Kutoka Singida hadi Dar es Salaam kwa matumaini ya kupata msaada wa elimu

Inaendelea.....

Baada ya kurudisha mahari yangu na kuchukua Pete yangu, nilikaa Kama miezi 6 hivi nikapata mdada mmoja huko Arusha mmeru Fulani hivi akiwa ndio kamaliza chuo tukaongea akaniomba kwanza nimtafutie japo kazi ili hata maandalizi ya harusi na nini isiwe tabu kunisumbua Mimi kugharamia shughuli zote, Basi kwangu nikaona ni bonge la wazo na kwa sababu ya connection mjini Kama mnavyojua Tena ni kitendo Cha kuagiza tu huyu kesho aje kazini na kupata kazi fasta tu week mtu huyo job.

Kufika job week mbili baadae simu hazipokelewi Mara visingizio vingi sana,kosa kubwa hakujua kuwa kwenye hiyo ofsi hiyo manager ni rafiki yangu tumekulia wote pori tumechunga sana na kuogelea kwenye maji machafu, nikampigia mshikaji simu kwani Kuna Nini huko akaniambia usijali nimpe kazi ya kufuatilia ilichukua siku tatu akanasa kila kitu Hadi kutumiwa video yupo bar anakunywa aisee nusu nizimie yaani, nikapanda Gari Hadi huko nikafika hotelini nikamwita kaja nikamhoji akagoma Tena na kilio na kusema anasingiziwa tu daah nikamwonyesha kila kitu kabaki mdomo wazi ni vilio Tena kuomba msamaha.

Itaendeleaa.....
Daahh endelea Mkuu nimesoma mwanzo mwisho aiseee huu n muujiza mkuu na nimejifunza vtu vingi sana kwanza uvumilivu, Heshima kumuheshimu kila mtuu na kikubwa zaid n kumtanguliza M/Mungu kwa kila kitu unachokifanya endelea mkuuu tafazal
Ahsante mkuu naendelea
 
Inaendelea......

Baada kujitetea sana kiukweli nilitulia sana Kama Lisaa hivi nikatafakari , Kama alinambia hanywi na Leo kanywa na Kama alinambia ananipenda Leo yupo bar anakunywa je huyu ni mtu sahihi wa kuambatana nae kweli? .

Ukweli ulinishinda nikamwambia dear naomba tu kwa ustarabu nakuachia kila kitu nilichokupa Hadi vyombo nilivyokununulia kuja kuanzia maisha Ila kazi kwanzia Sasa huna akaniambia utanifukuza wewe Kama na Nani nikamwambia Basi usijali mie Sina lolote humu Ila nimeshasema kazi huna.

Tukaachana hapo mie nikatulia bhana kiburi chote Cha kunijibu unanifukuza wewe kama Nani kumbe mtawala mkubwa kwenye taasisi hiyo ndio anatoka nae, so nilipojaribu kutikisa kibiriti kikaitikia kuwa njiti zimo na zipo tayari kuwa looh hapo nikafurahi sana nikarudi kazini kwangu nikamwambia Mungu ikiwa unajua ni wapi uliponitoa kwa Nini uache niumizwe kiasai hichi.

Baada Kama miezi kadhaa hivi kipindi Cha jiwe kuingia madarakani akapita na wote, jamaa mpka now yupo Katavi analima bi mdada ana watoto wawili baba tofauti kazi Hana anajiuzia bar tu, maisha yakasonga baada ya mda Tena nikakuta na mdada Safi yupo Tanroad mkoa x mdada mzuri tukapendana kweli mikakati ikaanza niende kujitambulisha kwao theni kwetu.

Siku nimepanga nikampitie nikaona nifanye kushtukiza alafu nilikuwa na zawadi nzuri sana kwake nikafika huko mkoani nikachukua room hotelini Safi mida kama ya saa mbili nikaibuka na boda Hadi hapo anapikaa lengo nikampe zawadi tupige story nirudi kulala Basi bhana kwa mbwembwe zote na mazaga kibao nikagonga mlango akaitikia mwanaume wewe Nani nikamwambia njoo fungua mlango jamaa akaja kufungua amejifunga taulo only daah nikamwambia Fulani yupo kasema ndio kwani we Nani nikamwambia mie Kaka yake, jamaa akaguna akamwita nae kaja kwa mbwembwe yupo kwenye kanga kufika tu kaishiwa pozi yaani nilifanya kurudi nyuma nikamwambia ahsante sana love mie Mungu ananipenda sana so kwa heri huyo hakunitafuta Hadi leo.

Itaendeleaa........
 
Inaendelea......

Basi siku hiyo ndio ikaisha hivyo nami nipo kimya tu sikutaka kumshirikisha mtu yeyote hata rafiki yangu ninaelala nae geto moja pia sikumwambia, Basi baada Kama week moja hivi yule mzee alikuja na Gari akashuka hapo alikuwa kavaa miwani nyeusi fulani akaniita njoo kijana wangu nikaenda akaniambia vipi Kuna mtu unamdai nikamjibu hapana, je Kuna mtu anakudai nikasema ndio maana hela ya kazi siku mbili sijakabidhi na ninazo zote Basi akaniambia utamkabidhi Nani Sasa nikamwambia Kuna mtu hapa naweza mkabidhi atampa ni mwaminifu tu.

Baada ya kumjibu maswali hayo nikamuuliza kwani mie naenda wapi kwa mda huu baba angu akaniambia unaenda Tabora shuleni, ukweli hapa sikuamini ninachokisikia masikioni mwangu ghafla machozi yananitoka nikamuuliza ni kweli inawezekana ? Je jina langu bado lipo kweli huko akaniambia wewe nenda shuleni Kama bado unapenda kusoma nikamwambia napenda sana kusoma.

Baada ya hapo nimekabidhi hela nikaandika kibarua kidogo kumwaga rafiki yangu tulikuwa wote getoni maana hakuwa na simu na kipindi hicho wenye simu ni wa kuhesabu maana hata huyo mzee sijui Kama alikuwa nayo maana sikumuona akiwa nayo hata kidogo,
tulianza safari Hadi karume pale nikaambiwa chagua viatu pair 4 hivi nikachagua akalipa mzee tukaondoka Hadi kwenye mashuka akanunua nakuweka kwenye bag tukaanza safari Hadi ubungo nikakatiwa ticket tukaondoka tukaenda nikapelekwa kwa Dada mmoja hivi nikatambulishwa nikaambiwa huyu dada atakupeleka stand asubuhi, mzee akaniuliza wewe una sh ngapi hapo mfukoni nikamwambia Nina laki na nusu akaniambia hiyo inakutosha kabisaa njiani mahitaji mengine utayapata shuleni.

Basi kesho yake safari ikaanza Kama siku tatu hivi ndio nikaingia Tabora kumbuka kipindi hicho kwanzia dodoma ni vumbi mwanzo mwisho, nilifika stand pale Tabora maana nilikuwa nimeambiwa ukishuka chukua daladala ya baiskeli mpka hapo shuleni utapokelewa Basi nami niliuliza watu hapo Tabora boys ni wapi nikachukuliwa na daladala Hadi hapo shuleni nikapelekwa ofsi ya mkuu wa shule nikapokelewa na second master akaniuliza wewe ndio Fulani nikasema ndio, basi akaniambia wewe umekuja kusoma au umekuja kuiona shule tu alafu urudi nikamwambia nimekuja kusoma.

Hapo nakumbuka ilikuwa umebaki week moja tu mitahani ya mwezi wa sita ianze Basi nikapelekwa kwa mkuu wa shule nikaambiwa utakaa hapa mpaka shule ikija kufunguliwa ndio utaenda bwenini nikaona hapa sawa na kwenye Chumba tulikuwa wawili na jamaa mmoja alikuwa form six basi tukawa tunapiga story ananitia moyo sana nikaanza kukopy notes na kusoma karibia usiku kucha week likakata , mkuu wa shule aliporudi alinikuta kidogo nimechangamka akaniambia vipi unaweza kufanya mitihani na wenzio nikasema ndio naweza kujaribu akasema sawa Basi jiandae jumatatu mitahani unaanza.

Nami bila kinyongo nilipiga msuli haswa wa kusoma huku yule jamaa wa form six akinitia moyo na kunifundisha sana tena kwa bidii kweli jtatu ikafika nami huyo kwenye Chumba Cha paper nikazama hapo ndipo nilianza rasmi kumwogopa Mungu kwani kila siku nilikuwa naingia kwenye Chumba Cha mtihani nimefunga na haya ndio matokeo yangu ya mtihani wa mwezi wa sita form one nikiwa nimefika shuleni week mbili kabla ya mitahani kuanza,

MATHEMATICS: A 100
PHYSICS. A 95
CHEMISTRY A 98
BIOLOGY. A 100
GEOGRAPHY A 100
HISTORY. A 100
CIVICS. A 98
ENGLISH F 15
KISWAHILI A 100

Baada ya matokeo hayo mkuu wa shule alinambia unastahili kutunzwa kwa gharama yeyote nikasema sawa akaninunulia saa Kama zawadi na maisha yakasonga mbele miaka iliyofuata ikawa napita kwenye kipindi kigumu sana hasa kwenye likizo mda mwingi nilikuwa naweza shinda bila kula na mda mwingine tukifunga shule nami naenda kutafuta vibarua kwa mfano niliendaga huko wilaya ya Uyui kata ya Loya kuvua samaki na mwaka mwingine pia nikaenda huko kuvuna mpunga sikurudi nyumbani maana nilikuwa naogopa kurudi home likizo najua nikirudi naweza nusirudi shuleni tena.



Itaendeleaa.....
Mungu ni mkubwa!
 
Inaendelea......

Mda ukapita Sasa awamu hii nikasema wacha nitulie Sasa niangalie nikamwona kamdada kamoja, nikamchora Kama miezi kadhaa bila kuonyesha dalili zote kuwa nampenda na namtaka, baadae nikatupia ndoano ikanasa binti mrembo kweli anafanya kazi kwenye shirika kubwa la kimataifa hapa nchini tukaongea akanielewa yule uzuri sehemu alipokuwa anafanyia kazi hapo Kuna watoto wa nzi kibao tu bila yeye kuwajua nikawambia jamani kazi kwenu shemeji yenu huyo nipeni sifa.

Jamaa yangu kasema unataka ushahidi kwa video au sauti au wa kuambiwa nikamwambia nipe ushahidi wa kumtia mtu hatiani,Basi nikatulia Kama week moja tu nikashushiwa uchafu wote nikasema isiwe tabu labda huenda alikuwa nao zamani coz anaweza badilika akiwa nami nikamtumia japo kidogo nikamwambia usirudie Tena nakupenda sana akalia mno akasema amekoma hatarudia Tena ilikuwa bahati mbaya tu, nikamwambia sawa tubu Sasa kwa Mungu Hadi tukamshirikisha mzee mmoja wa kanisa kwa Siri kubwa na maisha yakaendelea Kama miezi 6 mingine nikamwambia vipi uko tayari kwenda kunitambulisha kwenu akasema hapana bado anajipanga vizuri looh nikamwambia unajipanga Nini muoaji ni Mimi mie nimejiandaa kila kitu hata leo hii jeuri ya sherehe ninayo akagoma.

Nikamwambia kwa nini lakini akasema bado kidogo,nikaona isiwe tabu nikamcheki mshikaji wangu yupo kwa Sirro nikamwambia utanisadiaje akasema usijali akaandaa kibali kakipeleka kwenye mtandao Fulani akaomba print ...... Ngoma ikajibu mazaga Kama yote hapo alipo ana mimba ya miezi mitano na anapanga kuichomoa Ila jamaa mwenye nao akagoma duuu😳😳😳😳 hapa nikampigia simu nikamwambia ahsante na ushahidi huo hapo nikatulia na maisha.


Sasa ndugu zangu wanajf wapi nakosea Mimi kwenye mahusiano au Nini huwa sifanyi wapendwa maana nashindwa kuelewa kabisa wakuu now nimekuwa na umri unaenda natamani kuwa na ndoa Sasa maana Sina kipingamizi tena.

Karibuni kwa ushauri watu wenye mawazo chanya Ila nikuombe wewe mwenye akili ndogo kama hutakuwa na la maana soma alafu pita hivi.

konda msafi Mshana Jr Bujibuji Wangari Maathai
 
Inaendelea......

Mda ukapita Sasa awamu hii nikasema wacha nitulie Sasa niangalie nikamwona kamdada kamoja, nikamchora Kama miezi kadhaa bila kuonyesha dalili zote kuwa nampenda na namtaka, baadae nikatupia ndoano ikanasa binti mrembo kweli anafanya kazi kwenye shirika kubwa la kimataifa hapa nchini tukaongea akanielewa yule uzuri sehemu alipokuwa anafanyia kazi hapo Kuna watoto wa nzi kibao tu bila yeye kuwajua nikawambia jamani kazi kwenu shemeji yenu huyo nipeni sifa.

Jamaa yangu kasema unataka ushahidi kwa video au sauti au wa kuambiwa nikamwambia nipe ushahidi wa kumtia mtu hatiani,Basi nikatulia Kama week moja tu nikashushiwa uchafu wote nikasema isiwe tabu labda huenda alikuwa nao zamani coz anaweza badilika akiwa nami nikamtumia japo kidogo nikamwambia usirudie Tena nakupenda sana akalia mno akasema amekoma hatarudia Tena ilikuwa bahati mbaya tu, nikamwambia sawa tubu Sasa kwa Mungu Hadi tukamshirikisha mzee mmoja wa kanisa kwa Siri kubwa na maisha yakaendelea Kama miezi 6 mingine nikamwambia vipi uko tayari kwenda kunitambulisha kwenu akasema hapana bado anajipanga vizuri looh nikamwambia unajipanga Nini muoaji ni Mimi mie nimejiandaa kila kitu hata leo hii jeuri ya sherehe ninayo akagoma.

Nikamwambia kwa nini lakini akasema bado kidogo,nikaona isiwe tabu nikamcheki mshikaji wangu yupo kwa Sirro nikamwambia utanisadiaje akasema usijali akaandaa kibali kakipeleka kwenye mtandao Fulani akaomba print ...... Ngoma ikajibu mazaga Kama yote hapo alipo ana mimba ya miezi mitano na anapanga kuichomoa Ila jamaa mwenye nao akagoma duuu😳😳😳😳 hapa nikampigia simu nikamwambia ahsante na ushahidi huo hapo nikatulia na maisha.


Sasa ndugu zangu wanajf wapi nakosea Mimi kwenye mahusiano au Nini huwa sifanyi wapendwa maana nashindwa kuelewa kabisa wakuu now nimekuwa na umri unaenda natamani kuwa na ndoa Sasa maana Sina kipingamizi tena.

