Kutoka Chato: Rais Magufuli amwapisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Kwanini Mbuzi, papai, fenesi na Kware wawe na Corona?

Kama korona inahusishwa/ imetokana na popo, hao wanyama anaowataja inashangaza nini kama wakikutwa nayo.
La kujiuliza anaijua korona, jinsi inavyoambukizwa nk.?

Kwa sababu korona ukutani ipo, juu ya meza na viti ipo, kwenye mabasi na vya kufunguliwa milango ipo, ndio maana inashauriwa vipulizwe madawa na kufutwa, ndio maana inashauriwa watu kunawa mikono. Ambacho haelewi ni nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inshort mzee anakataa uwepo wa Corona Tanzania. Majibu yaliotolewa before ni ya uongo. Maabara ya taifa inatumika na mabeberu. Hivyo watu wasiwe na hofu wachape kazi!

Sent From Galaxy S20 Ultra
 
MWIGULU AZIA TOSAMAGANGA NDUGU WANANUN'GUNIKA ,HAWANA IMANI KUWA NDUGU YAO KAFA KWA CONVID19....WAZEE WANATAKA KUFANYA TAMBIKO ....
MAREHEMU ALIKUWA AKIISHI PEKE YAKE ....WALIOENDA KUMCHUKUA AKAFIKA HOSPITALI AKIWA KAFARIKI USIKU HUO NI KINA NANI ????
 
Pole kaka,unataka kusema rais wetu anajua watanzania wote Ni wasomi Kama wewe hata akiongea kwa fasihi na nahau tutamuulewa tu.Kuhusu hicho ulichoekewa wewe,shida ya maabara yetu vifaa au Wataalamu? Na uchachuaji ulianza baada ya hao hao kumwambia Corona ipo nchini na tayari watu 16 wamekufa au ulianza baada ya jamaa kugoma kucopy na kupaste Mambo ya wazungu? Ni hatua gani zimechukukiwa kuhusu uchachuaji huo? Baada ya kutuambia maabara inachachua,ametoa njia nyingine inayoweza kutumiwa na watanzania kupima Kama wana corona?
Kama Leo umeona uwamuzi alio ufanya waziri wa afya utakua umeamini nilicho kwambia kwa kauli ya raisi kuwa Hadi papai kukutwa na virusi vya corona

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
View attachment 1440120
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440121
Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440122
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini hati ya kiapo ya Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440123
Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) akizunguma mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuapishwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440124
Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) akisaini hati ya kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuapa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440126
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kumuapisha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

View attachment 1440125
Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mbunge wa Iramba Magharibi) mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.
Nasikitika sana kwa kumpoteza Waziri wetu mpendwa wa Katiba na Sheria aliyepita, Mungu amrehemu. Still, nina faraja pia kwamba Mwigulu amerudi kazini tena, I really wanted this man back into the cabinet! Nafurahi kumuona amerudi kwa sababu mamlaka ya uteuzi ilikuwa na uwezo wa kuchukua mtu mwingine tofauti na yeye, lakini bahati hiyo imeangukia kwake tena. Hongera zake Mh. Waziri, kama Simbachawene tu vile, niliyasema humu juzi nikimuusia mtu alikuwa anajaribu kumchafua Mwigulu
 
Ukiachana na mapapai yaliyopimwa, Fenesi na Oil chafu Kuna Jambo kubwa Rais kaliongea hapa. Nanukuu...

"Nchi yetu inawaajiri kama Walimu, lakini tumeendelea kulipa mishahara bila hata wao kufundisha, zipo nchi zimeshindwa kulipa, niwathibitishie Walimu tutaendelea mpaka Shule zitakapofunguliwa na wafanyakazi wengine tutaendelea kuwalipa" - Rais John Magufuli.

Nchi ambazo zimeshaanza kukata mishahara ya wafanyakazi wake wa umma ni Uingereza wao wanalipwa asilimia 80 tu, Denmark wanalipa asilimia 75, Rwanda Pilots wamepunguzwa kazi na waliobakia Nusu mshahara umeondoka. South Korea wanalipa asilimia 70 tu ya mshahara.

Katika hili tunamoongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Share na waalimu wengine hili Jambo linawahusu.

1588759965537.png
 
Kwani hapa kwenu kakorona kameshaleta athari zozote za kiuchumi pia?. Si watu wanaendelea tu kuchapa kazi! Tena wengine wanachapia kwenye makazi yao watakakozikwa! Ofisi haitoshi hadi kazi zimehamia maskani.

Kama kweli kakorona kana kameathiri kaisi Cha kumsifia jamaa, leo idadi halisi ni ngapi, ukiondoa Ile ya mapapai, mafenesi na Mbuzi?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
hizo nchi ulizotaja hata wakupunguza 50 percent ya mishahara ya Walimu wao bado sio sawa na ya Walimu wa Bongo
 
NAKUMBUKA ROSE MUHANDO MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI...KUNA WIMBO MMOJA ALIWAHI KUIMBA KWAMBA UTAWABEBA KWA MBELEKO MGONGONI LAKINI WATACHANA MBELEKO...WANAZINGUA. TENDA WEMA SEPA USISUBIRI MTU AKUSIFU.....WEWE FANYA KWA WEMA TU
 
Nyie watu muwe mnaelewa kinachoongolewa kabla hamjakurupuka kuleta jamvini! Si Uingereza wala Denmark waliopunguza mishahara kwa wafanyakazi wake!

Uingereza kwa mfano, hiyo 80% sio kwamba imepunguza mishahara ya watumishi wa umma bali inalipa wafanyakazi wa sekta binafsi ambao COVID-19 imesababisha wao kukosa kazi za ujira!

Tuchukue Tanzania kwa mfano! Nasikia kuna shule binafsi zimeacha kulipa mishahara baada ya kufungwa mashule. Katka mazingira kama hayo, ndipo serikali ya UK inalipa 80% hao wafanyakazi! Na hii inatumika sana kwa wale wafanyakazi wanaolipwa kwa masaa!

Kutokana na lockdown, hawa wafanyakazi hawaendi makazini, na kwahiyo NO PAY!

Kwa suala la Denmark, soma mwenyewe hapa:-
Denmark will compensate as much as 75% of the wages for some private sector employees who face losing their jobs as the economy slows down due to the spread of the coronavirus.
Sasa unaamini mfano wako wa Magu unaendana na hao?! Huyo Magu analipa mishahara kwa kampuni ipi binafsi?!

Mkiambiwa Magufuli muongo, mnakataa!!
 
Ukiachana na mapapai yaliyopimwa, Fenesi na Oil chafu Kuna Jambo kubwa Rais kaliongea hapa. Nanukuu...

"Nchi yetu inawaajiri kama Walimu, lakini tumeendelea kulipa mishahara bila hata wao kufundisha, zipo nchi zimeshindwa kulipa, niwathibitishie Walimu tutaendelea mpaka Shule zitakapofunguliwa na wafanyakazi wengine tutaendelea kuwalipa" - Rais John Magufuli.

Nchi ambazo zimeshaanza kukata mishahara ya wafanyakazi wake wa umma ni Uingereza wao wanalipwa asilimia 80 tu, Denmark wanalipa asilimia 75, Rwanda Pilots wamepunguzwa kazi na waliobakia Nusu mshahara umeondoka. South Korea wanalipa asilimia 70 tu ya mshahara.

Katika hili tunamoongeza Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Share na waalimu wengine hili Jambo linawahusu.
View attachment 1441445View attachment 1441445
Naunga mkono hoja
 
Kwani hapa kwenu kakorona kameshaleta athari zozote za kiuchumi pia?. Si watu wanaendelea tu kuchapa kazi! Tena wengine wanachapia kwenye makazi yao watakakozikwa! Ofisi haitoshi hadi kazi zimehamia maskani.

Kama kweli kakorona kana kameathiri kaisi Cha kumsifia jamaa, leo idadi halisi ni ngapi, ukiondoa Ile ya mapapai, mafenesi na Mbuzi?



Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo ukiwafungia watu jioni saa 12 jioni Hadi saa 11 alfajiri, ndio inatosha kudumaza Uchumi? Vingine ni visingizio tu vya serikali
 
Wadanganye wasiofuatilia vyombo vya habari,Rwandair Senior Employees ambao wanalipwa mpk $13,000/month wanapunguziwa mshahara kwa 65% na wafanyakazi wa chini watapunguziwa salary kwa 8%.

Shule zote Rwanda zitafunguliwa Sept. mwaka huu na walimu wote wameambiwa wataendelea kulipwa mshahara wote kama kawaida mpk muda huo,walimu wa Private Schools wameambiwa kuna Stimulus Package inapelekwa huko Private Sector so watalipwa at least nusu ya salary yao.
 
Wanabodi,

Kwa wale wenye nafasi, ifika saa 4:15 asubuhi hii, tujiunge na TBC kuangalia matangazo ya moja kwa moja ya live mubashara kutokea ikulu ya Chato.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Tweet ya Gerson Msigwa.

Pia leo ni siku ya kimataifa ya kuadhimisha siku ya uhuru wa habari, huku Tanzania tukiwa kwenye hii vita ya kimataifa ya kupambana na janga la Corona, serikali ya Tanzania ikishutumiwa kuficha idadi ya kweli ya vifo vya Corona, hivyo tufuatilie kwa makini tukimsikiliza rais Magufuli atazungumza nini.
P

==========

View attachment 1438587

BAADHI YA NUKUU:

Rais Magufuli: Miaka ya nyuma ulikuwa ukienda kutembela sehemu ukaambiwa kuna Surua unaogopa. Leo ugonjwa huo umeonekana wa kawaida na hofu imeondoka. Ni hivyo kwa magonjwa mengi ambayo tumekuwa tukiyaona kama nchi kama TB na Ukoma. Hofu hiyo imeondoka hata kwa Ebola


Rais Magufuli: Niwaombe watanzania hili tatizo (#COVID19) litaondoka na tuendelee kuchukua tahadhari zinazotakiwa tusihusishe na uchumi wa nchi yetu.

Nchini waajiriwa zaidi ya 49% ni walimu ila tumelipa mishahara shule zikiwa zimefungwa na tutaendelea kulipa.

Rais Magufuli: Waziri Mwigulu nimekuapisha leo, itabidi mkafanye uchunguzi kwenye masuala fulani ktk maabara ya Kitaifa inayohusika kupima #Corona

Nimeona walikuwa wanatoa tu matokeo watu wameathirika tu. Nilitoa maelekezo kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakaangalie.

Rais Magufuli: Namshukuru Katibu Mkuu mpya, wameenda na kufanya yafuatayo; Tulichukua sampuli ya Mbuzi, Kondoo, Papai, Oil ya gari na kupeleka maabara bila wao kujua

Sampuli ya oil kwa mfano tuliipa jina la Jabri Hamza mwenye miaka 30, ile ilileta “negative”

Rais Magufuli: Sampuli ya Fenesi iliyopewa jina la Sara Samweli matokeo yake yalikuwa 'inconclusive'

Sampuli ya Papai tukaipa jina ya Elizabeth Anne, majibu yakawa Positive kwamba lina Corona kwamba maji ya ndani ya papai yana #COVID19

Rais Magufuli: Sampuli ya ndege Kware imekuwa ‘positive’, ya Sungura ikawa ‘indeterminate', ya Mbuzi ikawa ‘positive’, ya Kondoo ikawa ‘negative’

Sasa ukiona ya binadamu ikawa positive maana yake na mapapai yote yaweke isolation au mbuzi na fenesi wote wawe isolated.

Rais Magufuli: Ukigundua kitu hiki lazima ujue kuna mchezo wa ajabu unafanyika katika maabara hii na katika nchi hii.

Ama wahusika wa maabara wamenunuliwa na mabeberu, au hawana utaalamu; kitu ambacho si kweli au vifaa maana hadi vipamba vinatoka nje.

Rais Magufuli: Kama hadi mapapai yana #CoronaVirus basi WHO inatakiwa ifanye kazi kubwa ktk haya, na kama hadi Mbuzi wana Corona basi wanasayansi hawajafanya kazi ya kutosha

Kutokana na hizi taarifa lazima kuna watu wameambiwa ‘positive’ wakati si wagonjwa wa #COVID19

Rais Magufuli: Kuna wengine si ajabu wakafa kwa hofu. Papai halijafa lipo tu linaiva, Mbuzi yule yupo tu wala hajafa hata fenesi lipo

Natoa wito kwa Watanzania msiwe na hofu. Wale ambao hawajachoka wala kuumia kwanini uwe na hofu? Mafua yamekuwepo ila haya ni advanced.

Rais Magufuli: Kitendo cha kukuta hata papai lina #COVID19 mule ndani wala sio juu, kwasababu ingekuwa juu wangesema labda aliyegusa ana #CoronaVirus. Wametoa specification vizuri kabisa, walichoma ndani wanachukua sampuli. Mbuzi, papai, fenesi na Kware wawe na Corona?

Rais Magufuli: Kuna vitu vingi vya kujiuliza, huenda kuna kitu hakijaeleweka kwa wanasayansi lakini hata dunia hawajakielewa

Natoa wito kwa wanaotumia vifaa hivi hasa Afrika, wachukue sampuli ya kitu chochote hata ukuta, mjusi watakuja kuthibitisha haya.

Rais Magufuli: Tuendelee kuchapa kazi, uzalishaji uendelee maradufu, tusitishane. Wanasiasa waache kuitumia #COVID19 kama agenda, haitasaidia

Mtu anasema funga Dar, funga Tanga, sifungi nilishasema. Ni lazima Watanzania tuchape kazi na kuendelea kuchukua tahadhari.

Magufuli: Inawezekana fenesi, papai lingekuwa linasikia kuwa lina #COVID19 lingekuwa limeshaoza kabisa. Lakini kwa vile halisikii, lina #CoronaVirus na bado lipo

Sasa wewe kama Waziri (Nchemba) mkashirikiane na Wizara ya Afya mkaangalie hiyo Maabara ya Taifa kuna nini?

Rais Magufuli: Mbeleni ninafikiria hata kuruhusu ligi iendelee ili watu wawe wanacheza tukiangalia kwa TV. Tuweke utaratibu mzuri.

Ninaelewa hata walioathirika na #COVID19 sijaona mwanamichezo aliyedhurika sana. Hii ni wazi kuwa wanaofanya michezo #Corona inawakwepa.

Rais Magufuli: Kama tunazuia hata kucheza mpira maana yake tunawaambia wapate #Corona. Najaribu kusubiri wataalamu wanishauri vizuri

Inawezekana tunaishi na huu ugonjwa kama watu wenye UKIMWI, TB, Surua na maisha yakaendelea. Tuache kuogopana na kutishana.

Rais Magufuli: Ninajua wapo wengine wangependa kuzungumza kuhusu #Corona. Naona na vyombo vingine vya habari wao ni corona tu, tena vya nje na huko vinapotangazia ndio imeua watu wengi

Lazima mjiulize kwanini havizungumzii ya kwao wanaongelea ya #Tanzania?

Rais Magufuli: Natoa wito kwa hasa vijana ambao kila siku wakimuona mtu amekufa ni #COVID19

Jaji Mkuu (Augustino Ramadhani) tumehangaika naye hapa kwa mwaka mzima, si vizuri kutaja matatizo yake. Baba yangu kafariki kwa saratani kama Jaji Mkuu ila watu wamebadili maneno ya ajabu.

Rais Magufuli: Si kila anayekufa ni #Corona. Malaria inaua, ajali inaua. Juzi Mkuranga wamekufa watu 21 kwa ajali, roho zao Mungu azipumzishe kwa amani

Siku hizi mtu hata akijifia chumbani kwake wanapoenda kuchukua ile maiti ni Corona. Ninawaomba Watanzania tubadilike.

Rais Magufuli: Nawapongeza madaktari, manesi na watendaji wa Wizara ya Afya kwa kuendelea kuhudumia Watanzania ktk kipindi hiki.

Kuna mengi ya kushangaza nchini. RC wa Mtwara nikamsikia kwenye vyombo vya habari eti "DC huyu hawezi kusafirishwa kwenda kwao", inasikitisha.

Rais Magufuli: Kama madaktari wanaenda kuwaona wagonjwa wakiwa na PPE. Walishindwaje viongozi wa Mkoa wa Mtwara chini ya RC kuifunga maiti PPE na kuipeleka Moshi?

Niwaombe viongozi wenzangu tusichukue hili kwa papara, tuwatumie wataalam kupata ushauri utakaosaidia.

Rais Magufuli: Ninaamini #CoronaVirus ipo ila si kwa 'extent' hiyo. Katika siku 2-3 zilizopita tulikuwa na watu 16 waliofariki kwa #COVID19

Sasa tafuta uwiano wa watu 16 na idadi ya watu karibu mil. 60 na uwiano wa nchi nyingine na idadi yao ya waliokufa halafu utaona.

Rais Magufuli: Tunawatisha Watanzania wanaogopa hata kwenda kufanya kazi au sokoni

Nilisoma kwenye WhatsApp mtu anasema “funga masoko”. Nikajiuliza huyu ana akili za kawaida? Hapo alipo hana shamba wakifunga masoko atapata wapi chakula? Tena yupo Dar, ni “shortsighted”

Rais Magufuli: Ukizuia soko la Kariakoo, watu milioni 6 wa Dar watakula wapi? Wabaya wetu wanataka tuingie kwenye ujinga huo.

Nchi zilizofunga mnaona matokeo yake. Sitaki kuzitaja ila kuna nchi watu wamekufa zaidi ya elfu 50 na zina uwezo wa kila kitu.

Rais Magufuli: Tuchukue tahadhari na kuwapuuza wanaojaribu kututisha, hawana maana. Tuendelee kumuomba Mungu.

Kuna Viongozi wengine wa dini wamemsahau Mungu, wameanza kuyumba na wameanza kuweka ubinadamu mbele. Wanasema tuache kuomba ili tujiokoe. Ni mambo ya ajabu!

Rais Magufuli: Hali si mbaya kama tunavyotishwa, sisi tupo vizuri na biashara zinaendelea ndio maana hata tunaweza kulipa mishahara.

Hata hao wanaosema tufunge huku anaendeshwa na gari limeandikwa STK, mafuta anawekewa na Serikali, amesahau alichokalia ndicho kinamlisha.

Rais Magufuli: Ninawasiliana na Madagascar na wameandika barua wanasema kuna dawa imepatikana. Tutatuma ndege ili ziweze kuletwa nchini.

Serikali tunafanya kazi usiku na mchana. Wengine wanasema nipo Chato, kwani waliambiwa sitakiwi kuwa huku? Huku si ndiko nitazikwa?

Rais Magufuli: Tunatakiwa kusimama pamoja. Nampongeza Mbatia (James) ni mwanasiasa mzuri. Wakati wa vita ni vita wote tushikamane twende mbele

Mpaka ananiandika SMS " Uwe na moyo mkuu, tuendelee kuchapa kazi". Ni wa Upinzani ila ni muelewa unajua yupo kwa ajili ya nchi.

Rais Magufuli: Kuna mwingine anazungumzia Dar wala hayupo Bungeni "Leo tumeahirisha kwenda Bungeni". ACHA!

Nimetoa maelekezo hakuna kuwalipa posho. Utalipwaje wakati huifanyii kazi? Usipoenda watakulipa hao mababeru wanaokutumia kuzungumza hayo unayotaka kuzungumza.
Wandugu, hapa nafanya tuu follow up ya Corona nikipitia kujikumbusha niliwahi kuandika nini au kusema nini kuhusu Corona na hiki kinacho endelea sasa. Corona is real tusifanye masihara, tujilinde kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.

Kila Jumamosi asubuhi kuanzia saa 1:30 hadi saa 3:00 asubuhi , Star TV, huwa ninakuwa live kwenye kipindi cha TV cha Jicho Letu Ndani ya Habari ambacho huwa kinatangwa live na Star TV kila siku za Jumamosi asubuhi, kwa Jumamosi ya kesho, mgeni wetu ni Waziri wa Habari, Dr. Harrison Mwakyembe tukijadili kuhusu athari za Corona kwenye sekta ya Habari, nini kifanyike.

Ukipata nafasi karibu utufuatilie.

Powa
 
Dah!!! tumetoka mbali kumb alishawahi kuvaa nguo aina ya shift!!!
1615389588744.png
 
Wanabodi,
leo ni siku ya kimataifa ya kuadhimisha siku ya uhuru wa habari, huku Tanzania tukiwa kwenye hii vita ya kimataifa ya kupambana na janga la Corona
P
==========
View attachment 1438587
Wanabodi, mimi ni miongoni mwa wana jf, tuliandika mengi kumhusu rais wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, hivyo kipindi hiki cha maombolezo, napitia baadhi ya mabandiko kwa ajili ya kumuaga rasmi.

Japo umetangulia, lakini kauli zako, maono yako na kile ulichokiamini, kitabaki na sisi Milele.
Sisi tulikupenda, lakini Mungu amekupenda zaidi.
Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe!.
Raha ya Milele Umpe Ee Bwana, na Mwanga wa Milele, Umuangazie, Apumzike kwa Amani...Amina x3.
RIP Dr. John Pombe Joseph Magufuli
Buriani ya kuonana...
Paskali
 
Back
Top Bottom