Kutojiuluzulu kwa Chenge na kutoomba radhi kwa Karamagi kunawaletea aibu kubwa

Azarel

JF-Expert Member
Aug 25, 2016
26,054
33,915
Habarini Wadau,

Hapo jana kulikuwa na uwasilishwaji wa ripoti ya pili ya WIZI wa mali ya Umma. Hili limeumiza wengi sana hususan watanzania masikini na wenye shida mbalimbali wakati nchi yao imejaa rasilimali. Wengi waliisikiliza ripoti ile.

Lakini, binafsi nikikumbuka yale maneno makali yaliyojaa hasira yaliyotolewa na Mh. Rais Magufuli, inanifanya nijiulize je Andrew Chenge (aliyekuwa mwanasheria mkuu wa muda mrefu zaidi kutoka Harvad University) ana ujasiri gani wa kuendelea kukaa katika madaraka?

Nazir Karamagi hata akihojiwa atajitetea nini mbele ya watanzania kwa wizi na utumiaji wa mali zao?

Ni kwanini Mkuu wa nchi alitoa fursa ya wao kuhojiwa badala ya kushitakiwa moja kwa moja?

Hawa wahujumu uchumi na Mafisadi wa mali za watanzania masikini ni kwanini wanapata viburi na ujasiri wa kuendelea kuenjoy uongozi na maisha hapa nchini?

Je Mh. Rais atawachukulia hatua kali kweli hawa?

Nawasilisha.
 
Huyu hana kosa alikua anatekeleza ilani ya chama mana hakuna msafi ndani ya chama...anaetakiwa kuomba radhi watz ni chama chakavu kwa kutuibia miaka yote hku wao na familia zao wakielea kwenye utajiri wa ajabu....jana boss wao alitakiwa kuomba radhi watz ndio wangemuelewa sio kuja na mikwara watu washulikiwe bungeni n nje ya bunge.

Hakuna msafi lumumba hata kingunge aliwahi kusema wote ni ukoo wa panya
 
Huyu hana kosa alikua anatekeleza ilani ya chama mana hakuna msafi ndani ya chama...anaetakiwa kuomba radhi watz ni chama chakavu kwa kutuibia miaka yote hku wao na familia zao wakielea kwenye utajiri wa ajabu....jana boss wao alitakiwa kuomba radhi watz ndio wangemuelewa sio kuja na mikwara watu washulikiwe bungeni n nje ya bunge.
Hakuna msafi lumumba hata kingunge aliwahi kusema wote ni ukoo wa panya
Acha kumficha chenge kwenye kivuli CHA chama huyo ni fisadi na si mzalendo alitumia uelewa wake kisheria kuihadaa Serikali kwa anacho kifanya hakuna ilani ya chama chochote duniani inayotaka rushwa .
 
Acha kumficha chenge kwenye kivuli CHA chama huyo ni fisadi na si mzalendo alitumia uelewa wake kisheria kuihadaa Serikali kwa anacho kifanya hakuna ilani ya chama chochote duniani inayotaka rushwa .
Chenge aliwalazmishwa kupitisha hiyo mikataba,hakuna aliesafi na hakula mwenywe hiyo pesa lazma kuna msururu wa mawaziri na makada wa ccm
 
mkuu, ukimzungumzia Andrew Chenge huwezi kuwaacha marais wastaafu wa awamu za tatu na nne.

aliyoyafanya wakati ule yalikuwa na baraka zote za baraza la mawaziri na wakuu wa nchi wa awamu hizo na ndio maana ameendelea kupeta.

na ukizingatia rais JPM alisema hatafukua makaburi unatarajia nini hapo?
 
Kumbuka aliaminiwa na Serikali pia alikaa muda mrefu sana kama mwanasheria mkuu na kama mshauli wa maswala yote ya kisheria serikalini. Yeye ndo anabeba mzigo wote sisi wa tz hatutaki kujua alikula na nani labda awataje yeye sisi tunambana tuliempa dhamana.
 
mkuu, ukimzungumzia Andrew Chenge huwezi kuwaacha marais wastaafu wa awamu za tatu na nne.
aliyoyafanya wakati ule yalikuwa na baraka zote za baraza la mawaziri na wakuu wa nchi wa awamu hizo na ndio maana ameendelea kupeta.
na ukizingatia rais JPM alisema hatafukua makaburi unatarajia nini hapo?
Yeye ndo wakulaumiwa mkapa mwinyi na kikwete hawajui sheria ndo mana wanakua na washauri wakisheria.
 
Chenge aliwalazmishwa kupitisha hiyo mikataba,hakuna aliesafi na hakula mwenywe hiyo pesa lazma kuna msururu wa mawaziri na makada wa ccm
Hivi nakupa mfano :ktk familia yako unawatoto wengi umewapeleka shule mmjoja akapata mimba je tukulaumu wewe mzazi kwa kumfundisha ngono mwanao? Jibu ni hapana mzazi una pray part yako na mtoto pia
 
Acha kumficha chenge kwenye kivuli CHA chama huyo ni fisadi na si mzalendo alitumia uelewa wake kisheria kuihadaa Serikali kwa anacho kifanya hakuna ilani ya chama chochote duniani inayotaka rushwa .
Hebu nitajie mtu kwenye hicho chama ambae hajawahi kupiga pesa za umma/ubadhirifu wa aina yoyote ile?
 
Hebu nitajie mtu kwenye hicho chama ambae hajawahi kupiga pesa za umma/ubadhirifu wa aina yoyote ile?
Ndio wapo wengi tu na kila Mtu atahukumiwa kwa alilofanya chama hakihusiki mahakamani .wameliibia taifa sio chama wote tunakosa huruma Muhimu
 
Habarini Wadau,

Hapo jana kulikuwa na uwasilishwaji wa ripoti ya pili ya WIZI wa mali ya Umma. Hili limeumiza wengi sana hususan watanzania masikini na wenye shida mbalimbali wakati nchi yao imejaa rasilimali. Wengi waliisikiliza ripoti ile.

Lakini, binafsi nikikumbuka yale maneno makali yaliyojaa hasira yaliyotolewa na Mh. Rais Magufuli, inanifanya nijiulize je Andrew Chenge (aliyekuwa mwanasheria mkuu wa muda mrefu zaidi kutoka Harvad University) ana ujasiri gani wa kuendelea kukaa katika madaraka?

Nazir Karamagi hata akihojiwa atajitetea nini mbele ya watanzania kwa wizi na utumiaji wa mali zao?

Ni kwanini Mkuu wa nchi alitoa fursa ya wao kuhojiwa badala ya kushitakiwa moja kwa moja?

Hawa wahujumu uchumi na Mafisadi wa mali za watanzania masikini ni kwanini wanapata viburi na ujasiri wa kuendelea kuenjoy uongozi na maisha hapa nchini?

Je Mh. Rais atawachukulia hatua kali kweli hawa?

Nawasilisha.

Kama pesa zilitumika kwenye chaguzi ili Chama Kishinde unadhani Chenge ataguswa?
 
Chenge na kalamagi walitekeleza maazimio ya baraza la mawaziri, hawakua wanajiamlia wao wenyewe.

Mbona Nyumba za serikali ziligawiwa kwa watu bure kabisa na tukaambiwa ilikua maamuzi ya serikali na sio ya waziri kujiamlia, sasa iweje kwa kina chenge na kalamagi??
 
Acha kumficha chenge kwenye kivuli CHA chama huyo ni fisadi na si mzalendo alitumia uelewa wake kisheria kuihadaa Serikali kwa anacho kifanya hakuna ilani ya chama chochote duniani inayotaka rushwa .
Mnataka kumuonea change bureee....kama kawaida yenu mnatafuta mbuzi wa kafara...wabunge wa CCM akiwemo JPM mwenyewe walioipigia kura za ndio hiyo mikataba bungeni mbona wenyewe hujawataka wajiuzuru
 
Chenge na kalamagi walitekeleza maazimio ya baraza la mawaziri, hawakua wanajiamlia wao wenyewe.

Mbona Nyumba za serikali ziligawiwa kwa watu bure kabisa na tukaambiwa ilikua maamuzi ya serikali na sio ya waziri kujiamlia, sasa iweje kwa kina chenge na kalamagi??
Naomba elewa kitu KIMOJA masula yoote ya kisheria nchini yanaamuliwa na mwanasheria mkuu hata baraza LA mawazili linapitisha jambo kwa kuzingatia maoni ya mwanasheria mkuu ktk maswala ya kimikataba.
 
Mie nashindwa kuelewa hivi ni nani alituloga???Miaka yote sisi ndio tupo madarakani na madudu yote hayo yamefanyika chini yetu na watu waliotajwa ni sehemu tu ya wale waliowahi tajwa ktk ufisadi mwingibe lakini bado haitoshi.!??WAOMBE RADHI ILI IWEJE??
 
Back
Top Bottom