Le Grand Alexei
Senior Member
- Nov 9, 2011
- 116
- 83
Siku chache baada ya mkutano mkuu wa 8 wa CCM kumalizika Dodoma kimemo kinachomhusu kada machachari wa CCM aliyeongoza kura za maoni za kuwania kusimamishwa kugombea Ubunge wa jimbo la Nzega mwaka 2010 na kukatwa jina kwa utata wa Uraia wake na badala yake kuteuliwa na NEC ya CCM Dkt Hamis Kigwangala aliyekuwa ameshika nafasi ya 3 kwenye kura hizo, na ambaye inasemekana wamepatana na kada mwenzake maarufu na Mbunge wa jimbo la Nzega Dkt Hamis Kigwangala.
Kwa namna ya kuvutia vijana hawa ambao mara kwa mara wamekuwa wakishindana wakiwa pande tofauti, na ambao inasemekana wapo kambi tofauti, Bashe akiwa kwa Lowassa na Kigwangala kwa Membe, kambi ambazo zinasigana katika kuusaka Urais wa JMT mwaka 2015.
Kimemo hicho, kinaambatanishwa hapa, kinaeleza mawasiliano yaliyokuwa yakitoka kwa Membe kwenda kwa Kigwangala, yakidai kuwa hakuna 'press conference' bali Bashe ana kesi ya kujibu na hivyo atasimamishwa kizimbani siku za usoni kwa kosa la kumtukana na kumkashifu Bernard Membe aliyekuwa anagombea Ujumbe wa NEC kupitia kundi la 'kifo' kwenye mkutano mkuu ule.
Hussein Bashe alitoa maneno makali ya kashfa dhidi ya membe, akidai hafai kupewa uongozi kwa kuwa ni mnafiki, muongo n.k. Badala ya Membe kujibu kwa kutumia njia ya media naona, kwa kimemo hiki, anaamua kumburuza mahakamani Hussein Bashe.
Re, Al.
Kwa namna ya kuvutia vijana hawa ambao mara kwa mara wamekuwa wakishindana wakiwa pande tofauti, na ambao inasemekana wapo kambi tofauti, Bashe akiwa kwa Lowassa na Kigwangala kwa Membe, kambi ambazo zinasigana katika kuusaka Urais wa JMT mwaka 2015.
Kimemo hicho, kinaambatanishwa hapa, kinaeleza mawasiliano yaliyokuwa yakitoka kwa Membe kwenda kwa Kigwangala, yakidai kuwa hakuna 'press conference' bali Bashe ana kesi ya kujibu na hivyo atasimamishwa kizimbani siku za usoni kwa kosa la kumtukana na kumkashifu Bernard Membe aliyekuwa anagombea Ujumbe wa NEC kupitia kundi la 'kifo' kwenye mkutano mkuu ule.
Hussein Bashe alitoa maneno makali ya kashfa dhidi ya membe, akidai hafai kupewa uongozi kwa kuwa ni mnafiki, muongo n.k. Badala ya Membe kujibu kwa kutumia njia ya media naona, kwa kimemo hiki, anaamua kumburuza mahakamani Hussein Bashe.
Re, Al.