Kutoa ajira kwa waliofeli divisheni 4 tena kuanzia point 28 mpaka 31 ni kutuharibia jamii

Chuki ni mbaya acha....mnalilia ajira zikitolewa mnavimba mpaka mnataka kupasuka...kama ajira zinawahusu four div 28-31 wewe si usubiri zikitoka za 1&2 ukaombe mkuu.
Halafu hao necta wanapopanga madaraja ya ufaulu hawajawahi kusema kwamba div four ni failure acha kupotosha umma,unaweza kufaulu sana lakini ukafeli katika utendaji wa kazi.
Wameamua kutoa ajira kwa form 4 huku wakijua nyie wasomi mpo cha msingi subiri zikitoka zinazowafaa wasomi wetu.
Kuna vichwa havitakiwi kupewa nafasi ya kuamua kwa ajili ya taifa.

unapotoa kipaumbele cha ajira kwa div 4 point 28 mpaka 31 na ukawaacha kuanzia pointi 27 kushuka chini na wengi wako mtaani hawana ajira unapeleka taarifa gani katika jamii kuwa kusoma sana hakuna maana? kwamba kufaulu siyo justification ya utendaji sasa kufeli ndiyo justification?

kwa nini wasiseme tunaajiri kidato cha nne na wale wa kidato cha nne wote walioko mtaani wajitokeje kugombania na wao wawachambue kulinganisha sifa mbalimbali ikiwemo elimu, lakini hawa wamekwisha wabagua wenye ufaulu mzuri kwa kuwaonyesha hawana sifa. kama mtu ana div 4 ya pointi 26 au 27 hana sifa.

mimi sielewi kama mnajua mnachokitetea au wale wenye maslahi na hili?
 
Taifa haliendelei kwasababu ya fikra kama hizo. Kuthamini sana ujuzi wa kwenye makaratasi (vyeti) kuliko kuwapima vijana kwa uwezo wao wote. Binadamu wana uwezo wa kukariri aliyofundishwa, kugundua mambo mapya na uwezo wa kukubalika kwenye jamii kutokana na kipaji alichonacho.
Kupata Divesheni 4 kwenye mtihani - sio kwamba huyu kijana hana akili. Nao wapewe nafasi kwenye ajira.
unachokiandika kinakubaliana na hoja yangu ila hata wewe hukielewi unakaa kubisha tu. mimi hoja yangu ni wawaite vijana wote waliohitimu kidato cha nne miaka ya nyuma .

kama kuna divisheni 1, 2 mpaka 3 ambao walibahatika kuendelea na kidato cha tano lakini matokeo ya kidato cha sita yakawa mabaya hawakuendelea huyo ataomba. kuna wenye ufaulu mzuri lakini kombinesheni ziligoma na wazazi hawana uwezo wa kuwaendeleza nao wataomba, kuna wengine wana 4 za pointi chini ya 28 lakini hawakwenda popote nao wataomba pamoja na hao wa pointi 28 mpaka 31.


wakiomba hawa watachambuliwa kwa kutumia vigezo vingine pamoja na elimu zao.

kama unasema elimu haionyeshi utendaji wa mtu sasa mtuambie ni kigezo gani kinatumika kuchagua hawa divisheni 4 ya pointi 28 mpaka 31 na kuwaacha wengine?

hawa wenye fikra za hivi itakuwa hata kwenye mafunzo yao wanawatunuku waliofeli ndiyo wanaopewa nishani na promosheni

huwezi kukataa kutambua mifumo ya kupima ufaulu au juhudi za wanafunzi katika kufutailia kile wanachoelekezwa kufanya
 
Mambo yamebadilika ndugu yangu. Yale mambo ya kutumia nguvu yameshapitwa na wakati. Sasa hivi nchi zinazojitambua kila kitu wanatengeneza wenyewe (wanajeshi wenyewe)
Hawa dvn 4 ndiyo wale wanavunja matofali kwa kichwa, mara analala, gari inapita juu yake. Ukitupiwa bomu nalo utalipiga kwa kichwa?
Tunataka tuone jeshi linatenda haki, watu wamevumbua bunduki, drone, gari n.k
Chukulia makambora 50 yamerushwa kwenye nchi yako, unatumia teknolojia gani kuyalipua yote kabla hayajatua kwenye ardhi yako? Wanaotakiwa kwenda jeshi ni 1-3 hawa utawaendeleza mpk watakuwa na PHD
Jeshi linahitaji madaktari, marubani, wanaIT (teknolojia), wanasaikolojia n.k ukiaangalia ni wasomi ndiyo wanaohitajika.
Kwa hiyo unatuaminisha kwamba 1-3 Wana teknolojia ya wa kulipua makombora 50 yakirushwa?? Elimu ya bongo ni mwenye uwezo wa kukariri ndo anafaulu braza ukijibu kwa ufahamu unafeli. Kuna watu wamesoma hadi PhD lakini ni weupe hamna kitu zaidi ya karatasi la Cheti. Na kama ishu ni hayo makaratasi hata mtu wa division 4 anaweza kuanza certificate Hadi level yoyote. Kumbuka Kuna watu Wana degree na PhD zao ila o-level walikuwa na division four kama hizo ulizozitaja.


Na vilevile ww mwenye division one au 2 unachomzidi division four ni msuli wa kukariri tu yaliyoandikwa ila Kwa mfano mnaweza mkapewa social based interview akakuzidi upeo na kujiamini. Na kuhusu matumizi ya teknolojia, sio kila mwenye elimu kubwa anaweza hiki kitu, Kuna watu Wana degree ila hata kuwasha kompyuta hawajui, ila Kuna form four wa division 4 anachezea kompyuta utadhani aliitengeneza yeye.
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Siyo wote walio feli hawana akili hapana wengine walifeli kwa sababu za kibinaadamu ikiwemo maradhi kuukamia mtihani na maandalizi mabovu ya mtihani
 
Back
Top Bottom