Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
Muda Mfupi uliopita Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda kamaliza mazungumzo na Waandihi wa Habari wa Vyombo mbalimbali na kusisitiza kuwa Taarifa kamili kuhusu Mawaziri wanaodaiwa kujiuzuru atazitoa rasmi Jumatatu atakapokuwa akiahirisha kikao cha Bunge.
Maswali ni mengi kwa kila nayeisikia kauli hii:
- Nini kimejitokeza hapa
- Kuna aliyezuia maamuzi haya yasipate baraka?
- PM kashikwa na kigugumizi gani?
- Mbona kila jambo katika kiako cha jana yalishafahamika mpaka maazimio?
- Kikao cha leo kilikuwa na Agenda gani?
- Ni kweli anasubiri baraka za Rais?
- Ilikuwa sanaa?
- Au ni mchezo gani unataka kufanyika hapa?
- Kwa nini Spika kaahirisha Bunge bila kuusoma Muongozo uliohusu ufafanuzi wa Serikali juu ya suala hili?
- Kwa nini wameiacha nchi katika sintofahamu kiasi hiki?
Ahadi yake ni Jumatatu
Game limeishia hapo kwa leo, Ila TUPO Dodoma na hakuna cha Mnadani wikiendi hii ni kona hadi kona hata kama yatakuwa maamuzi ya kushtukiza kama jana USIKU ghafla wakaghairi kuwapa niuz wanahabari. WE ARE MONITORING
Tunaendelea kusubiri
ADIOS
Ahsante sana Mkuu kwa kazi nzuri.