Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Ninasikitika sana kwamba nilisaidia kutoa Virodine kwa wagonjwa Lugalo hospitali na ziliwafanya kuharisha sana among other side effects including deaths. Virodine zinafanana sana na dawa za kienyeji na aliyesimamia hii study ni Dr Balele na ilimlipa sana!!! Hata ilipokuja kuwa kashfa baada ya wizara kukataa kwamba haijatoa kibali hata costech vilevile Balele alihamishiwa Makao Makuu ya Jeshi kuwa Director of Medical Services badala ya kuwa Doctor incharge Lugalo hospital na Director kurudishwa Lugalo!!! Sijui hii ilikuwa demotion au promotion?

Huu mradi wa Virodine baada ya kukataliwa kwa ethical issues aliuchukua General Mboma akijua anaongoza askari wasiojua kitu na akatengeneza pesa sana kwa kushirikiana na Balele! Mungu aturehemu waTz wengi walikufa nawafahamu lakini nani atawasemea??? Jwtz ni chombo kinachoogopwa kama supreme na ndio maana askari wetu hawana wanachojua zaidi ya kuelekeza silaha mbele tu. Bado tunacrem tu!! Ofisa wa Tz hana tofauti na askari wa Kenya tu hapa jirani, tuombe Mungu isizuke vita tu tutamalizana wenyewe kabla ya adui!

Nawakilisha wakuu! yapo mengi jeshini ila nani ana ujasiri wa kusema???

Na huyo Dr. Balele si ndio mkuu wa Mkoa Shinyanga sasa, au sio?
Mbona Tanzania tunaishi kana kwamba ndio tunaingia century ya 19?

Utafiti wa namna hii, sio huko jeshini tu, au hata kwenye magereza kwa wafungwa; hauwezi kuruhusiwa popote pale. Hii ni kukiuka haki za kibinadam. Mwanajeshi ni binaadam kama walivyo wengine, na analindwa na sheria na mikataba ya kimataifa inayokataza mambo kama haya. Hii ni aibu. Na sio kweli kabisa kwamba wahusika hawawezi kufikishwa mbele ya sheria. Ni kukosa tu wasimamizi; kama taasisi zetu zinazotetea haki za binaada. Kama kweli ushahidi upo, sioni tatizo lolote la kupeleka kesi hiyo mahakamani.
 
Na Waandishi Wetu Dar, Dodoma

WAKATI Spika wa Bunge, Samwel Sitta, akiagiza wabunge wa kambi ya upinzani kukatwa posho zao kwa kugomea kushiriki vikao vya Bunge, Kiongozi wa Kambi hiyo, Hamad Rashid Mohamed, amesema agizo hilo ni ukiukwaji wa sheria na Katiba ya nchi.


Hamad ambaye pia ni Mbunge wa Wawi (CUF) na Waziri Mkuu Kivuli, alisema mbali ya kukiuka sheria na Katiba ya nchi, agizo hilo la Spika Sitta, pia ni ukiukwaji wa misingi ya demokrasia na ustaarabu kwa wananchi katika kudai haki zao.


Agizo hilo la Spika ambalo alilitoa bungeni jana baada ya kipindi cha maswali na majibu, litawaumiza zaidi wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), ambao wameondoka kabisa bungeni tangu juzi kurejea Dar es Salaam.


Wabunge wengine vyama vya Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na United Democratic (UDP), ambao jana walirejea bungeni, watakosa posho ya siku ya juzi ambayo ilikuwa ya kwanza kwa mkutano wa 11 wa Bunge.


Wabunge hao walifikia uamuzi huo, wakipinga uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) wa kutaka ifanyike kura ya maoni visiwani Zanzibar ili kupata ridhaa ya wananchi ya ama kuundwa au kutoundwa kwa serikali ya mseto visiwani humo, ni wa vyama vya CUF, Chadema na UDP.


Akizungumza na gazeti hili jana, Hamad, alisema wameshangazwa na agizo hilo la Spika Sitta, kwa kuwa suala la kugoma, ni haki ya msingi ya Kikatiba na kidemokrasia na pia ndio njia pekee ya kistaarabu kwa wananchi katika kudai haki wanazohisi kudhulumiwa.


" Tunashangaa sana kusikia kwamba, kuna kanuni inayowazuia wabunge kugoma," alisema Hamad ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi wa CUF Taifa.


Akifafanua, alisema siku zote vinavyogoma ni vyama, viwe ni vya kisiasa au vya wafanyakazi na kutolea mfano wa mgomo uliofanywa hivi karibuni na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli nchini (TRL) kupitia chama chao (TRAWU).


Alisema kwa kuwa mgomo ni haki ya Kikatiba, kidemokrasia na pia ndio njia pekee ya kistaarabu kwa wananchi kudai haki, serikali haikuwachukulia hatua yoyote wafanyakazi hao, badala yake iliwafuata, ikasikiliza madai yao na kuyashughulikia.


Alisema utaratibu wa kugoma, uliwahi kutumiwa hata na Tanzania ambayo iliwagomea makaburu kwenye Jumuiya ya Madola kupinga vitendo vya ubaguzi wa rangi walivyokuwa wakiwafanyia wazalendo wa Afrika Kusini.


Kutokana na hali hiyo, alisema kwa vile hapa nchini hakujawa na utaratibu wa mgombea binafsi, uamuzi wa wabunge wa kambi ya upinzani kugoma, ni wa haki kwa kuwa ulifanywa na wabunge hao wakiviwakilisha vyama wanavyotoka.


Hata hivyo, alisema huenda wakarejea Bungeni Jumatatu wiki ya ijayo kuendelea na vikao baada ya kujadili suala hilo kwenye chama na kuangalia namna mipango yao ilivyo.


Hamad, alisema jana jioni, wabunge hao walitarajiwa kukutana na Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba makao makuu ya chama hicho, jijini Dar es Salaam kujadili, pamoja na mambo mengine, namna ya kwatakavyofanikisha maandamano ya amani visiwani Zanzibar keshokutwa.


Maandamano hayo yatakayoongozwa na Profesa Lipumba, yanatarajiwa kufanywa na CUF kwa lengo la kuishinikiza CCM isaini rasimu ya makubaliano ya mwafaka wa kisiasa visiwani humo, uliofikiwa kati ya vyama hivyo viwili baada ya kufanya mazungumzo ya kutafuta mwafaka huo kwa miezi 14.


Akitangaza uamuzi huo jana, Spika Sitta, alisema alipata mwongozo wa kisheria na kubaini kwamba, uamuzi huo wa kambi ya upinzani ulikuwa na kasoro.


Spika Sitta alifafanua kwamba, kutokana na kasoro hizo katika maamuzi ya kambi hiyo, Kamati ya Kanuni. itakutana leo kupata taarifa zaidi za kisheria kisha kutoa matangazo ya uamuzi bungeni.


Alisema kasoro hiyo imezingatia ukweli kwamba, suala hilo linahusisha vyama hivyo kuliingiza bungeni haikuwa sahihi.


Sitta aliongeza kwamba, iwapo suala hilo litaachiwa, linaweza kuwa na athari kwani ugomvi baina ya vyama, unaweza kuingizwa bungeni.


Alisema kutokana na wabunge hao kutoka nje ya bunge na kwenda kufanya kazi ambayo si ya bunge, hawastahili kulipwa posho.


?Jana (juzi) kulikuwa na tukio la wabunge wa CUF wakiungwa mkono na wenzao wa upinzani, kutoka nje ya ukumbi wa bunge, jana (juzi) nimetafuta ushauri wa kisheria, nikaibini jambo hili lina kasoro,? alisema Spika na kuongeza:


? Hapa kilichopo ni mazungumzo ya vyama, tukiruhusu ugomvi wa vyama kuingia hapa, basi itakuja kuwa na athari zaidi?.


Spika Sitta aliongeza kwamba leo (jana), wanasheria walikuwa wakiaanda taarifa ya taratibu ambayo itatolewa kwa Kamati ya Kanuni ambayo itakaa leo kisha itatangaza maamuzi bungeni.


Juzi wabunge wote wa upinzani walitoka bungeni, muda mfupi mara baada ya kumalizika wimbo wa taifa, wakionyesha mshikamano wao kupinga hatua ya kusuasa kwa utekelezaji wa mwafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar.


Uamuzi huo unatokana na kiini macho ambacho kimefanywa na Chama cha Mapinduzi (CCM), katika mkutano wake katika kijiji cha Butiama, ambao tamko la NEC-CCM, lilitaka suala hilo la serikali ya mseto lipigiwe kura ya maoni na wananchi wa visiwani humo.


Hata hivyo, tangu kutangazwa kwa uamuzi wa NEC-CCM, hali ya kisiasa (Political Climate) hasa visiwani humo, inaonekana kuchafuka, huku CUF ikitaka Jumuiya Kimataifa kuingilia kati na kutupa lawama hizo kwa Rais Jakaya Kikwete, kwamba anahusika na usanii huo.

Source: Mwananchi
 
Na Waandishi Wetu Dar, Dodoma

WAKATI Spika wa Bunge, Samwel Sitta, akiagiza wabunge wa kambi ya upinzani kukatwa posho zao kwa kugomea kushiriki vikao vya Bunge, Kiongozi wa Kambi hiyo, Hamad Rashid Mohamed, amesema agizo hilo ni ukiukwaji wa sheria na Katiba ya nchi.


Hamad ambaye pia ni Mbunge wa Wawi (CUF) na Waziri Mkuu Kivuli, alisema mbali ya kukiuka sheria na Katiba ya nchi, agizo hilo la Spika Sitta, pia ni ukiukwaji wa misingi ya demokrasia na ustaarabu kwa wananchi katika kudai haki zao.


Agizo hilo la Spika ambalo alilitoa bungeni jana baada ya kipindi cha maswali na majibu, litawaumiza zaidi wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), ambao wameondoka kabisa bungeni tangu juzi kurejea Dar es Salaam.


Wabunge wengine vyama vya Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na United Democratic (UDP), ambao jana walirejea bungeni, watakosa posho ya siku ya juzi ambayo ilikuwa ya kwanza kwa mkutano wa 11 wa Bunge.


Wabunge hao walifikia uamuzi huo, wakipinga uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) wa kutaka ifanyike kura ya maoni visiwani Zanzibar ili kupata ridhaa ya wananchi ya ama kuundwa au kutoundwa kwa serikali ya mseto visiwani humo, ni wa vyama vya CUF, Chadema na UDP.


Akizungumza na gazeti hili jana, Hamad, alisema wameshangazwa na agizo hilo la Spika Sitta, kwa kuwa suala la kugoma, ni haki ya msingi ya Kikatiba na kidemokrasia na pia ndio njia pekee ya kistaarabu kwa wananchi katika kudai haki wanazohisi kudhulumiwa.


" Tunashangaa sana kusikia kwamba, kuna kanuni inayowazuia wabunge kugoma," alisema Hamad ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Uongozi wa CUF Taifa.


Akifafanua, alisema siku zote vinavyogoma ni vyama, viwe ni vya kisiasa au vya wafanyakazi na kutolea mfano wa mgomo uliofanywa hivi karibuni na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli nchini (TRL) kupitia chama chao (TRAWU).


Alisema kwa kuwa mgomo ni haki ya Kikatiba, kidemokrasia na pia ndio njia pekee ya kistaarabu kwa wananchi kudai haki, serikali haikuwachukulia hatua yoyote wafanyakazi hao, badala yake iliwafuata, ikasikiliza madai yao na kuyashughulikia.


Alisema utaratibu wa kugoma, uliwahi kutumiwa hata na Tanzania ambayo iliwagomea makaburu kwenye Jumuiya ya Madola kupinga vitendo vya ubaguzi wa rangi walivyokuwa wakiwafanyia wazalendo wa Afrika Kusini.


Kutokana na hali hiyo, alisema kwa vile hapa nchini hakujawa na utaratibu wa mgombea binafsi, uamuzi wa wabunge wa kambi ya upinzani kugoma, ni wa haki kwa kuwa ulifanywa na wabunge hao wakiviwakilisha vyama wanavyotoka.


Hata hivyo, alisema huenda wakarejea Bungeni Jumatatu wiki ya ijayo kuendelea na vikao baada ya kujadili suala hilo kwenye chama na kuangalia namna mipango yao ilivyo.


Hamad, alisema jana jioni, wabunge hao walitarajiwa kukutana na Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba makao makuu ya chama hicho, jijini Dar es Salaam kujadili, pamoja na mambo mengine, namna ya kwatakavyofanikisha maandamano ya amani visiwani Zanzibar keshokutwa.


Maandamano hayo yatakayoongozwa na Profesa Lipumba, yanatarajiwa kufanywa na CUF kwa lengo la kuishinikiza CCM isaini rasimu ya makubaliano ya mwafaka wa kisiasa visiwani humo, uliofikiwa kati ya vyama hivyo viwili baada ya kufanya mazungumzo ya kutafuta mwafaka huo kwa miezi 14.


Akitangaza uamuzi huo jana, Spika Sitta, alisema alipata mwongozo wa kisheria na kubaini kwamba, uamuzi huo wa kambi ya upinzani ulikuwa na kasoro.


Spika Sitta alifafanua kwamba, kutokana na kasoro hizo katika maamuzi ya kambi hiyo, Kamati ya Kanuni. itakutana leo kupata taarifa zaidi za kisheria kisha kutoa matangazo ya uamuzi bungeni.


Alisema kasoro hiyo imezingatia ukweli kwamba, suala hilo linahusisha vyama hivyo kuliingiza bungeni haikuwa sahihi.


Sitta aliongeza kwamba, iwapo suala hilo litaachiwa, linaweza kuwa na athari kwani ugomvi baina ya vyama, unaweza kuingizwa bungeni.


