Kutofautiana na mtu mnayempenda nyie sio kosa la kijinai

Nanye Go

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
8,386
10,843
Dudu baya anatofauti na Marehemu Ruge Mutahaba, lakini serikali na wana ccm wameufanya ni msiba wa chama chao na serikali hiyohiyo ya ccm nayo imeufanya msiba ni wao.
Marehemu alikuwa b binadamu na alikosea na aliwakosea baadhi ya watu, na,watu hao wanayo haki kutokumpenda. Kama mlivyompenda ninyi wapo waliomchukia na wanamchukia hadi kesho.
Yani mkipendacho nyie mnataka kila mtu akipende?! Eti kwasababu rais alitweet masikitiko basi woote tufuate nyayo zake?! Mimi sidhani kama nisahihi. Rais abaki na maoni yake nasisi wananchi tuachwe na maoni yetu hata kama hamuyapendi?
Nakumbuka Lady JD pia amewahi kushitakiana na Ruge au clouds akikataa nyimbo zake kupigwa na stesheni hiyo bure. Ladyjd aliwahi kusema cliuds waimbe nyimbo zao waache kutumia wasanii na sanaa zao kujinufaisha.
Leo Dudubaya analaumiwa mlitaka naye asifu?! Sasa mlitaka akae kimya?! Wapo waliokaa kimya lakini haimaanishi wanampenda mnayempenda. Tujifunze kuvumiliana., Dudubaya ASAMEHEWE. Mmesha muhukumu kwa kumsema ni mjinga, kachanganyikiwa sasa mnashindwa nini kumsamehe?!
Povu lina ruhusiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dudu baya Moja ya Lawama zake Ni kudhulumiwa Na Ruge Na Clouds

Lakin hapo hapo analaumu Clouds kumpotezea
Sasa Kwanini ulaumu anaekudhulumu akiamua kufanya nawe Biashara ya kukudhulumu?

Dudu baya anatuambia Kila Mara Kuwa Clouds wamemshusha kimziki Ila anajizuia kutuambia nani alimpaisha Ki muziki

Ujinga ni kutaka usaidiwe ki lazima

Hapo hapo analalamika kudhulumiwa Halafu analalamika hawakuwa Na Mkataba ( Makubaliano), sasa Kama ulikubali kufanya Kazi Na Mtu bila ya makubaliano hoja ya kusema kakudhulumu inatokea wapi?

Ruge kaondoka, tunatega masikio Na macho kushuhudia utajiri wa Billionaire Mlevi asie Na akili
 
Bongo ukifa ukiwa maarufu ni tatizo mmeshaingiza uchama kila aliyeguswa na Ruge katoa ya moyoni Lowassa Maalimu Seiph Kikwete.hawa ni vyama tofauti mtu yoyote aliyefanikiwa lazima achukiwe na wachache
 
Bongo ukifa ukiwa maarufu ni tatizo mmeshaingiza uchama kila aliyeguswa na Ruge katoa ya moyoni Lowassa Maalimu Seiph Kikwete.hawa ni vyama tofauti mtu yoyote aliyefanikiwa lazima achukiwe na wachache
Sasa mbona yaliyotoka moyo wa Dudubaya mnayapinga?! Kutoa yake ya moyoni sio lazima ziwe sifa, hata lawama ni yametoka moyoni mwake. Ukipenda kupendwa jua wapo wanaokuchukia kwa magnitude ileile unayopendwa.
Sioni kwanini Mwakwembe aseme eti Rais kaguswa katweet, lakini huyu dudubaya yeye haguswi. Kwani akiguswa Rais unadhani wooote tumeguswa? au wananchi woote tunalazimika kuguswa? muwe na torelance kwa wenzenu, mistake tulazimishane kupenda au kuchukia. Kila mtu anafikra huru na hizo ndizo huzaa hisia huru na maoni huru.
 
Naomba niwakumbushe jambo moja,Mwalimu Nyerere aliwaagiza polisi Mwanza kuwaachia huru mara moja Wahutu na Watusi waliojimwaga barabarani kushangilia vifo vya Marais Rwanda na Burundi ambao ndege yao ilitunguliwa Mwaka 1994 wakitokea Tanzania kwenye mkutano wa upatanishi.

Mwalimu alisema huwezi kumzuia mtu kushangilia kufa kwa adui yake na kweli warundi hao na wanyarwanda waliachiliwa mara moja.

Naaamini na ninaendelea kuamini kwamba si kila mtu anaweza akasikitika na kuombeleza kifo cha mtu ambaye hana ukaribu naye ama ana mahusiano naye mabaya.

Nawatakia mchana mwema,mimi naomboleza kifo cha Ruge

R.I. P. Ruge Mutahaba
 
Dudu baya Moja ya Lawama zake Ni kudhulumiwa Na Ruge Na Clouds

Lakin hapo hapo analaumu Clouds kumpotezea
Sasa Kwanini ulaumu anaekudhulumu akiamua kufanya nawe Biashara ya kukudhulumu?

Dudu baya anatuambia Kila Mara Kuwa Clouds wamemshusha kimziki Ila anajizuia kutuambia nani alimpaisha Ki muziki

Ujinga ni kutaka usaidiwe ki lazima

Hapo hapo analalamika kudhulumiwa Halafu analalamika hawakuwa Na Mkataba ( Makubaliano), sasa Kama ulikubali kufanya Kazi Na Mtu bila ya makubaliano hoja ya kusema kakudhulumu inatokea wapi?

Ruge kaondoka, tunatega masikio Na macho kushuhudia utajiri wa Billionaire Mlevi asie Na akili
Hawezi kunyanyuka tena, muda wake ulishapita. Watu tulioruka debe kipindi anatamba na nyimbo kama nampenda mpezi usiopenda chapaa sasa hivi tunakaribia kupata wajukuu. Yule anapambana na historia
 
Dudu katoa ya moyoni ata kama katoa wakati usio sahihi lakini kwamwaga nyongo yake .
Najua na naamini wapo wengi walimchukia Marehemu na wana maoni yanayofanana na ya Dudu ila UNAFKI .

Tz kwa unafki tunashika no moja Duniani na ndio kwa asilimia kubwa unaotutafuna.
Kiongozi mkubwa au Tajiri anaweza akautubia watu kwa kuwakejeli au kuwatukana na pengine kafanya maamuzi ya kuwaumiza Watu wanashangilia na kupiga makofi huku unaumia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dudu katoa ya moyoni ata kama katoa wakati usio sahihi lakini kwamwaga nyongo yake .
Najua na naamini wapo wengi walimchukia Marehemu na wana maoni yanayofanana na ya Dudu ila UNAFKI .

Tz kwa unafki tunashika no moja Duniani na ndio kwa asilimia kubwa unaotutafuna.
Kiongozi mkubwa au Tajiri anaweza akautubia watu kwa kuwakejeli au kuwatukana na pengine kafanya maamuzi ya kuwaumiza Watu wanashangilia na kupiga makofi huku unaumia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Umesema kweli na mimi sipendi unafiki, kujipendekeza ili upate kitu bila kujali unaumiza wangapi. Hata kam Ruge ataenda peponi, hiyo ni business yake na Mungu, wapo miongoni mwetu tuliobaki wanayo yakuueleza umma ambayo wele wampendao hawapendi kuyasikia.
Tukiuza nafsi zetu kwa sababu ya fursa za kupewa sasa uhuru wa mawazo uko wapi?
 
Who the hell is dudubaya??? Katoa hata ajira kwa watu wawili? Mxiewwww
I would care less about ajira, but I respect him as a human. Yani wewe unawatukuza waliokuajiri tu, unasahau utu wa mtu. kwani who is Ruge by the way, unadhani kwakua kuna watu aliwapa ajira hivyo wooote tutamtukuza.
I will stand by Dudubaya, unafiki mbaya sana.
 
I would care less about ajira, but I respect him as a human. Yani wewe unawatukuza waliokuajiri tu, unasahau utu wa mtu. kwani who is Ruge by the way, unadhani kwakua kuna watu aliwapa ajira hivyo wooote tutamtukuza.
I will stand by Dudubaya, unafiki mbaya sana.

hahaa kama wewe unavyostand na Dudubaya,wengine wana stand na Ruge..

hakuna anayekulazimisha umsujudu Dudubaya,ila ndio utolerate kuwaona wengine wanamsujudu Ruge katika mazingira hayo hayo ambayo wewe umo….kila mtu ana choice yake mkuu...tusilazimishane…

who is Ruge???? leo kufa wewe au huyo Dudubaya uone kama hata watu wawili watajitokeza kweye mazishi yako….

Kama ni kutoka kimziki,Dudu baya sio msanii wa juzi,kama alibanwa alifanya nini kukabiliana na hilo...saa nyingine tuna attribute kushidwa kwetu kwa mtu mmoja..is not fair...

Alitoa ajira yes,kama humtukuzi kuna watu watamtukuza….ndio maana kunakuwaga na medal,badges,tuzo za heshima...ni wachache sana watafikia kupewa heshima ndani ya jamii..au wewe unadhania usipompa heshima basi watu wote hawatamuheshimu?? baki na lidudubaya lako..linachojua ni kutumia mabavu kumbe sehemu nyingine inayotumika ni akili… konki konki konki ...my Ars***
 
hahaa kama wewe unavyostand na Dudubaya,wengine wana stand na Ruge..

hakuna anayekulazimisha umsujudu Dudubaya,ila ndio utolerate kuwaona wengine wanamsujudu Ruge katika mazingira hayo hayo ambayo wewe umo….kila mtu ana choice yake mkuu...tusilazimishane…

who is Ruge???? leo kufa wewe au huyo Dudubaya uone kama hata watu wawili watajitokeza kweye mazishi yako….

Kama ni kutoka kimziki,Dudu baya sio msanii wa juzi,kama alibanwa alifanya nini kukabiliana na hilo...saa nyingine tuna attribute kushidwa kwetu kwa mtu mmoja..is not fair...

Alitoa ajira yes,kama humtukuzi kuna watu watamtukuza….ndio maana kunakuwaga na medal,badges,tuzo za heshima...ni wachache sana watafikia kupewa heshima ndani ya jamii..au wewe unadhania usipompa heshima basi watu wote hawatamuheshimu?? baki na lidudubaya lako..linachojua ni kutumia mabavu kumbe sehemu nyingine inayotumika ni akili… konki konki konki ...my Ars***
Hahaha hayo maisha yao mimi namuunga mkono Dudubaya, hakutaka unafiki hata kama atabaki peke yake aliyasema aliyotaka kusema na huo ndio uanaume sio kuwa mnafiki na kujipendekeza.
Dudubaya ana moyo kama wale waliotoa yao ya moyoni, Eti kwa sababu Magufuli alitweet kwanza akisikitishwa sasa Tanzania nzima tusikitishwe? Hata mimi sisikitishwi, Simfahamu ruge na sijui kwanini wanalazimisha uwe msiba wa taifa wakati ni msiba wa familia ya Ruge.
Mliosaidiwa nendeni mkaomboleze lakini sio mlazimishe na tusiomfahamu Ruge tuomboleze, sisi hatumfahamu zaidi ya kumsoma humu kwenye media.
Nitasimama upande wa Dudu baya, name sipendi unafiki vilevile na kujipendekeza mwiko.
 
Hahaha hayo maisha yao mimi namuunga mkono Dudubaya, hakutaka unafiki hata kama atabaki peke yake aliyasema aliyotaka kusema na huo ndio uanaume sio kuwa mnafiki na kujipendekeza.
Dudubaya ana moyo kama wale waliotoa yao ya moyoni, Eti kwa sababu Magufuli alitweet kwanza akisikitishwa sasa Tanzania nzima tusikitishwe? Hata mimi sisikitishwi, Simfahamu ruge na sijui kwanini wanalazimisha uwe msiba wa taifa wakati ni msiba wa familia ya Ruge.
Mliosaidiwa nendeni mkaomboleze lakini sio mlazimishe na tusiomfahamu Ruge tuomboleze, sisi hatumfahamu zaidi ya kumsoma humu kwenye media.
Nitasimama upande wa Dudu baya, name sipendi unafiki vilevile na kujipendekeza mwiko.

MMMMNhhhh

ngoja nikalale mie...Post yako hii nzima yote imejaa neno unafiki..tehee tehee..sijui umekosa linguine la kusema? lol..angalia tena research zinasema Watanzania ni wanafiki..sasa wewe Na dudubaya wako mkatafute nchi ya kuishi ambayo watu wake sio wanafiki

...nani kakulazimisha msiba wa Ruge uwe wako,as far as I know..kila mtu yuko huru kufanya analotaka kipindi hiki...

..serikali inatambua mchango wake katika jamii yetu ndio maana imetaka kuwa involved haijakulazimisha uende Bukoba kuzika??!!

My last post to you..si vizuri kuongelea ujinga ,ujinga tu..sijui hata kwa nini najibu hii topic lol

.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom