkaa na mafuta ya taa hawana anasa ya nishati mbadala ya jua, umeishi wapi we mja? Ni mtu aliye nje ya mguso tu ndie anaweza kudai hilo. Ijue jamii ya watu unayoiongelea kabla ya kuoni njozi. Baada ya kudai kwamba kutoa umeme bure kutawaongezea TANESCO mapato unaendelea kufyatua mchemko mwingine.

Kusema kumkatia mtu umeme si jawabu hakuna maana kuwa wampe umeme bure.

Mtu halipi, hajalipa daima, unasema aendelee kupewa umeme, maana yake apewe bure!

Umedai kukatia watu umeme hakutawaongezea TANESCO mapato. Ukiwapa bure ndio utawaongezea mapato? Nani huwa anaendelea kukopesha mtu ambae halipi? Kweli hujambo we ndugu? Kampuni inapokata huduma kushurutisha ulipaji na kukosa mapato ya ankara hizo ni heri kuliko kuendelea kutoa umeme bure, itakula kwao TANESCO!

Unaweza uka assume mambo mpaka ng'ombe warudi zizini lakini huwezi kutumia assumption 1) kutoa hitimisho 2) kukosoa watu/idara. Hujafanya tafiti kujua kwamba sababu ya wateja kutolipa umeme ni makarani wa TANESCO kutopokea malipo haraka. Huwezi ku assume kwamba mteja akiendelea kulimbikizwa deni ndio atashika dini na kukimbia kulipa, hujui hilo, ni kukosoa kiholela, utapelea.

Hayo mengine ya mimi kuwa "fools," "juvenile" asiyefikiri na ushauri wa maisha sikuyapa taadhima kwa sababu nimekuachia wewe kaka.
 
Watanzania ambao bado wanahangaika kutawala nishati ya mkaa na mafuta ya taa hawana anasa ya nishati mbadala ya jua, umeishi wapi we mja? Ni mtu aliye nje ya mguso tu ndie anaweza kudai hilo. Ijue jamii ya watu unayoiongelea kabla ya kuoni njozi. Baada ya kudai kwamba kutoa umeme bure kutawaongezea TANESCO mapato unaendelea kufyatua mchemko mwingine.

Nilichosema mimi ni hiki hapa chini. Umeondoa neno WAKO halafu ukajifanya haukuona neno NA KADHALIKA! Selective editing ili ujenge hoja mahali ambapo hapana hoja. Ndiyo maana naita arguments zako ni juvenile.

Wako watu ambao baada ya kukatiwa umeme kwa kile walichoona ni uonevu wameamua kutafuta njia mbadala kama solar n.k.

Umeme unachangia 0.6% tu ya mahitaji ya nishati ya Tanzania. Ni households 286,000 pekee ndiyo zina umeme Tanzania na sehemu kubwa ziko mijini. Chini ya 2% ya watanzania wanaoishi vijini ndiyo wana access na umeme , zaidi ya 98% hawana. Nusu ya production ya umeme Tanzania inatumiwa na viwanda na sehemu za biashara, ni nusu tu ndiyo inayotumika majumbani. Kwa hiyo kusema watumiaji wote wa wa umeme hawawezi kutafuta njia mbadala ni upotoshaji. Wenye viwanda vikubwa kama Tanga Cement baada ya kukorofishana na Tanesco na kutokana na umeme usio na uhakika wametafuta vyanzo mbadala. Wafanya biashara na watumiaji wakubwa wa umeme majumbani wana jenereta. Hizi zote ni vyanzo mbadala. Watumiaji wa umeme wadogo nao wengi wao wamepunguza matumizi yao na kutumia vyanzo kama kuni, mkaa n.k. kupikia vitu kama maharage majumbani. Yote haya ni kutafuta njia mbadala. Wengine wameweka solar panels kwa ajili ya security lights zao. Watu wengi wanatumia umeme kwa ajili ya mwangaza tu. Ukilinganisha gharama ya kuunganisha umeme, bei ya solar panel kwa mahitaji yao ni competitive. Watanzania wanatumia 25-50% ya mapato yao kwa ajili ya nishati ukilinganisha na 2-7% anayotumia aishie ulaya. Ukweli ni kuwa wanaotumia umeme Tanzania ni sehemu ndogo sana ya population yake. Tanesco wanapaswa kupanga mikakati ya kupanua wigo la watumiaji badala ya kufanya kampeni za kukusanya madeni! Kukusanya madeni ni wajib, hakuhitaji kampeni.

Mtu halipi, hajalipa daima, unasema aendelee kupewa umeme, maana yake apewe bure!


Mtu ambae hajalipa daima hawezi kuwa na deni na Tanesco maana hauunganishiwi umeme kabla ya kulipa. Mtu anayetumia umeme bure kama unavyodai ni mtu aliyejiunganishia kinyume cha taratibu. Huyu ni mhalifu, hastahili kampeni.
Si wote hawalipi kutokana na kiburi. Wako wengi wana migogoro na Tanesco ndiyo maana hawalipi. Kubambikiwa bili, matatizo ya umeme kuwaharibia vyombo vyao n.k. Kuwakatia umeme kabla ya kujaribu kutatua kero zao si biashara nzuri. Watu ambao hawalipi kutokana na kiburi ni taasisi za serikali. Hizi ndizo zilizolimbikiza madeni makubwa wakijua kuwa tanesco haina ubavu wa kuwakatia. Hawa nao hawaitaji kampeni bali kupelekwa mahakamani. Tanesco wana ubavu huo? Badal yake watafukuzana na watumiaji wa kawaida wa majumbani ambao wana videni uchwara!

Umedai kukatia watu umeme hakutawaongezea TANESCO mapato. Ukiwapa bure ndio utawaongezea mapato? Nani huwa anaendelea kukopesha mtu ambae halipi? Kweli hujambo we ndugu? Kampuni inapokata huduma kushurutisha ulipaji na kukosa mapato ya ankara hizo ni heri kuliko kuendelea kutoa umeme bure, itakula kwao TANESCO!

Mwenye matatizo ni wewe, bwana mdogo. Nionyeshe niliposema kuwa watu wapewe umeme bure! Nilichosema ni kuwa kukatia watu umeme HAKUTAWAONGEZEA mapato TANESCO. Wewe ujuae kila kitu basi nieleze namna ambavyo kumkatia mtu umeme kutawaongezea mapato Tanesco. Kinachotakiwa ni kutafuta namna ya kuwafanya watu walipe madeni yao yaliyo halali na kuendelea kuwa wateja wa TANESCO. Kukata umeme kunatakiwa kuwa hatua ya mwisho. Mtu unayemkatia umeme anapaswa kuwa yule ambae biashara yake hauitaki tena na uko tayari kumpeleka Mahakamani. Kumkatia mtu umeme ati kwa sababu hajalipa mwezi mmoja au kwa sababu hakuweza kuwaonyesha risiti yake ya malipo ya mwezi huu ( yanatokea) ni upuuzi wa hali ya juu. Ni mawazo finyu kama haya ndiyo yaliyowafanya kumkatia umeme mteja anayelipa mamia ya mamilioni kwa mwezi kwa ajili ya deni la sh milioni 49! Tuseme kama asingeingilia Chairman wa bodi kuwarudishia umeme na Tanga Cement wangekaa bila umeme wiki moja tu, Tanesco wangekuwa wamejiongezeaje mapato? Na wengi kama hawa wako. Tanesco badala ya kuangalia namna gani ya kuboresha huduma zao kwao wao wanakazania madeni! Mchango wa Tanesco katika uzalishaji mbovu wa viwanda vyetu hata siku moja hawauzungumzi
i.