Alisema kutokana na wabunge hao kutoka nje ya bunge na kwenda kufanya kazi ambayo si ya bunge, hawastahili kulipwa posho.


?Jana (juzi) kulikuwa na tukio la wabunge wa CUF wakiungwa mkono na wenzao wa upinzani, kutoka nje ya ukumbi wa bunge, jana (juzi) nimetafuta ushauri wa kisheria, nikaibini jambo hili lina kasoro,? alisema Spika na kuongeza:


? Hapa kilichopo ni mazungumzo ya vyama, tukiruhusu ugomvi wa vyama kuingia hapa, basi itakuja kuwa na athari zaidi?.


Spika Sitta aliongeza kwamba leo (jana), wanasheria walikuwa wakiaanda taarifa ya taratibu ambayo itatolewa kwa Kamati ya Kanuni ambayo itakaa leo kisha itatangaza maamuzi bungeni.


Juzi wabunge wote wa upinzani walitoka bungeni, muda mfupi mara baada ya kumalizika wimbo wa taifa, wakionyesha mshikamano wao kupinga hatua ya kusuasa kwa utekelezaji wa mwafaka wa kisiasa visiwani Zanzibar.


Uamuzi huo unatokana na kiini macho ambacho kimefanywa na Chama cha Mapinduzi (CCM), katika mkutano wake katika kijiji cha Butiama, ambao tamko la NEC-CCM, lilitaka suala hilo la serikali ya mseto lipigiwe kura ya maoni na wananchi wa visiwani humo.


Hata hivyo, tangu kutangazwa kwa uamuzi wa NEC-CCM, hali ya kisiasa (Political Climate) hasa visiwani humo, inaonekana kuchafuka, huku CUF ikitaka Jumuiya Kimataifa kuingilia kati na kutupa lawama hizo kwa Rais Jakaya Kikwete, kwamba anahusika na usanii huo.

Source: Mwananchi


Kama hili ni kosa kwa hawa jamaa kwa mujibu wa sheria ama kanuni za Bunge na adhabu inaanza mara moja vipi Rostam na wenzake walio dharau tume ya Spika chini ya Mwakyembe wao swala lao sheria na hao wataalam wa sheria wanasemaje ?
 
Kama hili ni kosa kwa hawa jamaa kwa mujibu wa sheria ama kanuni za Bunge na adhabu inaanza mara moja vipi Rostam na wenzake walio dharau tume ya Spika chini ya Mwakyembe wao swala lao sheria na hao wataalam wa sheria wanasemaje ?


Rostam ndio taikun kwenye CCM Vipi ndugu yangu yaani hujui kama Rostam ndio CCM na ndio financer wa mtandao? yaani Mr Six mwenyewe anamtambua RA kama bossi wao iweje wamuadhibu?

Rules:
1.Always the boss is right
2.If the boss is wrong check rule number one!

Unalo?
 
Rostam ndio taikun kwenye CCM Vipi ndugu yangu yaani hujui kama Rostam ndio CCM na ndio financer wa mtandao? yaani Mr Six mwenyewe anamtambua RA kama bossi wao iweje wamuadhibu?

Rules:
1.Always the boss is right
2.If the boss is wrong check rule number one!

Unalo?

Loud and Clear!!
 
Naamini kuwa hatuwezi kuwa na demokrasi kamili wakati tunawachagulia watu namna ya kuonyesha kutoridhishwa kwao na maamuzi ya sehemu nyingine ya jamii, utawala n.k. Ni sheria moja tu inayobidi kutawala nayo ni kuwa wafanye hivyo kwa amani. Kususia kikao ni njia mojawapo.
 
MAJINA ya viongozi waandamizi wa serikali ya awamu ya tatu wanaohusishwa na mikataba mibovu, ambayo yameanza kutajwa waziwazi bungeni yameongezeka baada ya jana, aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba, naye kuingizwa katika orodha hiyo.

Mramba alitajwa na Godfrey Zambi (Mbozi Mashariki-CCM), wakati alipokuwa akiwasilisha hoja binafsi kulitaka Bunge liiagize serikali isitishe nyongeza ya pili ya mkataba wa Kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services (TICTS), inayofanya kazi ya upakuaji na upakiaji wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam.

Katika hoja hiyo, Zambi alisema kuwa Mramba ndiye aliyeandika barua yenye kumbukumbu Na. TYC/R/160/32 ya Septemba 6, 2005, akimtaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuhakikisha kuwa mkataba wa TICTS unaongezwa.

Zambi alisema kuwa barua hiyo, pamoja na mambo mengine kuhusu utendaji wa kampuni hiyo, vinaonyesha kuwa mkataba huo uliongezwa kwa manufaa ya watu binafsi.

Akiwasilisha hoja binafsi bungeni jana, mbunge huyo alisema kutokana utendaji usioridhisha wa Kampuni ya TICTS, ni vema serikali ikaifuta nyongeza ya pili ya mkataba wa miaka 15, uliosainiwa mwaka 2005.

Alisema mbali na kutoridhisha kiutendaji kwa kampuni hiyo, pia kusainiwa kwa mkataba huo mpya kumekiuka baadhi ya vipengele vilivyopo katika mkataba wa awali, ulioitaka serikali kutoongeza muda wa mkataba huo mpaka muda wa awali utakapoisha, isipokuwa kama kutakuwa na ulazima kwa manufaa ya taifa.

Zambi alisema kuwa hivi karibu Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipowasilisha taarifa yake ya ukaguzi, alibainisha kuwa amebaini kuwepo kwa ukiukwaji wa Sheria ya Manunuzi ya Umma katika kusaini mkataba huo.

Zambi alisema Kampuni ya TICTS haijawahi kufikisha malengo ya utendaji kazi yaliyopo kwenye mkataba wa awali, hivyo ana wasiwasi na mazingira yaliyotumika kuiongezea kampuni hiyo mkataba kabla ya kuisha kwa muda wa awali.

Alisema katika Bandari ya Dar es Salaam makontena yamekuwa yakirundikana na kukaa kwa muda mrefu, ambapo gharama za kukaa bandarini hapo hulipiwa na mwenye kontena, hali inayokimbiza wafanyabiashara na kuikosesha serikali mapato.

Alibainisha kuwa kampuni hiyo imeshindwa kununua vifaa vya kufanyia kazi ambapo wakati inasaini mkataba ilikodisha eneo kuwa la ardhi na vifaa, lakini yenyewe haikuwa na kifaa chochote na iliahidi kununua vifaa kidogo kidogo, jambo ambalo halijatekelezwa.

Mbunge huyo aliongeza kuwa, kiwango cha uwekezaji cha kampuni hiyo ni kidogo ikilinganishwa na mkataba, ambapo TICTS ilitakiwa iwe imewekeza jumla ya dola za Marekani milioni 10.389 hadi mwaka 2008, ambapo ipo tofauti ya dola za Marekani takribani milioni 4 na hali iliyopo sasa.

Alisema hali hiyo haionyeshi kama kweli TICTS ina dhamira ya kweli katika uwekezaji kwenye swala la vifaa, ambapo pia alibainisha kudanganywa kwa Kamati ya Bunge ilipotembelea kampuni hiyo, ili kuona kazi zake.

“Tarehe 23/1/2008 TICTS iliieleza Kamati ya Miundombinu kwamba imewekeza dola milioni 6 kwenye ununuzi wa vifaa, na tarehe 15/4/2008 ilisema imewekeza dola milioni 15 kwenye ununuzi wa vifaa, dhahiri huo ni uongo unaolenga kuipotosha kamati,” alisema Zambi.

Alisema haiwezekani ndani ya miezi mitatu wakawa wamenunua vifaa vya dola milioni 9, suala ambalo wameshindwa kulifanya kwa miaka saba, ambapo katika taarifa ya TICTS kwa kamati ilionyesha kuwa hiyo ni kampuni kubwa inayofanya kazi maeneo mbalimbali.

Alielezea kushangazwa kwake katika hoja hiyo binafsi kuwa haiwezekani kwa kampuni kubwa kama hiyo ishindwe kuwekeza katika ununuzi wa vifaa na hivyo kuendelea kutumia vifaa ilivyovikuta, ambavyo kwa sasa vingine ni chakavu na havifanyi kazi kwa ufanisi unaotakiwa.

Alisema kwa mujibu wa mikataba, kitengo hicho kilipaswa kulipa kodi pamoja na mrahaba kwani kimekuwa kikipata faida kubwa sana tangu kianzishwe, lakini kiasi cha fedha kinachowekezwa ni kidogo sana.

Zambi alisema pia mkataba huo hauruhusu mwekezaji mwingine kufanya biashara ya aina hiyo mpaka pale TICTS itakapokuwa imefikisha kuhudumia kontena 650,000 wakati sasa inahudumia kontena zipatazo 343,130.

“Kipengele hicho ni cha ajabu sana maana wanaweza kuamua kuhudumia chini ya viwango, ili wawe peke yao, na hatuwezi kuongeza wawekezaji wengine wakati mkataba hauruhusu hali hiyo,” alisema.

