Kutoka Afghanistan, hadi Lithuania, ni nchi gani zinazopenda kuendelea kutumiwa na Marekani kama ni karata ya kutupwa baadaye?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,033
VCG31N1234325178.jpg


Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na mwendelezo wa mivutano kati ya China na Marekani ambayo imeripotiwa mara kwa mara na vyombo vya habari. Marekani imekuwa ikitumia
ujanja wa kutumia upande wa tatu kujaribu kuiyumbisha China au kuingilia mambo ya ndani ya China, na China imekuwa ikifichua hali hiyo na kuitambua jumuiya ya kimataifa.

Kwa muda mrefu karata ambayo imekuwa inachezwa na Marekani kujaribu kuingilia mambo ya ndani ya China na kuiyumbisha China ni maswala ya “demokrasia” na “haki za binadamu”. Bahati mbaya ni kuwa karata hiyo inazidi kugonga mwamba kila kukicha, kwani kadiri siku zinavyozidi kusonga mbele, ndivyo jumuiya ya kimataifa inazidi kutambua unafiki wa Marekani kwenye maswala hayo, kwani nchini Marekani kwenyewe demokrasia inaonekana kuwa ni haki ya kundi fulani la watu, na kumekuwa na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, unaonesha kuwa hata haki ya msingi kama ya kuishi, ni kwa ajili ya baadhi ya watu.

Baada ya kuona kuwa inazidi kukosa sifa ya kujiita kinara wa demokrasia na haki za binadamu, sasa Marekani imepanua matumizi ya diplomasia kama njia ya kuiyumbisha China. Ni hivi karibuni tu Marekani imefanya utungaji wa sheria wa ujanja ujanja, ikilenga kutafuta nafasi ya ushiriki wa Taiwan ambayo ni sehemu ya China kwenye mkutano wa Shirika la Afya Duniani WHO. Hatua hiyo ni kinyume na makubaliano yaliyosainiwa kati ya China na Marekani, ambayo Marekani imeahidi kuheshimu mamlaka ya China na kutambua uwepo wa China moja. Ni wazi kuwa hatua hii ni sehemu ya uingiliaji wa Marekani kwenye mambo ya China.

Hatua hii imekuja siku chache baada ya Rais Joe Biden kusema hivi mwishoni mwa mwaka huu ataitisha mkutano wa nchi za “kidemokrasia”, na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Anthony Blinken, kusema ataialika Taiwan kushiriki kwenye mkutano huo. Na kabla ya hapo kulikuwa na kauli nyingi za Marekani kuhusu ushirikiano wa kijeshi na Taiwan.

Ujanja huu pia umeonekana nchini Lithuania, ambapo katika hali isiyoeleweka nchi hiyo imeamua kukaribisha kufunguliwa kwa “ofisi ya uwakilishi wa Taiwan”, na mara moja msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Bw. Ned Price alisema Marekani inaunga mkono washirika wake kuanzisha uhusiano na Taiwan.

Dunia nzima, ikiwa ni pamoja na Marekani, inatambua kuwa Taiwan ni sehemu ya China, na hali ya sasa kati ya pande hizo mbili za mlango bahari ni matokeo ya mgogoro wa zamani wa ndani. Ukweli huu unatambuliwa kisheria na nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa. Lakini pia suala hili limekuwa ni uchochoro unaotumiwa na Marekani kujipenyeza kuingia mambo ya ndani ya China, kwa kutumia upande wa tatu.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Marekani si nchi ya kuaminika inapokuja kwenye uhusiano wa kimataifa, hata iwe ni kwenye sheria za kimataifa. Kuna mifano mingi tu inayoonyesha kuwa Marekani inazitumia nchi nyingine kufanikisha malengo yake ya kiuchumi, kiusalama na kisiasa, na baada ya kufikia malengo yake inazitelekeza nchi hizo na kuziacha ziingie kwenye taabu ya muda mrefu.

Ikumbukwe kuwa Marekani iliingia Afghanistan kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi na kuleta usalama. Serikali ya wakati ule ya Afghanistan (2001) iliiamini serikali ya Marekani, lakini baada ya miaka ishirini ya mauaji na uharibifu mkubwa wa vita, Marekani imeitelekeza Afghanistan ambayo sasa imeambiwa inatakiwa kushughulikia matatizo yake yenyewe. Hali hii pia imetokea Iraq, Somalia na sehemu nyingine nyingi duniani, ambako baada ya Marekani kutimiza malengo yake inaondoka na kuzitelekeza nchi hizo.

Kwa nchi ambazo kwa makusudi zimeamua kupuuza sheria za kimataifa na kanuni za kidemokrasia za kimataifa ili kuifurahisha Marekani, zina mifano mingi ya kujifunza. Hatimaye baada ya kutumiwa na Marekani zitaishia kutupwa na kuachwa kwenye taabu za muda mrefu.
 
Kuangalia maslahi yenu kwanza ndo nchi zote wanafanya labda kasoro sisi
 
Kuna ile ya kujiuzuru kwa sababu ya kuunga mkono juhudi, deep down unajua kipi ni kipi. Asante sana kwa dondoo
 
Back
Top Bottom