Unaweza uka assume mambo mpaka ng'ombe warudi zizini lakini huwezi kutumia assumption 1) kutoa hitimisho 2) kukosoa watu/idara. Hujafanya tafiti kujua kwamba sababu ya wateja kutolipa umeme ni makarani wa TANESCO kutopokea malipo haraka. Huwezi ku assume kwamba mteja akiendelea kulimbikizwa deni ndio atashika dini na kukimbia kulipa, hujui hilo, ni kukosoa kiholela, unakuwa umepelea

Kweli kwenda shule si lazima kuelimika. Wapi nimesema kuwa sababu ya wateja kutolipa madeni ni makarani wa Tanesco kutopokea malipo haraka? Kuweko kwa foleni si lazima kuwe ni kutokana na uzembe kiutendaji (kutopokea malipo haraka) wa makarani. Inawezekana kabisa kuwa makarani hawatoshi, wako wachache. Inawezekana sehemu za kulipia ziko chache kulingana na mahitaji. Yote haya ulipaswa kuyafikiria kabla ya kuniwekea maneno kinywani ati kwa sababu nimesema kuna ugumu katika kulipia umeme tanesco ninamaanisha kuwa makarani ni wavivu! hapa wengine wamesema kuwa hata kulipa Luku ( ambapo mteja anaikopesha Tanesco kwa kulipia huduma ambayo hajaipata bado) nako kuna wakati kuna matatizo, unaambiwa system iko down, usubiri. Hapa napo tumlaumu karani? Kweli mzima wewe?

Kumuachia mteja alimbkize deni hadi jawabu pekee ni kumkatia umeme ni dalili ya uzembe wa mtoa huduma. Kwa nini hawakufanya jitiada wakati deni bado changa? Kwa nini wamesubiri mpaka mteja ageuke kuwa mdeni sugu? Hakuna cha assumption hapa. Nimekuwa mteja wa Tanesco muda mrefu na ninazungumzia experience. Katika hilo la kulipa deni, zote ni assumption. Una hakika gani kuwa ukimkatia mtu umeme ndiyo atalipa deni? Ingekuwa hivyo basi pasingekuwa na haja ya hizi kampeni za mara kwa mara maana baada ya kukatiwa mara moja basi mteja angeshika dini na kutolimbikiza madeni tena! Huu si ubishi tu wa ili mradi kubisha? Hakuna mahali ambapo ulipopinga hoja zangu kwa hoja bali kwa kupindisha maneno yangu na kuingiza vi-assumption vyako visivyo na maana!

Nimejaribu kukujibu kwa kadri ya uwezo wangu lakini kama hautakuwa na jipya sitaendellea kubisha nawe maana tutakuwa tunawaharibia wasomaji wengie.

Amandla......
 
Kweli kwenda shule si lazima kuelimika....Wewe ujuae kila kitu basi...naita arguments zako ni juvenile...Mwenye matatizo ni wewe, bwana mdogo. ... ...Kweli mzima wewe?

Nini kimekufanya udhani kwamba huyu Tindikali kaenda shule?

Na nimesomea nini, umeme? Haha haha a aaaaaaaaa......Unasema mimi si mzima, mara najua kila kitu, halafu argument zangu za bwana mdogo "juvenile"...Unachanganya sana sumu!

Mwisho wa siku umechemka kudai kwamba kukata umeme hakuongezi mapato. Kuendelea kutoa bure pia hakuongezi mapato. Kukata umeme ni hatua ya mwisho lakini hatujui, hatuwezi ku assume, kwamba TANESCO watakata kama hatua ya kwanza. Kukatia mtu umeme hakumaanishi humtaki tena, ni njia ya kumshurutisha kulipa.

Mfano wa Tanga Cement nao umepelea: Umedai deni lao halikuhalalisha kukatiwa umeme kwa sababu lilikuwa ni mil 49 tu. Na msingi wa hoja yako ni kwamba TANESCO wasikimbilie kukata umeme. Lakini umehoji kwa nini TANESCO wasubiri mpaka mteja awe mdeni sugu. Kwa hiyo ningetegemea ufurahi kwamba huyu Tanga Cement walimuwahi kabla deni halijakua. Sijui unanielewa we Athumani? Ndio maana mara nyingi unayooni yana michanganyo, unahukumu wakifanya, unahukumu wasipofanya.

Wawekezaji na wanasayansi wa dunia ya kwanza wanakiri kwamba hawajagundua njia mpya, bado hawajaweza kutawala vyanzo mbadala vya nishati kama jua, hivyo kusema Watanzania wanaweza kumudu hizo njia ni kutoelewa ukweli: Sikia chanzo hiki. Kwa sasa nishati ya TANESCO ndio tegemeo la Watanzania, hii ni pamoja na hao 98% ambao wanasubiri hiyo ndoto. Hawafikirii visahani vya kunasa jua!

Umedai ulikuwa unachukua siku nzima kubembeleza TANESCO wapokee hela zako. Sasa nimepindisha nini kusema ume assume kwamba makarani kutopokea malipo haraka ndio tatizo? Umebembeleza siku nzima, kwa hiyo wahusika hawakuchukua malipo yako haraka, wawe wamepungua, iwe foleni, wawe wanataka cha juu, vyovyote vile hawakuchukua malipo haraka. Hiki ni Kifipa? Unataka mivutano wa viima na viarifu? Ambayo unasema ni ya vijana? Unajua kaka, unapenda kujivisha taswira ya utu uzima na kushauri wengine mahala pa kwenda maishani lakini una chembechembe za namna zile zile za wale wale unazoziita "juvenile," jichunguze.

Na si kweli, au angalau hatujui, na hatuwezi ku assume, kwamba watumiaji umeme wengi matumizi yao ni taa tu na kwamba visahani vya kunasa jua vitakuwa nafuu zaidi na, au, vingetosha. Kijijini kwetu ni moja ya maeneo ya Tanzania yenye bahati ya kufikwa umeme. Bibi yangu ndani ana pasi ya umeme, ana chagi simu yake, ana ka runinga kake kakuukuu. Matumizi yake ni zaidi ya taa, bado anategemea TANESCO. Na mijini uswahilini kwa sisi wa hali ya chini na kawaida si ajabu kabisa kuwa na mi tarakishi na mijokofu na wengine nimeona mpaka wana ma viyoyozi, uswazi. Tunahitaji TANESCO, sio jua la kuwashia taa. Kushurutisha ulipiaji kwa kukata umeme ni njia iliyo vitabuni mwa watoa huduma wote duniani. Kama ulivyoahidi, nadhani hutaendeleza mabishano.
 
Nini kimekufanya udhani kwamba huyu Tindikali kaenda shule?

Na nimesomea nini, umeme? Haha haha a aaaaaaaaa......Unasema mimi si mzima, mara najua kila kitu, halafu argument zangu za bwana mdogo "juvenile"...Unachanganya sana sumu!

Don't flatter yourself! Sijakuita msomi, nimesema umeenda shule. Hata ngumbalu ni shule. Kwa vile natumaini unajua kuandika basi inadhihirisha uliingia darasani. Ulikoishia sijui wala sina haja ya kujua. Kujifanya unajua kila kitu SI kujua kila kitu. Na ndiyo, arguments zako ni juvenile. Na juvenile ni bwanamdogo hakuna cha bwana mdogo juvenile. Si sumu, ni ukweli.

Mwisho wa siku umechemka kudai kwamba kukata umeme hakuongezi mapato. Kuendelea kutoa bure pia hakuongezi mapato. Kukata umeme ni hatua ya mwisho lakini hatujui, hatuwezi ku assume, kwamba TANESCO watakata kama hatua ya kwanza. Kukatia mtu umeme hakumaanishi humtaki tena, ni njia ya kumshurutisha kulipa.

Naona unaamini kuwa ukisema uongo mara nyingi utageuka ukweli. Wapi niliposema Tanesco watoe umeme bure? Maana ya bure ni kuwa hauhitajiki kulipa. Kukopeshwa umeme si kutoa bure. Unapomkatia umeme sehemu yake ya kumuingizia kipato unamshurutisha vipi kulipa deni ambalo hakubaliani nalo? Ubabe wa namna hii ndiyo dalili ya kuwa hauhitaji biashara yake. Ungekuwa unahitaji biashara yake, ungekaa nae kwanza kujaribu kutatua tatizo kabla ya kumkatia umeme. Dhana ya lipa kwanza ndiyo tujadiliane si dhana ya mtu ambae yupo tayari kumsikiliza mwenzie. Na hii dhana imetawala Tanesco.

Mfano wa Tanga Cement nao umepelea: Umedai deni lao halikuhalalisha kukatiwa umeme kwa sababu lilikuwa ni mil 49 tu. Na msingi wa hoja yako ni kwamba TANESCO wasikimbilie kukata umeme. Lakini umehoji kwa nini TANESCO wasubiri mpaka mteja awe mdeni sugu. Kwa hiyo ningetegemea ufurahi kwamba huyu Tanga Cement walimuwahi kabla deni halijakua. Sijui unanielewa we Athumani? Ndio maana mara nyingi unayooni yana michanganyo, unahukumu wakifanya, unahukumu wasipofanya.

Umepelea kwa vile wewe umesema? Tanga Cement alikuwa analipa mamia ya mamilioni kwa mwezi. Hakuna mahali ambapo hata hao Tanesco walisema kuwa ni mdaiwa sugu. Hiyo milioni 49 ilikuwa ni sehemu ya bili ambayo walikuwa na tatizo nayo ( wengi wetu tuna experience ya Tanesco kubambikia bili). Nyingine walilipa. Kukataa kujadiliana nae wakati anaendelea kutumia umeme wa mamia ya mamilioni ni upuuzi wa hali ya juu. Kilichotokea ni Tanga Cement kutambua kuwa kwa Tanesco hakuna tija na kuwekeza kwenye njia mbadala. Hawa wakiwa na chanzo chao kinachowapa nishati ya uhakika na kujitoa kwenye wigo wa tanesco atakae kula hasara nani? Kama kweli tanesco wanaona kukata umeme ni njia sahihi ya kushurutisha madeni mbona hawawakatii wadeni wao sugu na wagubwa ambao ni taasisi za serikali! Badala yake wanaandama vidagaa na watu ambao wana rekodi nzuri ya kuwalipa! Na wewe unawatetea!

Wawekezaji na wanasayansi wa dunia ya kwanza wanakiri kwamba hawajagundua njia mpya, bado hawajaweza kutawala vyanzo mbadala vya nishati kama jua, hivyo kusema Watanzania wanaweza kumudu hizo njia ni kutoelewa ukweli: Sikia chanzo hiki. Kwa sasa nishati ya TANESCO ndio tegemeo la Watanzania, hii ni pamoja na hao 98% ambao wanasubiri hiyo ndoto. Hawafikirii visahani vya kunasa jua

Unadanganya tena. Njia mbadala zipo na zinajulikana, jua ni mojawapo tu. Kuna upepo, mawimbi, bio-mass ( bagasse, chembe ndogo zote za miti n.k). Uwezo wa kutawala vyanzo hivi nao upo. Kinachogomba ni kushindana na bei ya vyanzo vichafu. Pamoja na hayo, nchi nyingine kama Abu Dhabi wanajenga miji kama Masdar City (angalia hapa MASDAR - Abu Dhabi National Energy, Global Energy Company UAE, Polycrystalline UAE, Industries UAE, Energy Prize Dubai UAE, Monocrystalline UAE. )ambao itatumia nishati safi na endelevu kwa kiasi kikubwa. China wanajenga Dongtan Eco-City wenye madhumuni hayo hayo. Marekani wako nyuma sana katika nyanja hii.

Huyo Bill Gates uliyemweka anazungumzia uwezekano wa nishati endelevu kukidhi mahitaji ya Marekani! Mahitaji yetu watanzania ya umeme ya mwaka mzima ni sawa na mahitaji ya kamji kadogo huko Marekani ( na theluthi ndogo tuu ya mji kama Masdar). Sisi hatuhitaji hizo large scale energy projects anazozingumzia Bill Gates. Pili, marekani si mojawapo ya nchi ambazo zimewekeza na zinazotambulika kuwa wako mstari wa mbele katika kuendeleza nishati endelevu. hivyo kuwatumia kama mfano ni upotoshaji mwingine. Pamoja na Abu Dhabi na China, nchi kama Sweden, Denmark, Ujerumani wanawekeza kwa kiasi kikubwa kwenye nishati endelevu na huko ndiko tunakoweza kujifunza.

Na si kweli, au angalau hatujui, na hatuwezi ku assume, kwamba watumiaji umeme wengi matumizi yao ni taa tu na kwamba visahani vya kunasa jua vitakuwa nafuu zaidi na, au, vingetosha. Kijijini kwetu ni moja ya maeneo ya Tanzania yenye bahati ya kufikwa umeme. Bibi yangu ndani ana pasi ya umeme, ana chagi simu yake, ana ka runinga kake kakuukuu. Matumizi yake ni zaidi ya taa, bado anategemea TANESCO. Na mijini uswahilini kwa sisi wa hali ya chini na kawaida si ajabu kabisa kuwa na mi tarakishi na mijokofu na wengine nimeona mpaka wana ma viyoyozi, uswazi. Tunahitaji TANESCO, sio jua la kuwashia taa. Kushurutisha ulipiaji kwa kukata umeme ni njia iliyo vitabuni mwa watoa huduma wote duniani. Kama ulivyoahidi, nadhani hutaendeleza mabishano.

Bibi yako si mtumiaji wa kawaida wa umeme. Haujaishi uswahilini. Ingawa wako watu wenye majokofu, luninga, viyoyozi n.k. hawa si asilimia kubwa. Ingekuwa hivyo basi luninga isingekuwa dili wakati wa world cup. Maji ya baridi na aiskilimu isingekuwa dili maana wengi wana majokofu. Watu wasingekaa nje wakati wa joto kwa sababu wengi wana viyoyozi! Huu ni mfano wa ubishano wako, wa kuchukua mfano wa jirani yako au bibi yako na ku-extrapolate kwa wote. Maisha ya mkaazi wa kawaida wa mijini mwetu ambapo asilimia kubwa mno inaishi huko uswazi ni magumu. Kuzungumzia jokofu, kiyoyozi n.k. ni ndoto za alinacha.

Unasema kukata umeme ni njia iliyo vitabuni mwa watoa huduma wote duniani bila kutoa mifano. Nimetembelea nchiza kaskazini mwa ulaya na sijasikia hata siku moja mtu ana katiwa umeme. Tofauti na unavyotaka tuamini, kumkatia umeme ni hatua ya mwisho, ni dalili ya kukata tamaa. Tanesco wanaitumia kama ndiyo hatua ya kwanza. Mazoea ni kuwa katika hiki wanachoita kampeni ni hata mteja ambaye amechelewa kwenda kulipa (pengine alikuwa safarini) wanamkatia umeme. Tanesco wenyewe walikiri kuwa Tanga Cement alikuwa ni mlipaji mzuri na walichokuwa wakigombea ni sehemu tu ya bili ambayo walitofautiana. Asingekuwa mlipaji mzuri basi deni lingekuwa mamia ya mamilioni maana hayo ndiyo matumiazi yake kwa mwezi! Kumkatia umeme mtu ambaye historia yake inaonyesha kuwa ni mlipaji mzuri si biashara nzuri. Hasa ukizingatia umeme si bdhaa ambayo utaweza kumyang'anya mmoja ukampa mwingine.

Jisemee mwenyewe unaposema kuwa unahitaji Tanesco. Wako wengi walioisha fanya uamuzi wa kutumia Sola na faida yake wanaiona!

Amandla.......
 
Back
Top Bottom