Zitto atoa kauli juu ya Zuio la Gesi ya Tanzania kuingia nchini Kenya

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
608
1,540
Kenya Kuzuia Gesi ya Tanzania: Tanzania ichukue hatua dhidi ya Kenya

Wizara ya Nishati ya Kenya imepiga marufuku gesi ya kupikia kutoka Tanzania kuingia nchini humo. Tamko la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Kenya linasema ' ndani ya siku 7 kuanzia juzi tarehe 24 Aprili 2017, itakuwa ni marufuku Kwa Kenya kuagiza Gesi ya kupikia kutoka Tanzania '. Uamuzi huu wa Kenya ni kinyume na misingi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania na Kenya ni wanachama. Kwa mujibu wa Itifaki ya Soko la Pamoja, bidhaa za nchi zetu zinaruhusiwa kusambaa ndani ya jumuiya bila vikwazo.

Gesi ya kupikia kuingia Kenya hutokea Tanzania Kwa sababu Tanzania ni nchi pekee katika ukanda huu ambayo imewekeza mitambo ya kupokea Gesi na kuiweka kwenye mitungi. Bandari ya Dar Es salaam na mfumo mzuri zaidi wa kupokea gesi kuliko Bandari ya Mombasa na hivyo kuifanya gesi inayotoka Tanzania kuwa na gharama nafuu nchini Kenya kuliko gesi inayoagizwa kupitia bandari ya mombasa.

Uamuzi wa kuzuia Gesi kutoka Tanzania ni uamuzi wenye kulenga kuilinda bandari ya Mombasa Kwa kuvunja mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kwa kutaka kuifanya Tanzania iendelee kuwa muuzaji wa malighafi kwenda Kenya badala ya bidhaa zilizokamili Kama gesi ya kupikia.

Uamuzi huu wa Serikali ya Kenya una lengo la kuathiri urari wa biashara kati ya Tanzania na Kenya ambapo Kwa miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa nyingi zaidi huko Kenya kuliko inazoagiza kutoka nchi hiyo.

Ninamsihi Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania afuatilie suala hili na kuzungumza na mwenzake wa Kenya ili waondoe vikwazo Hivi vya biashara ambavyo havina maana yeyote na vinazuia raia wa kenya kupata bidhaa nafuu kutoka Tanzania. Viwanda vingi vya Kenya hutegemea malighafi kutoka Tanzania, kuzuia gesi ya kupikia na kuendelea kuagiza malighafi za kuendesha viwanda vyao ni sera ya Kenya kuifanya Tanzania kuwa chanzo cha malighafi tu na sio chanzo cha bidhaa zilizoongezwa thamani.

Serikali ya Tanzania isikubali hili na ianze mazungumzo mara moja na Serikali ya Kenya ili Watanzania wanaouza gesi ya kupikia huko Kenya waendelee kuuza na kutumia Bandari ya Dar Es Salaam. Kama Serikali ya Kenya ikiendelea na msimamo wake basi Tanzania ichukue msimamo kama huo Kwa bidhaa za Kenya Kama maziwa ambayo yamejaa kwenye soko letu.

Zitto Kabwe, Mb
Kigoma mjini
26/4/2017
 
Yaani unapata wapi guts za kuwazungumzia Bongo movie na filamu zao mbovu?hapa tunaongelea habari za gesi sio mapicha yasiyokuwa na vigezo
Siwaongelei bongo Movie ila ninachojaribu kusema "mtenda akitendewa huisi ameonewa"
Kiongozi mmoja amewatendea watanzania walalahoi kwa kuzuia mrija wa mkate wao Wa kila siku kwa ajili ya kulinda vya ndani lakini hakuna aliyeonyesha kujali
Sasa Kenya nao wameamua kuzuia kama alivyozuia yule basi kelele juu
 
Siwaongelei bongo Movie ila ninachojaribu kusema "mtenda akitendewa huisi ameonewa"
Kiongozi mmoja amewatendea watanzania walalahoi kwa kuzuia mrija wa mkate wao Wa kila siku kwa ajili ya kulinda vya ndani lakini hakuna aliyeonyesha kujali
Sasa Kenya nao wameamua kuzuia kama alivyozuia yule basi kelele juu
Wanachotakiwa mbongo movie mkuu ni kutengeneza filamu bora na nzuri tutanunua tu mbona enzi za marehemu industry yao ilikuwa sana tatizo lao sasa wanajifanya masuper star wakati hawafika huko na kitu kingine ni jukumu LA serikali kukaa nao ili msambazaji wa hizo movie awalipe kulingana na thamani ya kazi yao? Huwezi lazimisha watu wanunue kitu kibovu,wakenya wao wanalinda bandari yao kwenye miundombinu ya gesi na uzuri kuna utengamano wa A.mashariki kama Zitto alivyoshauri ni vyema wakae mawaziri ili watatue ilo swala
 
Tanzania na Kenya are long rivarls toka kwa kipind ile tunanyanganyana Mali za former EAC, na Kenya amekuwa sio MTU wa kuipromote region but someone who promote himself.... Taking examples na issue nyng ambazo huwa ni joint ventures au vtu ambavyo yye hamiliki na kuclaim ni vyake(refers to the might migration na Kilimanjaro mountain). Hyo inamaanisha uhusiano wa EAC umekaa kipolitical zaid na sio..economically..hamna mutual relationship kwa nchi zetu. moja inatumia advantage ya mwingne n then surpass effort ya mwngne anapojitahd kuinuka...That's to say faida katka ushirikiano wa EAC ni mdgo. Some countries are SEGREGATIVE by nature like KENYA....Hyo inanfanya nisiamin uwepo wa EAC na sion economic benefit yake zaid ya kubase zaid kwenye political issues
 
Kiukweli hili sio suala la kupuuzia hata kidogo ,inakuwa haina maana ya kuwa na jumuiya ya afrika amashariki kama wenzetu wana maamuzi hayo lengo la jumuiya ni kuondoa vikwazo kwa nchi wanachama vya kibiashara,usalama,technology kwa maana hiyo waziri wa nishati tz Fanya mazungumzo na hawa jamaa zetu wa Kenya kumaliza hili jambo kama watakata hatua stahiki zichukuliwe
 
Zitto Zuberi Kabwe, umeandika vema lakini akili ya mkenya huijui, hawako normal as normal as think, Waziri wa Kenya alipopiga marufuku ashajua Tz tutalalamika, vikao vitakaa, itaruhusiwa, LAKNI KWAKE UJUMBE UTAKUWA UMEFIKA, NA WAPAKIA GESI MITUNGINI WATAHAMIA MOMBASA, NA WAKENYA WAKIENDA DUKA LA GESI HAWATANUNUA ZA TZ, HIVYO NDIO AKILI ILIVYO, TULIONA MAZIWA YA MUSOMA, TULIONA TANBOND, TULIONA MAJI YA KUNYWA. tuachane na tabia hizi za kufanywa mbele na nyuma kote halali yao, akili ya mkenya inataka jino kwa jino, Jino kwa jino ndio normality ya Kenyan brain
Kenya Kuzuia Gesi ya Tanzania: Tanzania ichukue hatua dhidi ya Kenya

Wizara ya Nishati ya Kenya imepiga marufuku gesi ya kupikia kutoka Tanzania kuingia nchini humo. Tamko la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Kenya linasema ' ndani ya siku 7 kuanzia juzi tarehe 24 Aprili 2017, itakuwa ni marufuku Kwa Kenya kuagiza Gesi ya kupikia kutoka Tanzania '. Uamuzi huu wa Kenya ni kinyume na misingi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania na Kenya ni wanachama. Kwa mujibu wa Itifaki ya Soko la Pamoja, bidhaa za nchi zetu zinaruhusiwa kusambaa ndani ya jumuiya bila vikwazo.

Gesi ya kupikia kuingia Kenya hutokea Tanzania Kwa sababu Tanzania ni nchi pekee katika ukanda huu ambayo imewekeza mitambo ya kupokea Gesi na kuiweka kwenye mitungi. Bandari ya Dar Es salaam na mfumo mzuri zaidi wa kupokea gesi kuliko Bandari ya Mombasa na hivyo kuifanya gesi inayotoka Tanzania kuwa na gharama nafuu nchini Kenya kuliko gesi inayoagizwa kupitia bandari ya mombasa.

Uamuzi wa kuzuia Gesi kutoka Tanzania ni uamuzi wenye kulenga kuilinda bandari ya Mombasa Kwa kuvunja mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kwa kutaka kuifanya Tanzania iendelee kuwa muuzaji wa malighafi kwenda Kenya badala ya bidhaa zilizokamili Kama gesi ya kupikia.

Uamuzi huu wa Serikali ya Kenya una lengo la kuathiri urari wa biashara kati ya Tanzania na Kenya ambapo Kwa miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa nyingi zaidi huko Kenya kuliko inazoagiza kutoka nchi hiyo.

Ninamsihi Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania afuatilie suala hili na kuzungumza na mwenzake wa Kenya ili waondoe vikwazo Hivi vya biashara ambavyo havina maana yeyote na vinazuia raia wa kenya kupata bidhaa nafuu kutoka Tanzania. Viwanda vingi vya Kenya hutegemea malighafi kutoka Tanzania, kuzuia gesi ya kupikia na kuendelea kuagiza malighafi za kuendesha viwanda vyao ni sera ya Kenya kuifanya Tanzania kuwa chanzo cha malighafi tu na sio chanzo cha bidhaa zilizoongezwa thamani.

Serikali ya Tanzania isikubali hili na ianze mazungumzo mara moja na Serikali ya Kenya ili Watanzania wanaouza gesi ya kupikia huko Kenya waendelee kuuza na kutumia Bandari ya Dar Es Salaam. Kama Serikali ya Kenya ikiendelea na msimamo wake basi Tanzania ichukue msimamo kama huo Kwa bidhaa za Kenya Kama maziwa ambayo yamejaa kwenye soko letu.

Zitto Kabwe, Mb
Kigoma mjini
26/4/2017
 
Kenya Kuzuia Gesi ya Tanzania: Tanzania ichukue hatua dhidi ya Kenya

Wizara ya Nishati ya Kenya imepiga marufuku gesi ya kupikia kutoka Tanzania kuingia nchini humo. Tamko la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Kenya linasema ' ndani ya siku 7 kuanzia juzi tarehe 24 Aprili 2017, itakuwa ni marufuku Kwa Kenya kuagiza Gesi ya kupikia kutoka Tanzania '. Uamuzi huu wa Kenya ni kinyume na misingi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania na Kenya ni wanachama. Kwa mujibu wa Itifaki ya Soko la Pamoja, bidhaa za nchi zetu zinaruhusiwa kusambaa ndani ya jumuiya bila vikwazo.

Gesi ya kupikia kuingia Kenya hutokea Tanzania Kwa sababu Tanzania ni nchi pekee katika ukanda huu ambayo imewekeza mitambo ya kupokea Gesi na kuiweka kwenye mitungi. Bandari ya Dar Es salaam na mfumo mzuri zaidi wa kupokea gesi kuliko Bandari ya Mombasa na hivyo kuifanya gesi inayotoka Tanzania kuwa na gharama nafuu nchini Kenya kuliko gesi inayoagizwa kupitia bandari ya mombasa.

Uamuzi wa kuzuia Gesi kutoka Tanzania ni uamuzi wenye kulenga kuilinda bandari ya Mombasa Kwa kuvunja mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kwa kutaka kuifanya Tanzania iendelee kuwa muuzaji wa malighafi kwenda Kenya badala ya bidhaa zilizokamili Kama gesi ya kupikia.

Uamuzi huu wa Serikali ya Kenya una lengo la kuathiri urari wa biashara kati ya Tanzania na Kenya ambapo Kwa miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa nyingi zaidi huko Kenya kuliko inazoagiza kutoka nchi hiyo.

Ninamsihi Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania afuatilie suala hili na kuzungumza na mwenzake wa Kenya ili waondoe vikwazo Hivi vya biashara ambavyo havina maana yeyote na vinazuia raia wa kenya kupata bidhaa nafuu kutoka Tanzania. Viwanda vingi vya Kenya hutegemea malighafi kutoka Tanzania, kuzuia gesi ya kupikia na kuendelea kuagiza malighafi za kuendesha viwanda vyao ni sera ya Kenya kuifanya Tanzania kuwa chanzo cha malighafi tu na sio chanzo cha bidhaa zilizoongezwa thamani.

Serikali ya Tanzania isikubali hili na ianze mazungumzo mara moja na Serikali ya Kenya ili Watanzania wanaouza gesi ya kupikia huko Kenya waendelee kuuza na kutumia Bandari ya Dar Es Salaam. Kama Serikali ya Kenya ikiendelea na msimamo wake basi Tanzania ichukue msimamo kama huo Kwa bidhaa za Kenya Kama maziwa ambayo yamejaa kwenye soko letu.

Zitto Kabwe, Mb
Kigoma mjini
26/4/2017


MY COMMENTS:

- It is not fair, but smart. ha ha ha ha! na hii ni calculate strategy, siamini kama watasitisha kirahisi.
- Bidhaa za Kenya Tanzania ni nyingi sana, and we just enjoy, serekali wala haiangalii kwa uwiano na viwanda vyetu.
- Hii inapendeza sana sasa kama na sie wa Tanzania twaonekana ni threat kwa wakenya kwenye biashara.
- Kwa nini zito asiongelee haya bungeni kuliko kushauri tu kwa hawa jamaa zetu?
 
