Kesi ya Kupinga matokeo inayomkabili Mheshimiwa Tundu Antiphas Mughwai Lissu wa Jimbo la Singida CHADEMA, asubuhi hii imeahirishwa kwa muda wa masaa mawili na nusu, ili upande wa walalamikaji ukawatafute mashahidi ambao hawajaweza kufika mahakamani kama tulivyoambiwa jana. Gari la Chama cha Mapinduzi limefika mahakamani na walalamikaji wake na kupeleka taarifa hiyo, lakini pia wameamua kuongezea kuwa wakili wao wa kujitegemea Gabriel Wasonga hajisikii vizuri, na mashahidi hawajaja bado. Tupo ndani ya Jengo la mahakama hapa na Tundu Lissu pamoja na wafuasi na wasikilizaji kuwasubiri. Jana jioni aliyepaswa kutoa ushahidi aliingia mitini hakuonekana, na mwingine wa mwisho aliyetoa ushahidi jana, aliwaumbua baada ya kuwaambia yeye anamwogopa Mungu, walimchukua yeye ni CHADEMA, wakamhonga akaseme uongo mahakamani. yeye alipofika akasimamia anachojua wakaaibika sana, walimnyima hata nauli ya kurudi Kijijini Isuna. Tutaendelea kuwaletea yanayojiri huku