Alisema ili kuonyesha kwamba kigezo cha ufanisi kwa kampuni hiyo kimeshuka na muda wa meli kusubiri kuingia bandarini umeongezeka, alisema kuwa wastani wa muda wa mzunguko wa meli umeongezeka na wastani wa kontena zinazotakiwa kuwa ndani ya kitengo umezidi na kuwa TEUs 9,000 wakati uwezo wa kitengo ni TEUs 6,500.

Alisema bandarini hapo hivi sasa upo msongamano wa meli zinazosubiri kuingia ambapo hali hiyo imesababishwa na utendaji usioridhisha wa TICTS ambayo tena imeongezewa muda wa miaka 15 ya mkataba wake.

Alibainisha kuwa ili kuondoa kasoro zote zilizopo kwenye mkataba wa TICTS na kuiwezesha serikali kuongeza mapato yake, inapaswa kusitisha nyongeza ya mkataba na kufanya mapitio ya mkataba wa awali, ili vifungu vya makataba huo visivyo na manufaa kwa nchi virekebishwe.

Source: Gazeti Tanzania Daima
 
Zambi ni mbunge wa kwanza kufanya upembuzi wa wanayotokea hivi sasa. Asilimia kubwa inaflow na media...
 
madhambi yao yamefikia mahali ambapo hayawezekani kufichika tena! Naye Mramba sijui ameficha vijisent vingapi nje!!!
 
madhambi yao yamefikia mahali ambapo hayawezekani kufichika tena! Naye Mramba sijui ameficha vijisent vingapi nje!!!

Tungelikuwa na Serikali inayowasikiliza wananchi tayari tungelikuwa MATAJIRI gafla. Nina uhakika bajeti ijayo tusingeomba misaada ya wahisani. Tukichukua pesa za hawa mabwana wakubwa waliojiwekea kipengele cha TAKRIMA kwenye katiba hili waweze kufanikisha UFISADI tunaweza kufika mbali.

TUnatakiwa kuiomba serikali ipate taharifa za kila kiongozi aliyeko madarakani na ambaye ametoka madarakani ana kiasi gani na amezipataje. Hii nafikiri ikiwa kamati ya bunge itatufaa sana.
 
kusema ukweli mungu anaataka tanzania yribadilikendio maana mnaona mambo ambayoyamekuwa kikwazokwa maendeleo yetu yanaanza kuwekwa wazi
 
MAJINA ya viongozi waandamizi wa serikali ya awamu ya tatu wanaohusishwa na mikataba mibovu, ambayo yameanza kutajwa waziwazi bungeni yameongezeka baada ya jana, aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba, naye kuingizwa katika orodha hiyo.
Mramba alitajwa na Godfrey Zambi (Mbozi Mashariki-CCM), wakati alipokuwa akiwasilisha hoja binafsi kulitaka Bunge liiagize serikali isitishe nyongeza ya pili ya mkataba wa Kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services (TICTS), inayofanya kazi ya upakuaji na upakiaji wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam.

Katika hoja hiyo, Zambi alisema kuwa Mramba ndiye aliyeandika barua yenye kumbukumbu Na. TYC/R/160/32 ya Septemba 6, 2005, akimtaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuhakikisha kuwa mkataba wa TICTS unaongezwa.

Zambi alisema kuwa barua hiyo, pamoja na mambo mengine kuhusu utendaji wa kampuni hiyo, vinaonyesha kuwa mkataba huo uliongezwa kwa manufaa ya watu binafsi.

Akiwasilisha hoja binafsi bungeni jana, mbunge huyo alisema kutokana utendaji usioridhisha wa Kampuni ya TICTS, ni vema serikali ikaifuta nyongeza ya pili ya mkataba wa miaka 15, uliosainiwa mwaka 2005.

Alisema mbali na kutoridhisha kiutendaji kwa kampuni hiyo, pia kusainiwa kwa mkataba huo mpya kumekiuka baadhi ya vipengele vilivyopo katika mkataba wa awali, ulioitaka serikali kutoongeza muda wa mkataba huo mpaka muda wa awali utakapoisha, isipokuwa kama kutakuwa na ulazima kwa manufaa ya taifa.

Zambi alisema kuwa hivi karibu Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipowasilisha taarifa yake ya ukaguzi, alibainisha kuwa amebaini kuwepo kwa ukiukwaji wa Sheria ya Manunuzi ya Umma katika kusaini mkataba huo.

Zambi alisema Kampuni ya TICTS haijawahi kufikisha malengo ya utendaji kazi yaliyopo kwenye mkataba wa awali, hivyo ana wasiwasi na mazingira yaliyotumika kuiongezea kampuni hiyo mkataba kabla ya kuisha kwa muda wa awali.

