Kutoka Mbeya ::: Niliyoyaona:::

Baba_Enock

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
7,076
2,443
Well:

Baada ya uchaguzi Baba_Enock ameamua kuja kwenye jiji la MBEYA kupumzika japo kidogo kabla hajaenda "Likizo ya mwisho wa Mwaka" kijijini kwao

Katika pitapita ameona mambo mengi yanachangamsha ubongo: Nitaandika baadh hapa:-

- Kuna ongezeko kubwa sana la Mahoteli na Night Clubs na Pubs! Enzi za Mbeya Peak and Mount Livingstone zimepita

- Soko la jipya la Mwanjelwa linajengwa kitaalamu sana though "pole pole"

- Pale Kabwe kuna jengo kubwa limejengwa na kwenye "lango kuu" kuna kibao kimetundikwa na kuandikwa "Payment Toilet"

- Kituo cha daladala Kadege ni cha daladala zinazokwenda "either direction" Yanapandisha kuelekea Mafiati na yanayotelemka kuelekea Iyunga/Standi yanaegeshwa upande mmoja

- Kila daladala ina "dust bin", pamoja na kwamba hiyo dust bin na yenyewe n kama dust

- Mnyama aka Nguruwe wanafugwa kama Kuku: Unakutana nao mitaani wakijitafutia mlo

- Geti la kutokea Standi Kuu ni la Kamba

- Kuna joto kama Dar es Salaam au zaidi kidogo

- Wanawake wenyej wa hapa huvaa kandambili na soksi

- Kule Mbozi kwenye kimwondo unaweza kushangaa: hamna kibao knachoelekeza kilipo kimwodo (Meteolite) na ukifika kilipo ni mazingira ambayo huwezi kufurahishwa na hata yule "mlinzi" wa pale ni kama amelazimishwa na Wizara kukaa pale
 
Aksante mkuu kwa updates!
Hilo JOTO KULIKO LA DAR, limetokea wapi Mbeya?...ulijaribu kufuatilia kidogo sababu yake?
 
Baba Enock usisahau kutembea tembea na mida ya usiku kwani Mbeya usiku mambo ni tofauti sana na mchana.
Tembelea night clubs na pubs yaani huwezi amini kama ni Mbeya uliyoiona mida ya mchana.
 
Baba Enock usisahau kutembea tembea na mida ya usiku kwani Mbeya usiku mambo ni tofauti sana na mchana.
Tembelea night clubs na pubs yaani huwezi amini kama ni Mbeya uliyoiona mida ya mchana.
U mean kuna Corner Bar na Kino wa Kutosha???? na walivyojazia watoto wa mbeya Baba Enock play safe.....
 
Kweli baba enock, Mbeya ya sasa ni tofauti na mbeya ya zamani. Ulifika pale mafiati,kuna night club maarufu sana pale (jina limenitoka). vp Mammaland pale forest, uhindini kuna Pamoz (niliwahi enda once pale ukumbi si mbaya - ila panajaa watoto wa shule-wanaingia na vibegi vya kubadilisha nguo!!)! Mwanjerwa sasa pamekuwa ndy mjini haswaa!! (ila vumbi tu!). Usitamani kushuka airport masika! (nadhan ujenzi wa airport mpya utabadilisha mambo-hakuna usafiri wa ndege zaidi ya zile za kukodi!).
Ndaga fwijo\!
 
Kwa kuongezea daladala ni kituo hadi kituo hakuna msaada tutani,chumba cha guest house cha 10,000 Mbeya ,Arusha ni 20,000/=ila unyanfu umepanda bei sana ,but napenda sana kula amafufu ya kuchoma ,Mbeya Kwetu
 
Kuna hoteli nzuri sana siku hizi inaitwa BEACO njia kuu ukiwa unaelekea meta...
 
Kweli baba enock, Mbeya ya sasa ni tofauti na mbeya ya zamani. Ulifika pale mafiati,kuna night club maarufu sana pale (jina limenitoka)......

Inaitwa carnival,
Ipo baa ingine pale soko matola inaitwa "karembu", ni maarufu pia.
Karibu Baba E, walao upate Tusker baridi hapo karembu !
 
Wadau,

Nimesharudi Dar::

Nimeipenda sana Mbeya:

Kwa kuogezea,

- BEACO kwa standards ipo juu zaidi ya hotel zote jijini Mbeya, wahitaji tu kufanya "polishing" ya wahudumu kuelewa kuwa "hospitality industry" ni zaidi ya kutabasamu.

- Mbeya Paradise imegeuka kuwa ukumbi wa mikutano na kwahiyo kama unakwenda "kupumzika" ukichelewa kuamka "breakfast" unakuta wameshatoa vyombo na wanaandaa chai ya wageni wa mkutano

- Hoteli nyingine ambazo zipo "along" the road kuanzia Uyole mpaka njia panda ya stendi wanajitahidi kiasi chao

- Pamoz bado ipo, Mbeya Carnival ipo pia lakini zote mbili zimepungukiwa "creativity", kwahiyo kidogo zimekuwa kama "vijiwe fulani"

- Shaba Pub ni mpya kwenye "game", nadhani officially itafunguliwa end of november 2010, kama hawatapungukiwa na "momentum", wanaweza kuwa "talk of the town". Ipo soweto. DJs wanaonekana kuwa walevi sana na matokeo yake wanapo weka muziki, wanakuwa wanafanya "jockery" almost mpaka muziki unaisha!

- Kuna ongezeko la "dada poa" kuliko wakati mwingine wowote: sijaribu ku-offend mtu yeyote, lakini ongezeko la vyuo vikuu has got something to do with it. Vyuo vikifunguliwa hizo sehemu zote za "night clubs" zinajaa kuliko hata Corner baa - Sinza!

- Utengule Country Hotel ndiyo hotel pekee yenye "swimming pool" jijini Mbeya, kwahiyo weekend wale "upper-middle-class" unakuta "wanaogelea" na familia zao: kuna kiingilio cha buku tatu

- Kule Songwe ujenzi wa uwanja wa ndege unaendelea japo pole pole sana, nilikuwa huko miezi sita iliyopita, na this time around nimekuta zile structures bado zipo kwenye "shell": siyo mtaalamu wa Civil therefore not sure what is going on there!
 
Back
Top Bottom