Kutoka Bungeni - Jumamosi 21, Aprili 2012 (Videos)

Muda Mfupi uliopita Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda kamaliza mazungumzo na Waandihi wa Habari wa Vyombo mbalimbali na kusisitiza kuwa Taarifa kamili kuhusu Mawaziri wanaodaiwa kujiuzuru atazitoa rasmi Jumatatu atakapokuwa akiahirisha kikao cha Bunge.

Maswali ni mengi kwa kila nayeisikia kauli hii:

  1. Nini kimejitokeza hapa
  2. Kuna aliyezuia maamuzi haya yasipate baraka?
  3. PM kashikwa na kigugumizi gani?
  4. Mbona kila jambo katika kiako cha jana yalishafahamika mpaka maazimio?
  5. Kikao cha leo kilikuwa na Agenda gani?
  6. Ni kweli anasubiri baraka za Rais?
  7. Ilikuwa sanaa?
  8. Au ni mchezo gani unataka kufanyika hapa?
  9. Kwa nini Spika kaahirisha Bunge bila kuusoma Muongozo uliohusu ufafanuzi wa Serikali juu ya suala hili?
  10. Kwa nini wameiacha nchi katika sintofahamu kiasi hiki?


Ahadi yake ni Jumatatu

Game limeishia hapo kwa leo, Ila TUPO Dodoma na hakuna cha Mnadani wikiendi hii ni kona hadi kona hata kama yatakuwa maamuzi ya kushtukiza kama jana USIKU ghafla wakaghairi kuwapa niuz wanahabari. WE ARE MONITORING

Tunaendelea kusubiri


ADIOS

Ahsante sana Mkuu kwa kazi nzuri.
 
Waziri wa viwanda na biashara Mh.Cyril Chami (Moshi Vijijini), japo amekiri yuko tayari kujiuzulu sisi wapigakura wake tunamwambia ni bora aachie ngazi mapema maana piga ua hatorudi bungeni ng'o 2015 hata kwa dawa na Mbege.

Amedanganya wazee wetu sana kwa ahadi hewa-najua anawaza kujifajiri na ujenzi wa kabarabara, huku ni Mwizi. Hato rudi bungeni 2015 huyo Chami
 
kule kuhema kwa omari nundu ni ishara tosha ya ku-panic,hiyo haihitaji uwe mtaalamu wa "uchunguzi watu" kulijua hilo,wasiwasi wangu ni kuwa kuna siku watakuja kudondoka kwa presha,hongera kamanda zitto kwa hoja yako nyemelezi na chokonozi,lazima watambue kuwa watanzania wamechoshwa na ushetani wao.
 
kule kuhema kwa omari nundu ni ishara tosha ya ku-panic,hiyo haihitaji uwe mtaalamu wa "uchunguzi watu" kulijua hilo,wasiwasi wangu ni kuwa kuna siku watakuja kudondoka kwa presha,hongera kamanda zitto kwa hoja yako nyemelezi na chokonozi,lazima watambue kuwa watanzania wamechoshwa na ushetani wao.
 
Asante sana GR,JF idumu daima,, twende kwenye soka sasa Arsenal then Barca woooooo
 
hata kama hawatakubaliwa kujiuzulu nature itaendelea kuwapush aside, ikumbukwe mawaziri wote hawa wamekubwa na zimu la kujiuzulu toka mwaka jana wakati wa bunge la bajeti
 
Baraza lote la mawaziri livunjwe tu JK ajipange upya atafute damu changa,atuondolee vizee vilafi na mafisadi

Tatizo kubwa ni kwamba waziri ni lazima awe mbunge; na ukiangalia wabunge wa CCM awamu hii wengi wamebebwa (sio competent). Katika wabunge wa CCM ni wachache sana ambao hawajawahi kuwa mawaziri ( na sina uhakika kama wapo watakao weza uwaziri - labda from Zanzibar) . Ebu angalia Lusinde, Prof. Maji Marefu, Komba, viti maalum ndio usiseme. In short JK sijui atatoa wapi mawaziri wachapakazi wakati wabunge wenyewe hoi. Kama wengine walivyo suggest kuna haja yakuvunja kila kitu tuanze upya. It might be very costly lakini it is better tukaanza na kitu kinachoeleweka kuliko hivi viraka viraka tunavyoweka. Ingekuwa vizuri ifanyike namna yakumuwajibisha raisi mwenyewe (wenye kujua sheria/taratibu watusaidie) otherwise hii pot inachemka nafikiri kuifunika hakutasaidia.

 
haha pole kijana, watu wapo mnadani wanakula nyama ya mbuzi yenye kuwekwa nyongo. Nzuri zaidi wapo na mwanao wakike au dadako wakimuwezesha kwani boom lishakata. Hongera kwa kupata mkwe/shemeji gamba/gwanda
Ningekuwa naambiwa mm LAZIMA ningepigana au ningepigwa ban humu jamvini, ban la nne tokea niingie rasmi JF 2009!
 
Duh...nchi kweli inapita kwenye changamoto nzito...tuendelee kuomba mungu aachilie hekima yake na maongozi yake
 
Mbowe anawahamsisha watanzania wote viongozi wa Dini, vyama vya siasa na wadau wote katika mchakato wa katiba kuifikiria kwa kina Hoja ya Serikali za Majimbo na DECENTRALIZATION ndio utakuwa ufumbuzi wa matatizo haya ya watanzania, hata kama mabadiliko ya mawaziri yatafanyika bila kubadili mfumo huu ambao CDM imeshatoa mwelekeo katika sera yake ya MAJIMBO hakuna mabadiliko yatakayotokea

MBOWE KAHITIMISHA

KANGE LOGOLA NDEGE anazungumza

Ghost Ryder,

..mimi sikubaliani na serikali za majimbo.

..tunataka kujenga Tanzania moja na siyo kuturudisha kwenye migawanyiko ya umajimbo.

..kuleta serikali za majimbo ni kuongeza nafasi za watawala na wanasiasa, pamoja na gharama za kuwahudumia.
 
GHOST RYDER

Hongera sana mkuu kwa ulichoamua kukifanya. Nakupa hongera kwa siyo hizo updates zako. Hizo naziona ni za muhimu lakini si muhimu sana kama suala hili uliloamua. Muundo wa kutoa hizo updates nimeufuatilia sana toka jana ulipoanza kuitoa hiyo thread. Badala ya kurundika rundika nyuzi za ajabu na ambazo zingehesabiwa kama tetesi kwa wale ambao wanadhani kila lisemwalo ni tetesi bila ya kuangalia huyo anayeongea yupo katika position ipi, wewe kwa ufundi umeamua ile thread ya mwanzo ndio unayoiendeleza ili kuipa uhalisia wake.

Yapasa kuigwa. Nakutakia kazi njema hapo bondeni ulipo, maana mi niko kwa juu kidogo hapa.
 
Spika Makinda to Mbowe "una bahati Jambazi lako limekuwahi kuomba mwongozo sivyo ungekosa nafasi" Mnyika aliomba mwongozo kabla ya Mbowe kuongea

Hii ina maana kuu mbili, either wakiwa nje huwa wanataniana sana na kuitana majina ya ajabu ajabu (which is normal) if they don't take it personal or Spika akiwa nje huwa anawaita wapambanaji wa CDM majambazi bila ya wao kujua.

Japo anaweza kujitetea kuwa ali-misspoke. Ila hii statement hata mimi ilinistua kiasi kuwa huenda spika ana kitu moyoni kinamsumbua sana kuhusu CDM japo sheria za bunge hazimruhusu kuonesha chuki dhidi ya chama chochote ila bunge lionekane ni impartial.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom