Kutoka Mahakama ya Mafisadi mpaka Mahakama ya Kusamehe Mafisadi...!

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Watu wanaitazama Tanzania kwa jicho lingine. Labda huu nao ni ubunifu wa Utawala na pengine ni mafanikio miongoni mwa mafanikio.

Watawala walianza na kile kilichoitwa kutumbuwa mafisadi na kuwasekwa ndani waliotuhumiwa. Mara ikaundwa mahakama ya Mafisadi na kutangaziwa kiama mafisadi wote. Wakati huo nchi ilihanikizwa na sauti za walibambikiziwa kesi mbali mbali na hata wengine kupatwa na vihoro.

Mamia ya Watanzania wamekaa ndani na uchunguzi haufiki kikomo. Lakini la kushangaza hizo kesi za Uhujumu uchumi zilizosajiliwa mahakamani haziendani na idadi ya wingi walioko mahabusu kwa ujhujumi uchumi. Hapo ndipo wasi wasi ulipoanzia.

Sasa baada ya miaka tulitegemea Mahakama hii itumike kutenda HAKI na kuwatia hatiani wale wote walioitwa Mafisadi. Tulitarajia Nguvu ielekezwe kuthibitisha uhujumu uchumi wa hao washukiwa waliobatizwa makosa yao tayari kabla ya Mahakama kuthibitisha na hatma yake nguvu sasa inatolewa kuwataka wakiri na kuomba kuachiliwa hapa kuna nini? Huku ndio kunaitwa kukokoteza na kujiaibisha.

Bahati mbaya Tanzania ndio inaaibishwa na watawala wetu. Tukiambiwa hatufuati sheria kuna watu wanatoka povu lililopitiliza. Unamlazimisha mtu kuomba msamaha wa uhujumu uchumi na kulipa mabilioni lakini unbaacha mahakama ya mafisadfi haina kesi inayoendelea na halafu unakazania kulipwa mapesa. Hii mahakama ina kazi gani? Nani hapa anahadaiwa kwa maslahi yepi?

Ndiyo, Tanzania inaaibishwa, inaaibishwa mifumo yetu ya HAKI na Mahakama kwa kukubali utashi wa mtu kuwa ndio utashi wa Tanzania. Ya nini yote haya?

YA NINI YOTE HAYA?

Huku ni kufeli na kutapatapa. Kuna mahala tulijikwaa. Hakukuwa na ulazima wa kufanya haya tokea mwanzo ukijuwa mwisho wake ni huku. Tulishasema, chini ya utawala wa CCM huwezi kumuadabisha mtu kwa ufisadi na wewe ukawa salama. Tanzania ufisadi uko kwenye mfumo. Baada ya kuwavuruga baadhi ya watu kwa makeke ya kujitakia, leo unakaribia uchaguzi unaanza kuona aibu. Unalazimisha watu wapige goti kwenye Chama na sasa walioitwa mafisadi kwa nguvu zote kabla ya mahakama kuthibitisha wanapewa "deadline" ya kukiri makosa nje ya mahakama na kutakiwa kulipa fedha. Narudia huku ni kutapatapa na kufanya aibu kwa Taifa.


USHAURI WA BURE

Watawala wangechora mstari mwekundu na kushughulika na Katiba mpya kuweka misingi. Hiki kilichofanyika ni hadaa na kuliaibisha Taifa.

Wale wazee na vijana waliobatizwa jina la Mafisadi wasionewe bure tatizo ni mfumo. Tunacheza na maisha ya watu kwea sifa zisizomaana na tumeshindwa kutumia fursa adhimu ya madaraka kuwaandalia Watanzania tunu ya taifa ya Katiba mpya halafu tunaleta mazingaombwe.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake.

Katiba Mpya inawezekana.



Kishada
 
Watu wanaposema mambo yanayofanyika Tanzania yako Tanzania tu(Only in Tanzania) wako sahihi kwa 100%.
Habari za kwamba Rais Magufuli aliwaahidi Watanzania kuunda Mahakama ya Mafisadi ili iwashughulikie watu waliokwiba na kufuja fedha na mali ya umma sasa imedhihirika ilikuwa ni gea ya kuingilia Ikulu tu.

https://www.ippmedia.com/sw/habari/hatimaye-mahakama-ya-mafisadi-kuanza-julai

Juzi Watz na dunia yote wamebakia midomo wazi baada ya Rais huyuhuyu anayejitanabaisha kwa kupambana na RUSHWA kuwageuka Wadanganyika na kuamua KUWASAMEHE WEZI NA MAFISADI WOTE walioko Magerezani kirahisi kabisa kwa kuwaelekeza KUANDIKA BARUA ZA KUOMBA MSAMAHA NA KURUDISHA CHENJI ZA MAGUFULI.

Kila mtu anajiuliza hii kitu imekaaje? Je, iko sheria inayoruhusu Mafisadi kuomba msamaha kwa barua na kurudisha pesa? Makosa ya Ufsadi yanaangukia kwenye MAKOSA YA UHUJUMU UCHUMI na huwa hayana dhamana. Lakini leo hii Rais kaamuka tu anatangaza Mafisadi waombe msamaha na kurudisha fedha na KESI KWISHNE...!!

Je, katika UTAWALA WA SHERIA na UTAWALA BORA hii inakubalika? Je, Rais Magufuli haoni kwamba kitendo hiki ni kuchochea WIZI WA KIFISADI na UHUJUMU UCHUMI? Watu wakishajua na kuamini kwamba UKIIBA MALI YA UMMA KINACHOTAKIWA NI KUOMBA MSAMAHA NA KURUDISHA PESA na hakuna adhabu ya Kifungo,faini au vyote viwili hali itakuwa mbaya sana huko mbele ya safari..!!.Tunataka Jaji Mkuu, DCI na Wanasheria wetu Tanzania wajitokeze hadaharani na wawaambie Watz na dunia nzima kama alichofanya Rais ni sahihi...!!

Kwa sasa dunia inasikilizia hekaheka za Wamerekani kutaka kumwondoa Rais Donald Trump madarakani kwa kutumia mfumo wa IMPEACHMENT BAADA YA KUKIUKA KATIBA YA WAMEREKANI. Lakini kwa Watz wanao ona Rais wao anakanyaga Katiba aliyoapa KUILINDA na KUITETEA wametulia tuli as if nothing is happening..!!!!. Hii ni aibu kubwa sana kwa Tanzania. Rais aliyechaguliwa na Wananchi kujiona yuko juu ya Sheria na Katiba na kujifanyia mambo yake anavyojisikia kana kwamba ni mungu mdogo wa Tanzania halafu hakuna anayehiji wala kudadishi. Nani aliyewaroga Wadanganyika?

Poleni sana Wadanganyika. There is a very very long walk to Uhuru.
 
Tutakupa kesi ya kuhujumu uchumi.. umaembiwa watakao patikanana kuanzia sasa sheria ifuate mkondo wake.
 
Kila siku Jiwe anasema nchi hii tajiri sana....anajenga Flaiova,SGR na Stieglers Gorge kwa fedha ya ndani...!!
Sasa hela ya Uchaguzi inakosekanaje?
ndo kashaishiwa hivyo!
huwezi ukafanya matumizi yasiyo na mwelekeo stahili ukategemea uchumi wako utakuwa kisa una "assets"! nchi ni kweli ni tajiri sana...ila haina hela 😂
 
Wewe sio mzalendo wa nchi, mwacheni Raisi afanye kazi

Nani Mzalendo kati ya yule anaye samehe Mafisadi na aanyetaka washughulikiwe?
Unless unataka kunambia neno 'FISADI' limepoteza kabsa maana halisi kwenye awamu hii ya 5...!!!
 
Lakini unafahamu ya kwamba, kusamehe watuhumiwa WA makosa mbalimbali yakiwemo makosa ya jinai kwa watuhumiwa ambao Kesi zao zipo Mahakamani ni kuvunja Katiba ya JMT ?Unalijua suala hili lakini?
[/Q2UOTE]
Kwanza nani kampa ruhusa ya kuongolea suala lililopo mahakani? Au hii sheria iko kwenye rasimu ya katiba mpya?
 
Kama kesi za mafisada upelelezi ulishindikana basi mafisadi hao wawaachie badala ya kutengeneza migogoro ya kikatiba na kisiasa.
 
Back
Top Bottom