Kenya Kuzuia Gesi ya Tanzania: Tanzania ichukue hatua dhidi ya Kenya

Wizara ya Nishati ya Kenya imepiga marufuku gesi ya kupikia kutoka Tanzania kuingia nchini humo. Tamko la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati ya Kenya linasema ' ndani ya siku 7 kuanzia juzi tarehe 24 Aprili 2017, itakuwa ni marufuku Kwa Kenya kuagiza Gesi ya kupikia kutoka Tanzania '. Uamuzi huu wa Kenya ni kinyume na misingi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania na Kenya ni wanachama. Kwa mujibu wa Itifaki ya Soko la Pamoja, bidhaa za nchi zetu zinaruhusiwa kusambaa ndani ya jumuiya bila vikwazo.

Gesi ya kupikia kuingia Kenya hutokea Tanzania Kwa sababu Tanzania ni nchi pekee katika ukanda huu ambayo imewekeza mitambo ya kupokea Gesi na kuiweka kwenye mitungi. Bandari ya Dar Es salaam na mfumo mzuri zaidi wa kupokea gesi kuliko Bandari ya Mombasa na hivyo kuifanya gesi inayotoka Tanzania kuwa na gharama nafuu nchini Kenya kuliko gesi inayoagizwa kupitia bandari ya mombasa.

Uamuzi wa kuzuia Gesi kutoka Tanzania ni uamuzi wenye kulenga kuilinda bandari ya Mombasa Kwa kuvunja mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kwa kutaka kuifanya Tanzania iendelee kuwa muuzaji wa malighafi kwenda Kenya badala ya bidhaa zilizokamili Kama gesi ya kupikia.

Uamuzi huu wa Serikali ya Kenya una lengo la kuathiri urari wa biashara kati ya Tanzania na Kenya ambapo Kwa miaka ya hivi karibuni Tanzania imekuwa ikiuza bidhaa nyingi zaidi huko Kenya kuliko inazoagiza kutoka nchi hiyo.

Ninamsihi Waziri wa Biashara na Viwanda wa Tanzania afuatilie suala hili na kuzungumza na mwenzake wa Kenya ili waondoe vikwazo Hivi vya biashara ambavyo havina maana yeyote na vinazuia raia wa kenya kupata bidhaa nafuu kutoka Tanzania. Viwanda vingi vya Kenya hutegemea malighafi kutoka Tanzania, kuzuia gesi ya kupikia na kuendelea kuagiza malighafi za kuendesha viwanda vyao ni sera ya Kenya kuifanya Tanzania kuwa chanzo cha malighafi tu na sio chanzo cha bidhaa zilizoongezwa thamani.

Serikali ya Tanzania isikubali hili na ianze mazungumzo mara moja na Serikali ya Kenya ili Watanzania wanaouza gesi ya kupikia huko Kenya waendelee kuuza na kutumia Bandari ya Dar Es Salaam. Kama Serikali ya Kenya ikiendelea na msimamo wake basi Tanzania ichukue msimamo kama huo Kwa bidhaa za Kenya Kama maziwa ambayo yamejaa kwenye soko letu.

Zitto Kabwe, Mb
Kigoma mjini
26/4/2017
NI USHAURI MZURI SANA.
KATIKA NCHI ZA A. MASHARIKI, KENYA HAIUITAJI USHIRIKA HUU NA NI NCHI YA KWANZA ITAKAYOJITOA MAPEMA SANA.
INAONYESHA ZARAU SANA KWA MAMBO MENGI.
 
Tuimarishe soko la ndani na kutafuta masoko mengine kwenye nchi zisizo na husuda. Lakini tujue pia sababu hasa nini kinaifanya Kenya kuanza tabia hii, na kuifanyia kazi!
Nimeipenda Id yako kwanza, lakini hii ni ishara ya kwamba sera zetu Tz za kujitegemea na kuwa na taifa lenye kujitegemea lenyewe zinaanza kufanya vizuri zaidi. Unadhani kuna tatizo lililofikisha haya zaidi ya Tz kukua?

Kwa miaka mingi Kenya ililimonopoli soko la East and central Afrika, sasa tz inakuja tena kwa spidi, wanahofu, hawana lingine. Ki nafasi tu Tz iko sehemu nzuri sana. Nataraji kuyaona mengi sana mbeleni.
 
Kenya wao wanajionaga wanajua na wako vizuri kibiashara.
Hapa ni ushindani wa kibiashara tu, hakuna kuwabembeleza tujaribu kushusha bei ili tuongeze matumizi ya ndani vilevile tukuze soko la nje kwa nchi nyingine.
 
Back
Top Bottom