Karibuni kwa ushauri watu wenye mawazo chanya Ila nikuombe wewe mwenye akili ndogo kama hutakuwa na la maana soma alafu pita hivi.

konda msafi Mshana Jr Bujibuji Wangari Maathai
Dah! Mkuu pole sana, hii dunia haina usawa kabisa. Mafanikio ya kiuchumi unayo ila mafanikio ya kimahusiano yanakusumbua. Unajua nini mkuu, hawa wanawake "warembo" wa mjini wana shida kubwa sana kwenye ubongo wao, kwanza hawana hofu ya Mungu, pili ni waigizaji wazuri sana yaani ni waongo na hawana mshipa wa aibu.
Kama upo 35 and below bado hujachelewa kupata mwanamke mrembo na atakayekupenda na kukuheshimu. Tafuta msichana aliyemaliza form four au aliye high school. Wasichana waliopo level hiyo bado hawajui mambo mengi ya kikahaba ya mjini. Ukimpata wa hivyo wewe ndio utamfundisha maisha. Ukimpata piga mimba kwanza, kama kamaliza form four then mpeleke high school shule ya kulipia baada ya kujifungua. Watoto wa high school na waliomaliza form four wengi wao bado wako innocent na utam-shape unavyopenda mwenyewe.

Kama una approach 40 tafuta msichana wa chuo wale wa mwaka wa kwanza au wa pili. Pia chuoni bado wapo wasichana wasiojua mambo mengi.

Njia nyingine nenda kaishi uswahilini. Jichanganye uswahilini, kuna wasichana wanaochipukia ambao bado hawajawa corrupted na mambo ya mjini, vitoto vilivyotulia vipo vingi tu Uswazi kuna mabinti warembo sana wenye umri kati ya 18 hadi 23.

Ushauri wangu wa kumalizia, "achana na hawa warembo unaokutana nao barabarani na mjini tayari wamependeza, hawa hawajui kupenda, ni mabingwa wa ku-fake mapenzi". Kuna watoto wazuri sana mtaani na bado hawajajua mambo mengi. Usipoteze muda wako kuhangaika na hawa ambao tayari walishajiremba na kurembeka. Tafuta yule ambaye bado hajajua kujiremba aanze kujiremba akiwa na wewe. Watoto waliomaliza secondary na waliopo high school wanafaa zaidi, pia wa chuoni wa mwaka wa kwanza na wa pili nao wanafaa.
 
Mabinti wa siku hizi kama walivyo wanaume wengi wanapenda zaidi kutest mitambo kabla ya ndoa.
Sasa wewe utaratibu wako wa kukaa na mdada mapenzini bila kufanya lile tendo nadhani ndilo linawaweka kwenye lmtihani na kuamua kujippozea kwingine huku wakisubiri ahadi yako itimie.

Cha kufanya ni kutafuta mwanamke bikra baaas. Utamjuaje? Hapo ni muhimu kujuana na wazee kadhaa maana ni ngumu kwa kweli. Kama ni mtu wa maombi pia MUNGU aweza kukusaidia.

Inawezekana unategemea sana ujuzi wako wa kazi uliyonayo kutafuta mke(hii mara nyingi huwa haisaidii).

Halafu nikuulize ndugu, ina maana mpaka leo hujawahi gusa utupu wa mwanamke kimapenzi?
 
Dah! Mkuu pole sana, hii dunia haina usawa kabisa. Mafanikio ya kiuchumi unayo ila mafanikio ya kimahusiano yanakusumbua. Unajua nini mkuu, hawa wanawake "warembo" wa mjini wana shida kubwa sana kwenye ubongo wao, kwanza hawana hofu ya Mungu, pili ni waigizaji wazuri sana yaani ni waongo na hawana mshipa wa aibu.
Kama upo 35 and below bado hujachelewa kupata mwanamke mrembo na atakayekupenda na kukuheshimu. Tafuta msichana aliyemaliza form four au aliye high school. Wasichana waliopo level hiyo bado hawajui mambo mengi ya kikahaba ya mjini. Ukimpata wa hivyo wewe ndio utamfundisha maisha. Ukimpata piga mimba kwanza, kama kamaliza form four then mpeleke high school shule ya kulipia baada ya kujifungua. Watoto wa high school na waliomaliza form four wengi wao bado wako innocent na utam-shape unavyopenda mwenyewe.