Alisema katika Bandari ya Dar es Salaam makontena yamekuwa yakirundikana na kukaa kwa muda mrefu, ambapo gharama za kukaa bandarini hapo hulipiwa na mwenye kontena, hali inayokimbiza wafanyabiashara na kuikosesha serikali mapato.

Alibainisha kuwa kampuni hiyo imeshindwa kununua vifaa vya kufanyia kazi ambapo wakati inasaini mkataba ilikodisha eneo kuwa la ardhi na vifaa, lakini yenyewe haikuwa na kifaa chochote na iliahidi kununua vifaa kidogo kidogo, jambo ambalo halijatekelezwa.

Mbunge huyo aliongeza kuwa, kiwango cha uwekezaji cha kampuni hiyo ni kidogo ikilinganishwa na mkataba, ambapo TICTS ilitakiwa iwe imewekeza jumla ya dola za Marekani milioni 10.389 hadi mwaka 2008, ambapo ipo tofauti ya dola za Marekani takribani milioni 4 na hali iliyopo sasa.

Alisema hali hiyo haionyeshi kama kweli TICTS ina dhamira ya kweli katika uwekezaji kwenye swala la vifaa, ambapo pia alibainisha kudanganywa kwa Kamati ya Bunge ilipotembelea kampuni hiyo, ili kuona kazi zake.

“Tarehe 23/1/2008 TICTS iliieleza Kamati ya Miundombinu kwamba imewekeza dola milioni 6 kwenye ununuzi wa vifaa, na tarehe 15/4/2008 ilisema imewekeza dola milioni 15 kwenye ununuzi wa vifaa, dhahiri huo ni uongo unaolenga kuipotosha kamati,” alisema Zambi.

Alisema haiwezekani ndani ya miezi mitatu wakawa wamenunua vifaa vya dola milioni 9, suala ambalo wameshindwa kulifanya kwa miaka saba, ambapo katika taarifa ya TICTS kwa kamati ilionyesha kuwa hiyo ni kampuni kubwa inayofanya kazi maeneo mbalimbali.

Alielezea kushangazwa kwake katika hoja hiyo binafsi kuwa haiwezekani kwa kampuni kubwa kama hiyo ishindwe kuwekeza katika ununuzi wa vifaa na hivyo kuendelea kutumia vifaa ilivyovikuta, ambavyo kwa sasa vingine ni chakavu na havifanyi kazi kwa ufanisi unaotakiwa.

Alisema kwa mujibu wa mikataba, kitengo hicho kilipaswa kulipa kodi pamoja na mrahaba kwani kimekuwa kikipata faida kubwa sana tangu kianzishwe, lakini kiasi cha fedha kinachowekezwa ni kidogo sana.

Zambi alisema pia mkataba huo hauruhusu mwekezaji mwingine kufanya biashara ya aina hiyo mpaka pale TICTS itakapokuwa imefikisha kuhudumia kontena 650,000 wakati sasa inahudumia kontena zipatazo 343,130.

“Kipengele hicho ni cha ajabu sana maana wanaweza kuamua kuhudumia chini ya viwango, ili wawe peke yao, na hatuwezi kuongeza wawekezaji wengine wakati mkataba hauruhusu hali hiyo,” alisema.

Alisema ili kuonyesha kwamba kigezo cha ufanisi kwa kampuni hiyo kimeshuka na muda wa meli kusubiri kuingia bandarini umeongezeka, alisema kuwa wastani wa muda wa mzunguko wa meli umeongezeka na wastani wa kontena zinazotakiwa kuwa ndani ya kitengo umezidi na kuwa TEUs 9,000 wakati uwezo wa kitengo ni TEUs 6,500.

Alisema bandarini hapo hivi sasa upo msongamano wa meli zinazosubiri kuingia ambapo hali hiyo imesababishwa na utendaji usioridhisha wa TICTS ambayo tena imeongezewa muda wa miaka 15 ya mkataba wake.

Alibainisha kuwa ili kuondoa kasoro zote zilizopo kwenye mkataba wa TICTS na kuiwezesha serikali kuongeza mapato yake, inapaswa kusitisha nyongeza ya mkataba na kufanya mapitio ya mkataba wa awali, ili vifungu vya makataba huo visivyo na manufaa kwa nchi virekebishwe.

Source: Gazeti Tanzania Daima

Mramba ndiye Kingpin wa ufisadi wote wa enzi za Mkapa. Ningewashauri waBunge wasitishe mkataba wa TICTS na kuanza upya badala ya kuendelea kushona viraka.
 
Mramba ndiye Kingpin wa ufisadi wote wa enzi za Mkapa.

Sasa ukimuhoji vizuri Mramba, ndio utamkuta yule jamaa ya mkapa Mushi, kwa sababu ndiye aliyekuwa akitumiwa kumpa message za ufisadi,

ukimkamata makapa lazima pia na huyu mramba achukuliwe, wote lao moja, yaani siku ya kuwakamata lazima uwachukue wote siku hiyo hiyo makapa, mramba, rostam, mushi, ruhinda, yona, kigoda, idd simba, masilingi, kazaura, mary kejo, mahalu, chenge, mahita, mstaafu wa idara, kesi yao ikisikilizwa na kuisha mahakamani, basi ndio utakuwa mwanzo na mwwisho wa maneno ya ufisadi bongo! Hawa ndio the head wa ufisadi, wengine walidandia tu treni wasioijua inakwenda wapi wala inakotoka!

Mungu Aibariki Tanzania!
 
Sasa ukimuhoji vizuri Mramba, ndio utamkuta yule jamaa ya mkapa Mushi, kwa sababu ndiye aliyekuwa akitumiwa kumpa message za ufisadi,

Ukimkamata Mkapa lazima pia na huyu mramba achukuliwe, wote lao moja, yaani siku ya kuwakamata lazima uwachukue wote siku hiyo hiyo makapa, mramba, rostam, mushi, ruhinda, yona, kigoda, idd simba, masilingi, kazaura, mary kejo, mahalu, chenge, mahita, mstaafu wa idara, kesi yao ikisikilizwa na kusha mahakamani, basi ndioutakuwa mwanzo na mwwisho wa maneno ya ufisadi bongo!

Mungu Aibariki Tanzania!

Ukiwasweka ndani hao pesa ya walipa kodi itapumua kidogo na maisha bora kidogo tutaanza kuona mwanga Hebu wachukuliwe haraka hawa!
 
Ni saa baba h umewataja hao woote wengine sijapata kuwasikia lakini mbona umesahau kuwataja magwiji wa ufisadi Mhe LOWASA na Mhe SUMAYE hawa ndiyo vigogo wa ufisadi mungu awalaani
 
Kusafisha Safu Nzimka Inahitaji Moyo Wa Uzalendo Na Ujasiri Kama Wa Sokoine .................sidhani Kama Jk Mcheka Cheka Anayaweza Haya....huyu Alitakiwa Awe Pr Wa Rais Na Si Raisi Mwenyewe...hajui Analolifanya.....
 
lakini mbona umesahau kuwataja magwiji wa ufisadi Mhe LOWASA na Mhe SUMAYE hawa ndiyo vigogo wa ufisadi mungu awalaani

Mkuu hawa walikuwa wadandiaji tu, wale kule ndio the originals, Lowassa na kuchota kote kwa zamani hajafikia hawa jamaa bro,

mkuu sister wangu ni jirani na kigoda, nimeiona ile nyumba ya serikali ikiwa ya kawaida wakati anahamia, nenda sasa hutaamini kuwa ni ile ile, na sasa ni yake sio ya serikali tena na ameiongeza kwa juu, na ile Range anayoendesha ambayo ni mpya huiwezi itoa dukani bila Dola za US elfu sabini yaani $ 70,000 yaani exactly sawa na ile ya mkapa je ni kweli walinunua pamoja, au walipewa bure? Kama walinunua hela walitoa wapi? Kama walipewa, walipewa na nani? Kwa sababu gani? Mbona mawaziri wengine hawakupewa?

Yaaani huyu Kigoda ana jeuri ya pesa kwamba hata pale bungeni yeye huiegesha hii gari mahali pa wakubwa wa taifa, na hakuna wa kumuuliza wakati wabunge wote wengine huegesha magari yao sehemu ya wabunge tu!
 
Mkapa humwambii kitu juu ya Mramba. siku zote mtu aliekulia mkeo huwa adui lakini kwa Mkapa sivyo amekuwa Best friend wake.labda anamshukuru kwa kumuachia ANNA Mkapa.
 
Mramba hawawezi kumgusa kwani anajua siri nyingi. Ukimshambulia huyu ni kama unamshambulia Mstaafu mwenyewe. Hapa lazima spin iwepo ili soo limuangukie mwingine la sivyo Mramba akiamua kumwaga manyanga hapatakalika...

tip of the iceberg:

"Mramba ndiye aliyeandika barua yenye kumbukumbu Na. TYC/R/160/32 ya Septemba 6, 2005, akimtaka Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuhakikisha kuwa mkataba wa TICTS unaongezwa."

Kwa makusudi kabisa wanaruka kuandika kile Mramba alichoandika. Mramba aliandika "Nimeagizwa na rais..."
 
Back
Top Bottom