Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Mr.Toyo

JF-Expert Member
Feb 9, 2007
433
117
Wangwe agoma kufuta kauli yake bungeni

MBUNGE wa Tarime Chacha Wangwe amekataa kufuta kauli yake ya Julai 10, mwaka jana kwamba kulikuwepo na vitendo vya vurugu na mauaji wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa wa Rais na wabunge katika Jimbo la Tarime, Desemba,2005.

Mbunge huyo alisema hayo katika waraka aliomwandikia Spika wa Bunge Samuel Sitta, akisema yeye mwenyewe na wanachama, wananchi na wapiga kura wa Jimbo hilo waliathirika moja kwa moja na vurugu, majeraha na mauaji hayo na kwamba hakutoa kauli hiyo kwa urahisi au kwa kuifurahia au bila kufikiria uzito wake.

“Nilitoa kauli hiyo kwa kuelewa fika uzito wake lakini kwa kutegemea kwamba ingefanyiwa kazi na vyombo vinavyohusika ili hatua za kinidhamu au kisheria kuchukuliwa dhidi ya waliohusika na vitendo hivyo vya kihalifu.

“Suala la tafsiri ya ya kauli yangu halikuwa na haliwezi kuwa ni hoja ya msingi. Kwa hiyo, sidhani kama ni sahihi au halili kwa mimi kuadhibiwa kwa kusema ukweli ambao hata hivyo umetafsiriwa na Mheshimiwa Spika,” alisema Wangwe.

Mbunge huyo katika waraka wake aliomwandikia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano alisema hawezi kufuta kauli yake kwa kuwa Kamati ya Bunge imethibitisha ukweli wa kauli yake.

Katika waraka huo alisema kuwa anafahamu fika kwa msimamao huo anaweza kuadhibiwa na Bunge na kwamba hata kama ataadhibiwa itakuwa ni kwa sababu ya kusema ukweli uliothibitishwa na Kamati iliyoundwa na Spika.

“Nilitegemea baada ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama kuthibitisha ukweli wa kauli yangu, Mheshimiwa Spika ungevielekeza vyombo husika kuifanyia kazi kauli hiyo na ripoti ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama,” alisema Wangwe katika sehemu ya waraka huo.

Mbunge huyo alisema kwa kuwa aliitoa kauli hiyo ndani ya Bunge na alitakiwa kuithibitisha mbele ya Bunge, alitegemea kwamba ripoti ya kamati hiyo ingetolewa hadharani kwa Wabungeni ili nao wafahamu ukweli au uongo wa kauli yake.

Alisema alitegemea kuwa angepatiwa nakala ya ripoti ya Kamati hiyo ili ajue ni uongo upi hasa anaotakiwa kuufuta kusudi asiadhibiwe na Bunge.

“Yote haya hayajafanyika kwa sababu ambazo ni wewe mwenyewe unayaweza kuzifahamu au kuzielezea. Kwa maana hiyo, siko tayari kufuta kauli ya kweli na ambayo ukweli wake umethibitishwa na Kamati ya Bunge.” Alisema Wangwe.

Mbunge huyo alisema kuwa haoni sabuabu ya kufuta kauli yake kwa kuwa Kanuni za Bunge haziruhusu wala kuunga mkono tafsiri ya kauli ya Spika juu ya kauli yake (Wangwe) na kwamba hadhani kama ni sahihi au halali kwa yeye kuadhibiwa kwa kusema ukweli.
 
Maana Mzee Ndesa amekuwa indicted na wangwe anaweza kukabidhiwa kwa DCI .CCM bwana wana mbinu za kijingaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Absolutely nonsense, hivi ni nani ambaye anafanya mambo kama haya katika karne hii, wabunge lazima wasimame kidete na hii serikali ambayo inaonekana kubana uhuru wa wabunge. Who is this Idiot?
 
Way to go Chacha. At least you show the way how our MP should move forward the agendas. Not for their own good, but for all Tanzanians. The parliament should put the government in check for all the dubious stuff they do on every single day.

We will back you up, just make a list and we will sign.
 
Wangwe kuadabishwa na kamati iliyojadili akina Mengi na Malima

*Spika Sitta asema ameonesha utovu wa nidhamu
*Ni baada ya kukataa kufuta kauli yake ya mauaji


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Samwel Sitta, ameitaka Kamati ya Maadili,Haki na Madaraka ya Bunge, ikutane mara moja na kumchukulia hatua Mbunge wa Tarime, Bw. Chacha Wangwe (CHADEMA), ambaye amekataa uamuzi wa Spika wa kufuta kauli aliyoitoa bungeni Julai 10 mwaka jana.

Bw. Sitta alisema hayo bungeni jana kabla Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa hajaahirisha Mkutano wa Sita wa Bunge.

Alisema kutokana na mbunge huyo kuamua kutofuata kanuni za Bunge na kukaidi agizo lake Spika na kutaka kuanzisha malumbano ni utovu wa nidhamu na hivyo kuiagiza kamati hiyo ikutane na kujadili hatua za kumchukulia mbunge huyo.

"Tangu jana kwa busara zangu, namwomba mbunge huyo wa Tarime afute kauli yake, lakini naona yeye hayuko tayari kwa hilo na ninavyoona anataka malumbano nami, kitu ambacho nakiona kuwa ni utovu wa nidhamu, naiagiza kamati hiyo ikae mara moja leo (jana), ili kuangalia hatua za kumchukulia mbunge huyu," alisema Bw. Sitta.

Kauli ambayo mbunge huyo alitakiwa aifute ni aliyosema kuwa kulitokea mauaji, vitisho na majeruhi kuhusiana na masuala ya kisiasa jimboni mwake, katika kipindi cha uchaguzi mkuu mwaka juzi.

Alisema kwa vile mbunge huyo amekiuka kanuni ya 50 (1) ya Bunge, kipengele hicho ambacho kinapiga marufuku mbunge kusema uongo bungeni, vile vile inawataka wabunge kuwa na uhakika na maneno wanayoyatoa kuwa ni sahihi, kuwa Bw. Wangwe aadhibiwe na kamati hiyo, kutokana na utovu wake wa nidhamu bungeni.


Source: Majira
 
Mbowe adai wapinzani wanakandamizwa bungeni

Na Muhibu Said

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amelishutumu Bunge akidai kwamba limekuwa likiwakandamiza wabunge wa kambi ya upinzani wanapoikosoa serikali.

Mbowe alitoa shutuma hizo alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili cha Kamati Kuu ya Chadema, kilichoanza katika jengo la Haidary Plaza, jijini Dar es Salaam jana na kuhudhuriwa na muasisi, Edwin Mtei na mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Bob Makani.

Hata hivyo, Mbowe hakufafanua shutuma hizo dhidi ya Bunge, lakini akaahidi kuwa chama chake kitatoa tamko rasmi leo baada ya Kamati Kuu kujadili suala hilo, namna serikali ya Rais Jakaya Kikwete inavyoipeleka nchi tangu iingie madarakani mwaka juzi na hali ya chama hicho.

"Bunge linakandamiza haki. Wabunge wa upinzani wanakandamizwa bungeni," alilalamika Mbowe.

Alisema serikali imeshindwa kuwaletea maisha bora Watanzania kama ilivyowaahidi, badala yake imekuwa ikikusanya mapato kwa nguvu kama mbinu ya kuficha aibu ya kushindwa kutimiza ahadi zake.

Mbowe alisema Chadema imesikitishwa na kauli mbalimbali za kisiasa zinazotolewa na baadhi ya viongozi wakuu wa serikali, akiwamo Waziri Mkuu, Edward Lowassa kwamba, uchumi wa nchi unapaa wakati hali ya maisha kwa wananchi wa kawaida ni mbaya.

Alisema Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, aliahidi kuwa bei ya mafuta haitapanda, lakini katika baadhi ya mikoa aliyoitembelea katika siku za karibuni, ameshuhudia bei ikiwa juu kutokana na kutokuwa na udhibiti wa kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.

Alisema pia nyongeza ya mshahara ya Sh9,000 kwa mwezi iliyotangazwa na serikali bungeni hivi karibuni, haikufanywa kwa moyo wa kuwapunguzia wananchi wa kawaida ukali wa maisha
 
Nasikia hoja zote zinazohusu hotuba za EL na Bi Mkubwa zimekuwa zikizimwa kabla moto wake haujawashwa!. Kuna hata baadhi ya wabunge ndani ya CCM wamekatazwa kuuliza baadhi ya maswali. Navyosikia (sijui kama ni kweli) Bunge hukusanya kwanza maswali na kuyapitisha yanakohitajika kupewa jibu kwa hiyo ni rahisi kuwekewa vikwazo mapema kabla hujakiwasha!
 
