Kutoka nje bila kufuli ni kuzidiwa au ni kunogewa na utamu?

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,397
40,289
Miaka iliyopita nilikuwa muhuni sana, kuna mrembo mmoja hivi alikuwa mwanachuo nikatokea kuvutiwa naye, nikaanzisha naye mahusiano huku nikimpiga jeki mahitaji yake madogo madogo. Mbaya zaidi, nilipokwa nikimuomba gemu alikuwa ananizungusha huku akinifariji ipo siku utafurahi. Ikabidi niwe mpole tu.

Ikabidi nijiongeze, nikamtafutia safari nje ya mkoa kwenda kushangaa shangaa mji. Lengo langu tuende ugenini ili tulale huko huko. Kwa bahati nzuri alikubali ile safari basi mimi nikawa najiandaa kwenye mazoezi na lishe ili tukifika huko nifanye shoo ya kibabe. Siku ilipofika tulianza safari huku tukishangaa mazingira ya hapa na pale.

Ilipofika jioni ikabidi tutafute sehemu ya kupumzika, nikalipia tukaingia ndani. Nilipokuwa ndani sikuonyesha papara yoyote, tukaagiza vinywaji huku tukipeana maneno matamu matamu; baada ya muda shoo ikaanza, ilipigwa shoo hakuna kupumzika huku nikilipizia zile ahadi hewa za mwanzoni.

Akawa anapiga kelele kwa kuzidiwa, nami nikawa nachochea tu, katika kuvutana vutana akacholopoka akatoka nje bila kufuli. Ikabidi nami nitoke nje niende kumbembeleza ili aweze kurudi. Nikawa namuuliza, kwa nini umetoka nje; ulizidiwa au ulinogewa na utamu? Hakunipa jibu zaidi ya kunizaba kibao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom