Raha ya milele umpe ehee bwana na mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani...Poleni Chadema na familia nzima ya Mtema kwa msiba mkubwa uliowafika..
Njia uliyoiendea ni njia ya ulimwengu wote, umetangulia sisi tupo nyuma yako tunakuja huko. Mwenyezi Mungu utuongoze sisi waja wako pindi mauti ikitufika tulale na tusife, ili ujapo tufufuliwe nawe na kwenda katika makao ya amani mbinguni. Amen
wanaharakati wa mageuzi,tumeondokewa na mmoja wawapigania haki za wanyonge,kuvunjika koleo si mwisho wa uhunzi,changamoto ulizotuachia katika kipiindi hiki kigumu ni chachu ya maendeleo katika harakati za kulikomboa taifa hili toka kwenye mikono dhalimu ya wachumia tumbo.Mungu ilaze mahali pema peponi roho ya mwanamapinduzi Regea Mtema ameen
Nawapa pole wote tulioguswa na Msiba wa Mwanaharakati, Dada, na Mpiganaji wetu Regia Mtema, kazi ya Mungu haina makosa, tumshukuru Mungu kwa kila Jambo, Bwana alitoa na Bwana alitwaa na Jina la Bwana na Lihimidiwe, Amina
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.