Kama una approach 40 tafuta msichana wa chuo wale wa mwaka wa kwanza au wa pili. Pia chuoni bado wapo wasichana wasiojua mambo mengi.

Njia nyingine nenda kaishi uswahilini. Jichanganye uswahilini, kuna wasichana wanaochipukia ambao bado hawajawa corrupted na mambo ya mjini, vitoto vilivyotulia vipo vingi tu Uswazi kuna mabinti warembo sana wenye umri kati ya 18 hadi 23.

Ushauri wangu wa kumalizia, "achana na hawa warembo unaokutana nao barabarani na mjini tayari wamependeza, hawa hawajui kupenda, ni mabingwa wa ku-fake mapenzi". Kuna watoto wazuri sana mtaani na bado hawajajua mambo mengi. Usipoteze muda wako kuhangaika na hawa ambao tayari walishajiremba na kurembeka. Tafuta yule ambaye bado hajajua kujiremba aanze kujiremba akiwa na wewe. Watoto waliomaliza secondary na waliopo high school wanafaa zaidi, pia wa chuoni wa mwaka wa kwanza na wa pili nao wanafaa.
Ahsante mkuu kwa ushauri huu mzuri ngoja nimshirikishe Mungu pia nione Nini kusudi lake haswa kwangu na anataka Nini juu yangu

Mungu mwaminifu huu ushauri imekuwa mtu wa pili Sasa wacha niweke record vizuri.

Ahsante na nimeshapoa kabisa japo nimependa milima na mabonde
🙌🙌🙌🙌🙌
 
Mabinti wa siku hizi kama walivyo wanaume wengi wanapenda zaidi kutest mitambo kabla ya ndoa.
Sasa wewe utaratibu wako wa kukaa na mdada mapenzini bila kufanya lile tendo nadhani ndilo linawaweka kwenye lmtihani na kuamua kujippozea kwingine huku wakisubiri ahadi yako itimie.

Cha kufanya ni kutafuta mwanamke bikra baaas. Utamjuaje? Hapo ni muhimu kujuana na wazee kadhaa maana ni ngumu kwa kweli. Kama ni mtu wa maombi pia MUNGU aweza kukusaidia.

Inawezekana unategemea sana ujuzi wako wa kazi uliyonayo kutafuta mke(hii mara nyingi huwa haisaidii).

Halafu nikuulize ndugu, ina maana mpaka leo hujawahi gusa utupu wa mwanamke kimapenzi?
Nisiwe Muongo nishawahi mkuu ibilisi alipita na mie speed 100 na kidogo si unajua Mambo ya njoo nirekebishie Computer yangu alafu chuo na zile hostel za mkoloni 😂😂😂😂😂
 
Nisiwe Muongo nishawahi mkuu ibilisi alipita na mie speed 100 na kidogo si unajua Mambo ya njoo nirekebishie Computer yangu alafu chuo na zile hostel za mkoloni 😂😂😂😂😂
Hahaahahaa.....

Basi kwa namna hiyohiyo uliyopiga kimasikhara huyo binti ndivyo na mabinti wengine (baadhi) hupigwa pia na wao ukute wana wachumba zao huko wakisubiri ndoa.

Mimi nadhani utafute binti mdogo 21-25 ambaye hajakegeuka sana au hajaguswa. Na usimcheleweshe umuweke ndani.
 
Hahaahahaa.....

Basi kwa namna hiyohiyo uliyopiga kimasikhara huyo binti ndivyo na mabinti wengine (baadhi) hupigwa pia na wao ukute wana wachumba zao huko wakisubiri ndoa.

Mimi nadhani utafute binti mdogo 21-25 ambaye hajakegeuka sana au hajaguswa. Na usimcheleweshe umuweke ndani.
Ahsante sana mkuu nauchukua huu 👏👏👏👏 Mungu akubariki
 
Pole,
Mimi Kwa mawazo yangu, nimeona kwa kweli una kiu ya upendo wa dhati.
Ukiangalia trend from parents to majanga unayokutana nayo inaonyesha unahitaji faraja na Ile ukaribu from Babe.

Mimi Kwa upande wangu, naomba tu muachie Mungu atakutengenezea Hili akitaka, Kama ilivyokua mwanzo ulilia Mungu asikie maombi Rudi tena KWA Mungu uhojiane nae kuhusu hilo.
Inawezekana wewe Bado hujawa tayar kuwa mume hivyo bado hujapata ubavu wako.

Wadada wazuri kitabia wapo ingawa ni ngumu kuwatambua.
Don't rush jipe muda like two years Mungu ataleta tu ubavu wako.

Usionyeshe too much pesa maana wengi wanachanganyikiwa nazo.
Maombi yangu upate a wife who is a team player maana una maono makubwa so you need a smart woman to push towards what you wish to do to this world.
 
Pia napishana na mdau aliyesema utafute binti from chuo or underage.
My dear hao nao wanaweza kukupa headache
Refer wimbo wa Lissa.
 
Mkuu tafuta mwanamke wa kawaida tu usipagawe na umbo au rangi. ww angalia akili yake tu kichwani yukoje na anawaza nn bhac km mawazo yake na yako yanaendana huyo weka ndani maumbo na sura Ni vitu vitakuvutia kwa kipindi kifupi Sana na furaha yake huwa haidumu coz kila kitu kinabadilika. Usipagawe na pisi kali nyingi huwa zina akili mgando.

Tafuta mwanamke wa kawaida tu ambae mtasikilizana. mkuu umepitia shida nyingi Sana hakuna haja ya kuendelea kuteseka na mapenzi.

Na endelea kumuomba mungu huenda kuna mtu kakuandalia ambae utatengenza nae maisha
 
Inaendelea baada ya mda sana nikawa na kazi yangu mpya nikamshukuru Mungu na maisha yanaendelea na kuzurura mikoa na wilaya mbalimbali nchini baadae nikapata nafasi ya kwenda kusoma nje masters na kurudi kuendelea kutumikia nchi yangu hata Sasa naendelea.

Changamoto:

Ndugu zangu katika maisha Kuna Mambo mengi sana Kuna changamoto nyingi sana nakumbana nazo kwenye maisha hasa zingine zinatokea kwa watu ambao usingeweza kufikiria ama kuwaza kuwa huyu niliemsaidia hiki au kile anaweza kunipitisha au kunisema kwa ubaya kiasi hiki! Ila yote kwa yote huwa namuachia Mungu na kuendelea kujifunza zaidi,
Kuna mahazi nahangaika kumpa mtu ufadhili wa masomo lakini natumia mda wangu na hela zangu kusema kuwa nirudishe fadhila zangu kwa Mungu lakini mtu anaenda kuishia kula Bata tu chuoni kusoma hasomi anatoka na matokeo ovyo na wengine kufel kabisa.

Nimesadia mabinti watano Kati ya hao wawili walipigwa mimba wakaacha shule mmoja yeye aliamua kunisikiliza yeye nimemtafutia na scholarship nje ya nchi yeye ananitia moyo kila hatua wengine wawili wapo nchini nao kidogo wanapambana.

Cha ajabu Sasa watoto wa ndugu zangu ambao nilisema nitamweleza nguvu kubwa kwao wao hata shule ya msingi hawamalizi Sasa najikuta namlilia Mungu afanye Jambo kwao Ila imekuwa ngumu sana.

Itaendeleaa.....
Mkuu umenipa hamasa ya kukufahamu in personal ila tuishie hapo tu
 
Chief , mie kwa mawazo yangu , ni nahisi njia unazotumia kutafuta mke hazipo sahihi.
Lakini Pia ,badala ya kumuachia MUNGU akuchagulie Mke huyo. Wewe unaenenda kwa akili za Kibinadamu.
 
Back
Top Bottom