For those with eyes to see (Bunge is live on ITV and Star TV )and ears to hear this is all very obvious.At times they get paranoid. They also at times look very insecure as if to say ie.body language,I hope the Speaker will come to our rescue before this goes too far.This is probably the only country in the world where you can carry on believing that you can " FOOL ALL OF THE PEOPLE ALL OF THE TIME "
 
Nasikia hoja zote zinazohusu hotuba za EL na Bi Mkubwa zimekuwa zikizimwa kabla moto wake haujawashwa!. Kuna hata baadhi ya wabunge ndani ya CCM wamekatazwa kuuliza baadhi ya maswali. Navyosikia (sijui kama ni kweli) Bunge hukusanya kwanza maswali na kuyapitisha yanakohitajika kupewa jibu kwa hiyo ni rahisi kuwekewa vikwazo mapema kabla hujakiwasha!

Mkandara,
Wabunge CCM vipi? Ndo maana vyombo vya habari mara nyingi tunasikia tu habari za upinzani- utadhani CCM hawapo!
 
Mzalendohalisi,

Ndani ya CCM wamo watu wazuri ambao wanaelewa kuwa nchi hii sasa inatawaliwa badala ya kuongozwa. Hawa ni wazee wetu, marafiki zetu na wengine huchelea kupiga makofi anaposimama mbunge wa Upinzani. Sii kwa sababu ya umaarufu wa mtu huyo ila wanajua kuna moto unawashwa!..
Wao kama wabunge wa CCM ambao wanajua fika kwamba kama sio nguvu ya mtandao wasingeipata ajira hiyo... na wakuu hawa wa chama ndio waajiri wao sio wananchi.
nafikiri tunapozungumzia sana Wapinzani ni kwa sababu wao hawawezi kumeza funda la mate na kumwachia Mungu.. huyatoa mawazo yao wazi, wakati hao wa chama tawala hufutika kurasa zao na kushika tama kusubiri wakati wa makofi!
 
kuna haja ya watanzania kuelikishwa ili waweze kujua kosa la kupeleka watu bubu bungeti kwani hili linaligarimu taifa zima bila kujali ni upinzani ama ni ccm.

kuna siku kitaeleweka tuu.
 
Slaa aondoa hoja ya BoT, adai hakuna jema bungeni

*Aenda kushtaki kwa wananchi
*Ikishindikana, kuchongea kwa wafadhili
*Adai ameanza kutishiwa maisha yake


Na Waandishi Wetu, Dodoma

MBUNGE wa Karatu, Dk Wilbrod Slaa (Chadema), amefuta kusudio lake la kuwasilisha bungeni hoja binafsi ya kutaka iundwe kamati teule kuchunguza ubadhirifu katika taasisi nyeti za umma, ikiwamo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kile alichoeleza kuwa Spika wa Bunge, Samwel Sitta, hajaiweka hoja hiyo katika shughuli za Bunge tangu alipoiwasilisha.


Dk Slaa alitangaza kufutwa kwa kusudio hilo mbele ya waandishi wa habari mjini hapa jana, huku akieleza kuwa suala hilo limezua mzozo ambao utakuwa na madhara kwa mustakabali wa Tanzania. Pia, mbunge huyo alitangaza mchakato mbadala wa kutaka suala hilo sasa lianze kushughulikiwa kwa njia mbalimbali ili hatimaye ukweli uweze kudhihiri na kuwekwa wazi.

Akiongozana na wabunge karibu wote wa kambi ya upinzani, akiwamo Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohammed (Wawi-CUF), Dk Slaa alisema uamuzi huo umefikiwa baada ya kubaini kutokuwapo kwa dhamira thabiti na dhati ya Bunge, chini ya Spika Samwel Sitta kuweza kukaa, kusikiliza, kujadili suala hilo nyeti wakati wa kikao cha Bunge kinachomalizika leo.

Licha ya kuvipongeza vyombo vya habari nchini kwa kuwezesha kufichuliwa kwa maovu mengi, Dk Slaa alieleza kuwa vikwazo alivyowekewa tangu mwanzo na Spika Sitta alipoamua kueleza dhamira ya kuanza rasmi mchakato huo, vimemkatisha tamaa. Jumanne asubuhi, kabla ya Bunge kuanza kusikiliza hoja binafsi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini (aliyesimamishwa), Zitto Kabwe, Spika Sitta alieleza kwa ufupi kuhusu hoja ya Slaa.

Alieleza kuwa suala hilo ni zito, lakini linalohitaji ushahidi, lenye kumtaka pia yeye (Spika) ajiridhishe kwanza na ushahidi wowote ambao unawasilishwa kwake na mtoa hoja (Slaa). Akizungumza kwa umakini mkubwa, lakini wenye kuonyesha dhahiri hasira, Dk Slaa alieleza kuwa licha ya kutotakiwa na kanuni za Bunge kumridhisha kwanza Spika Sitta kabla ya kuamua kuwasilisha hoja binafsi, lakini Agosti 13 aliwasilisha ushahidi na vielelezo vyote.

Jambo hilo alisema alilifanya ili kuthibitisha unyeti wa suala lenyewe na kuonyesha kitabu ambacho alisema ushahidi umekusanywa kwa umakini mkubwa kutoka hata ndani ya taasisi za serikali kwa mujibu wa sheria. Aliyataja maeneo mahsusi ambayo hoja yake ilikuwa imejielekeza zaidi kuwa ni makampuni ya Mwananchi Gold, Meremeta, Tan Gold na Land Gold na kuongeza kuwa ushahidi wote ulikuwa katika vipengele A-F.

Alieleza mshangao kuwa licha ya Spika kukabidhiwa tangu Agosti 13, lakini hadi jana hakuwa ameonyesha dhamira ya kuiweka hoja hiyo katika taratibu za mikutano ya Bunge. "Ni dhahiri kwamba tumebaini licha ya uzito wake, lakini hoja hii nzito yenye maslahi kwa wananchi inaendelea kupigwa danadana na kutokana na uamuzi huo tumeamua kutafuta njia nyingine kulishughulikia ikiwa ni pamoja na kukata rufaa kwa wananchi," alisema Dk Slaa na kuongeza;

"Tuna wasiwasi kwamba hizo ni mbinu za makusudi za kuificha ili isiweze kufahamika kwa wananchi wetu ambao ndio wametutuma na kutuingiza hapa bungeni. Viongozi wetu, watueleze wanachokiogopa ni nini hasa," alihoji Slaa na kuongeza; "Lakini, viongozi wetu watambue kuwa hata kama Tanzania inaendelea kusifiwa kimataifa, lakini uovu kama huu unaofanyika sasa, unafichwa na matokeo yake walalahoi ambao ni maskini wanaendelea kuteseka ungefichuliwa ungesaidia kulijengea heshima Bunge ambalo ni taasisi inayotakiwa kusimamia serikali," alieleza mbunge huyo.

Aliongeza kuwa inashangaza kuona viongozi wengi walioko madarakani wanapenda kuwasiliana hata na mashirika na wahisani walioko nje, ikiwamo Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa lengo la kujikosha ili waonekane wasafi, kumbe kuna mambo wanaficha ukweli wake.

Bila kuwataja viongozi wahusika, Dk Slaa alidai kuwa viongozi hao wameikosesha nchi kiasi cha Sh2 bilioni kutoka kwa wahisani hao hao tangu mwaka jana kutokana na kutorejeshwa kwa fedha walizokopeshwa na zilizotokana na mfumo wa ununuzi wa madeni.

"Tuna wasiwasi. Tuhuma hizi za wizi na ubadhirifu ni nzito, zinahitaji uchunguzi na kuchukuliwa hatua zikiwamo za kuwasimamisha wahusika, lakini tunashangaa kuona wanakingiwa kifua," alieleza. Aliongeza kuwa wasiwasi wao ni kuwa hicho kinachojaribiwa kufanywa kwa sasa si kizuri, huenda ni kutaka kuuchezea hata huo ushahidi, vielelezo vyote ambavyo vimewasilishwa kwa Spika na huenda ndiyo maana kumekuwapo na ucheleweshaji usio wa msingi.

Mbunge huyo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chadema, alisema baada ya kuondolewa kwa hoja hiyo, upinzani umedhamiria kuchukua hatua kadhaa zikiwamo za kisheria, kuwasiliana na wananchi kwa njia mbalimbali, ukiwamo mkutano wa hadhara ambao utafanyika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam kesho. Hatua nyingine, aliitaja ya kuwaeleza pia wafadhili na wahisani mbalimbali ndani na nje ya nchi wakiwamo Benki ya Dunia na IMF kuhusiana na suala hilo.

Hata hivyo, alisema kuwa rufaa pekee na kubwa itakuwa ile ambayo kwa kutumia umoja wa wapinzani, itakatwa kwa wananchi wote wa Tanzania ambao ndio wamepewa dhamana ya kuwaweka wao madarakani.
Kuhusu madhara yanayoweza kutokea kutokana na kuondolewa kwa hoja hiyo bungeni, Dk Slaa alisema wamejiandaa kukabiliana nayo ikiwa ni pamoja na kukumbana na vitisho kama vile ambavyo wamekuwa wakipata vikiwamo vya kutishiwa maisha.

"Tunajua athari zake, mbona tumekuwa tukipokea SMS kwa kutumia simu na namba binafsi, baadhi zinatishia maisha yetu, nasi tuko tayari kwani hii ni vita ni sawa na askari shupavu anayefia vitani akipigania nchi yake," alisema. "Hatuna tone la hofu, tunapigania haki ya maskini wa Kitanzania walio wanyonge," alisema mbunge huyo na kuongeza kuwa wamekatishwa tamaa, kiasi cha kuamini kuwa hata ikiwasilishwa bungeni hoja hiyo ingezimwa kama nyingine.

Naye Hamad Rashid Mohammed alionya dhidi ya tabia ya viongozi wa Tanzania kutoishi na kuheshimu viapo ambavyo waliapa wakati wakiingia madarakani na kukumbatia maovu. Alisema kutokana na kukosa aibu na utii kwa viapo vyao, ndio maana wamekalia kimya tuhuma za ujenzi wa minara pacha ya BoT ambayo imeiingizia nchi hasara inayofikia dola milioni 600, lakini hakuna kiongozi anayejali au kusumbuliwa na suala hilo.

Aliongeza kuwa hata wakaguzi wa hesabu wamenyimwa taarifa muhimu hivyo kutia mashaka juu ya suala hilo. Alidai kuwa BoT bila ruksa, uhalali wowote imetoa mikopo inayofikia Sh30 bilioni bila dhamana , jambo ambalo alisema wataendelea kulipigia kelele kama ambavyo wanafanya.



HILI LA KUTISHIWA MAISHA- HII NCHI INAELEKEA KUBAYA!
 
..kama watu wameweza ku-pull off hizo deals za mabilioni,sidhani kama watashindwa kuua mtu!

..maanake hapo una-deal na mafioso!
 
Nimepata nafasi ya kuzungumza na Katibu Mkuu wa Chadema na Naibu kiongozi wa upinzani Bungeni Dr. Wilbroad Slaa (Karatu-Chadema) kuhusu suala hili linaloendelea la Zito. Nitawaletea mahojiano hayo Exclusively kupitia KLH News ndani ya saa moja na nusu.
 
1. Tanzania tuna utamaduni wa kujadili kwa hoja na kwa amani sii kutishiana maisha!

2. Naona strategically baada ya yale ya Zitto -CHADEMA waliona wajipange vema na kwa makini zaidi- hence Slaa akaondoa hoja ya BoT.

3. Hivi wandugu CUF sii wapo wengi Bungeni? Mbona sijawaskia? Mbona CHADEMA wamesikika zaidi? Nimemsikia tu Hamad Rashid! Au wamekuwa na mkakati wa kuwa kimya kwanza?
 
1. Tanzania tuna utamaduni wa kujadili kwa hoja na kwa amani sii kutishiana maisha!

2. Naona strategically baada ya yale ya Zitto -CHADEMA waliona wajipange vema na kwa makini zaidi- hence Slaa akaondoa hoja ya BoT.

3. Hivi wandugu CUF sii wapo wengi Bungeni? Mbona sijawaskia? Mbona CHADEMA wamesikika zaidi? Au wamekuwa na mkakati wa kuwa kimya kwanza?


Mei Bi.............
 
Back
Top Bottom