chuse tbr
JF-Expert Member
- Aug 11, 2013
- 483
- 545
mie muislam ila nimekupa like maana unajitambua na unaitumia akili yako vizuri kuliko kufata kibubusaPole sana kwa Masaibu yaliyokupata Mkuu.
Jifunze kuwa Mfuasi wa Kristo na si Mfuasi wa haya Makanisa wala Watumishi wake wa Kimwili.Ukiwa Mfuasi wa Kristo hutohitajika kumuona kwa Fedha wala Sadaka (Gharama ya kuonana na Kristo ni Maombi na kusoma Neno la Mungu).Pia unaonana naye muda wowote.
Ukiisoma Biblia vizuri (Si kusoma vifungu), basi utagundua kuwa tunachezewa abrakadabra nyingi sana na hawa watu wanaojiita Manabii, Wachungaji nk.
Yesu aliagiza "Kuenenda ulimwenguni kuwafanya Mataifa yote kuwa wanafunzi, tukiwabatiza kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu" (Mathayo 28:19).Si kujenga Nyumba na kuchuna Fedha sehemu miaka nenda rudi.
Hizi sinema za Makanisa lukuki kila uchwao ni Uchafu tu uliojificha kwa mwamvuli cha kueneza neno la Mungu.
Makanisa hayawafundishi watu neno la kweli.Kazi yao ni Kuhubiri kupiga hela tu na si vinginvyo.Hii inakera sana na inarudisha nyuma imani za wachache waaminio.
Mahubiri yametawaliwa na Kupigana vijembe, unazi, ushaitwani nk.Je Injili ya Kristu itafundishwa muda gani?.
Nimeishaachana na haya Makanisa ya dili, Dini yangu iliyo safi isiyo na taka mbele za Mungu ni hii, kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo Mawaa (Waraka wa Yakobo 1:27).