Kutoka Bungeni - Jumamosi 21, Aprili 2012 (Videos)

Mnyika: Mfumko wa bei unatokana na Ufisadi na kukosekana kwa uwajibikaji

Pamoja na kutoa rai kwa Waziri wa Fedha kujiuzulu

Twende mbali kidogo na kufanya UKAGUZI MAALUMU maana misamaha sasa inafika TRILIONI MOJA

Tutagundua madudu mengi na kuchukua hatua kali kwa wahusika licha ya kutoa rai kwa wao kujipima na kufanya maamuzi ya busara kwa kuachia ngazi

Deni la Taifa limeongezeka na hali ya Uchumi ni mbaya

Anahamia katika Taarifa ya kamati ya Madini na Nishati
 
kuhusu msongamano dar es salaam, mnyika anaona tatizo ni utashi wa kisiasa tu!
 
Anamshangaa Ngeleja kuendelea kuwepo Ofisini mpaka sasa pamoja na madudu yote na makandokando yake

Anamtaka Raisi kutumia Mamlaka yake kumwajibisha na kusafisha serikali yake
 
Mnyika aiomba serikali kuunda kamati teule itakayochunguza malalamiko dhidi ya Ujenzi wa gati inayomkabili Nd. NUNDU kwani kuna madudu mengi yamefichika hapo
 
Hamna kitu yule nilizima tv mimi amekwisha maliza sio ni washe tv
 
Anahitimisha Mnyika kwa kuhoji Ripoti ya MUHESHIMIWA MASHA kuhusu nyongeza yab Posho za Askari wa Jeshi la Polisi kuwa iletwe Bungeni maana toka mchakato huo utolewe kimya mpaka leo na zoezi lilifanyika


MY TAKE: UFISADI MWINGINE HAPO, Huyu Jamaa alishalambishwa mchanga sasa itakuwaje au ndo atalamba na Reli kabisa kama mbuzi

 
Spika Makinda to Mbowe "una bahati Jambazi lako limekuwahi kuomba mwongozo sivyo ungekosa nafasi" Mnyika aliomba mwongozo kabla ya Mbowe kuongea

Mkuu lemonade nilifikiri nimesikia vibaya huyu mama alivyotamka kumbe na wewe umesikia? Hivi huyu ,mama ni mtu wa aina gani? Nimeamini hii sera ya 'mbayuwayu' ya 'kuwawezesha wanaweza' itakuja kuangamiza taifa. Mwanamke afanye kama anaweza hana haja ya kuwezeshwa, hii tabia ya kuwezeshana inaleta kaharufu ka kupendeleana katika mambo ya msingi...
 
Nyie watu wa JF mnaoona live huko bungeni mtupe habari za ukweli na si kuanzisha mada halafu mnakula kona.Wengine hatuna tv tunategemea habari nyingi toka hapa.
 
Hapo awali wakati nakamata Gahwa kidogo Myika aliomba muongozo kuhusu maelezo yanayotolewa na wabunge na kuupotosha Umma kutokana na kuwa na masilahi katika Taasisi wanazozitolea maelezo akimtaja SOPHIA SIMBA ambaye alilidanganya Bunge kuhusu TAASISI YA WAMA (Wanawake na Maendeleo ya Mama VASCO) na kumbe katika orodha ya wajumbe wa Bodi Mama SIMBA ni Mjumbe.

Mnyika Kahitaji Muongozo

Katika Hali isiyo ya Kawaida

SPIKA Kajibu kienyeji tu kuwa yeye haijui WAMA na kuwa anahitaji kujiridhisha kama ni Taasisi, Shirika Binafsi au la serikali na atatoa maelezo baadaye

Sasa sijui alikuwa kama anapotezea, Sanifu au ndo kanuni

Tunamsubiri,

MY TAKE: Harakati zimebisha HODI Magogoni kupitia Mlango wa UANI...TWENDE
 
Mnyika na wenzake wote wametoka nje ya mada! Thanx Anne kwa kuwarekibisha!
 
just info: kuna siri nzito juu ya kujiuzuru kwa mawaziri ..linaweza lisitokee
 
Saalaaaaam

Kumekucha baada ya hekaheka za jana huku macho na masikio yakiendelea kutosadiki yanayotarajiwa kujiri hasa baada ya kigugumizi kuwatawala wanaokusudiwa kufunguwa midomo yao kupaza sauti itakayokata mzizi wa fitna na kufungua ukurasa mpya wa historia ya uwajibikaji katika Serikali ya Awamu ya Nne.

Kwa ujumla wabunge wanaoonekana kuranda hapa katika viwanja vya bunge ni wachache saana, sijui wengine wako wapi na ORDER PAPER haionyeshi kama PM kapangiwa kusema jambo licha ya kuwa yeye a kama mtendaji mkuu wa serikali hawajibiki kufanya hivyo kwani wakati wowote anaohitaji kutoa taarifa kwa maelekezo na mwasiliano na Spika anaweza kufanya hivyo.

Tafakuri ni zito, na muda punde Bunge litaanza

Upande anaopitia PM ulinzi upo kuashiria anakuja na muda wowote atafika hapa mjengoni

Yapi yatajiri, Endelea kubaki JF


ADIOS

Thanks kwa taarifa,
Mbona Arusha Mambo FM wametutosa leo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom