Kutoa ajira kwa waliofeli divisheni 4 tena kuanzia point 28 mpaka 31 ni kutuharibia jamii

Kwa elimu ya kidato cha nne alifeli huyo maana hata form five haendi huyo.

lakini pointi yangu ajira kama tunaajiri kidato cha nne basi tushindanishe wa kidato cha nne walioko mtaani na kati ya wale watakaojitokeza basi tuchukue the best katika hao.

kwa vigezo vyao kama mtu alipata divisheni 2 au 3 na hana lolote kwa sasa maana kuna mtu anaweza kupata hata 1 form four na six akachemsha lakini hawa wanasema huyo hana vigezo
Hicho ni kigezo kidogo sana chakumpima binadamu , je wote waliofeli hawajaweza kufanikisha chochote katika maisha yao!?
Je waliofaulu wote wamefanikiwa !?
Kufeli elimu haimaanishi your useless still unaweza ukafanya jambo. Wamepewa nafasi wacha waitumie.
 
F = Fail
A,B,C,D = Pass
Mr J alisoma mchepuo wa sayansi O'level na alipata matikeo kam ifuatavyo.

Math =F
Eng. =F
Phy =D
Chem =D
Bio. =D
Geo =D
Hist. =D
Kisw. =D
Civ. =D
Bible. =F
Hiyo ni sawa na division 4 point 28.

Vip huyo amefeli pia....
Mr J anasifa za kusoma hadi PHD.
Mleta mada ni KILAZA na pia huwezi jua position ambayo hao watu wanahitajika
 
Mtoa mada hujaelimika hata kama umefika chuo kikuu unaweza zidiwa na hao div 4.
Aliekwbia div ni failure nani.
NECTA ndio wana eleza kuwa div4 ni failure au wizara ya elimu?
Kamsome plato upya jinsi ya kupanga makundi ya watu kuanzia Gold mpaka Silver.
Huna lolote kichwani, jeshi huwa linatoa special chance kwa graduate.
Umesoma mpaka chuo bado unawivu na vinafasi vya watu wa chini.
Anzisha kampuni uajiri wahitimu wenye digrii lakin usiipangie serikali.
yaani haya unayoyatetea ndiyo unajiona msomi wa ku quote plato????

elimu yetu ni shida tupu watu kukalili majina ya wanafalsafa wanaona wamejua.

narudia tena tangazo la ajira la serikali la kusema tunaajiri form 4 divisheni 4 pointi 28 mpaka 31 limetoka kwa kilaza anayetuharibia jamii. Tutajenga jamii yetu kwa kutengeneza ushindani ambao kila mwanajamii ataona anayejitahidi kusoma kwa bidii au kufanya kazi kwa bidii ndiye anayefanikiwa.

Lakini waliokalili sijui kuna makundi ya plato, kwamba plato alisema wanaopata sifuri ndiyo wenye akili hivyo akitaka kuajiri nafasi za umma anaita wenye sifuri hao siyo wasomi bali wamekalili tu
 
Mleta mada ni KILAZA na pia huwezi jua position ambayo hao watu wanahitajika
kilaza ni yule anayeamini kuna nafasi za vilaza hutakiwi kuweka watu wenye uelewa.

kama uliapata divisheni 3 na huna jambo lolote unalofanya, hukuendelea na lolote na mwingine akapata 4 ya 28 naye hana analolifanya yupi kilaza kati ya mimi ninayesema waite wote walinganishe na uchukue kwa kuchanganya na vigezo vingine na wewe unayekubali eti aitwe divisheni 4 tena pointi 28 mpaka 31 tu. huyu mwenye 2, three na four za mwanzoni hawana vigezo.

hizi ni hoja za watu waliofeli kulazimisha kuwa wao ni bora kuliko waliofaulu kuwashinda.
 
Hahahaaaaa, yani nimecheka sana.Ktk nchi ambazo watu wanaelewa maana ya jeshi huwa raia wake hawakimbilii kujiunga na jeshi.Bali hujiunga na jeshi baada ya kushawishiwa sana aidha kimaslahi au kipropaganda. Nashangaa Bongo watu wanapigana vikumbo kujiunga jeshini.
 
yaani haya unayoyatetea ndiyo unajiona msomi wa ku quote plato????

elimu yetu ni shida tupu watu kukalili majina ya wanafalsafa wanaona wamejua.

narudia tena tangazo la ajira la serikali la kusema tunaajiri form 4 divisheni 4 pointi 28 mpaka 31 limetoka kwa kilaza anayetuharibia jamii. Tutajenga jamii yetu kwa kutengeneza ushindani ambao kila mwanajamii ataona anayejitahidi kusoma kwa bidii au kufanya kazi kwa bidii ndiye anayefanikiwa.

Lakini waliokalili sijui kuna makundi ya plato, kwamba plato alisema wanaopata sifuri ndiyo wenye akili hivyo akitaka kuajiri nafasi za umma anaita wenye sifuri hao siyo wasomi bali wamekalili tu
Form 4 akikuuliza wewe kama msomi umebuni nini zaidi yake ili upewe ajira halafu yeye anyimwe utamjibu nini? .
Wewe hio digrii yako ninamashaka nayo makubwa sana, unavyotetea usomi halafu unapingaba na kanuni walizoweka wasomi.
Wewe nani anakutambua mpaka umpinge plato,tafiti gani umefanta au falsafa zipi umeanzisha?
Kwa taarifa yako nchi na mifumo inaongozwa kwa mifumo waliotunga kina plato, carlmax nk kama utaendelea kubisha hio digrii unyang'anywe haina tija.
 
Wewe ni mbuzi labisa kabla ya hiyo elimu ya form 4 watu walikuwa hawafanyi kazi?

Ujinga unakusumbua kinachofanya kazi siyo elimu ni ubongo wa mtu ni wangapi wamfaulu na hawawezi kazi?

Ni wangapi hawajafaulu na wanaweza kazi?
 
Ukiona hivyo, mtoa tangazo ana mbumbumbu wake kubao nyumbani. Matatizo yanayolipata jeshi la polisi kwa sasa ni kuwa na askari wengi wenye elimu ndogo. Uhamiaji mna iga? Kuzolota kwa elimu nchini lililetwa na kozi ya ualimu kuwachukua 'waliobaki' baada ya kuengua wa kuendelea na masomo na kozi zingine. Kuna walio faulu zaidi ya div 4 wamekosa nafasi kuendelea A level au vyuo wapo mitaani, kwa nini wazuiwe kuomba? Kuwa na failures uhamiaji ni sifa?
Kwani sasa hivi hakuna digrii holder shule ya msingi, mbona mambo yapo vilevile.
Suala ubora wa elimu ni pana sana linahitaji kitabu kizima kulielezea.
Walimu wa upe wamewafundisha mpaka mmeota mapembe halafu mnawadharau.
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Tanzania hatua tuliyo nayo haihitaji mtanzania mwenye akili. Yaani kama una akili wanakuua/kuku frustrate wasiokuwa na akili mpaka uchanganyikiwe au uozee kabulini. Ila ipo miaka itafika ambapo wenye akili watahitajika.
 
huu upuuzi kbsa, kuzan kuwa ufaulu wa darasan, unaendana na utendaji wa kazi, hizi colonial education zmewaharbu sana akil kwa kuwapa vipaumbele hao wasomi uchwara ktk kila jambo mnataka wapendelewe.

kufel form4 sio kigezo cha mtu kukosa akil na uwajibikan, kufaul form4 sio kigezo cha kuwa muwajibikaj, achen fikra potofu, jiulizen kwann matatizo hayakakwishi nchini japo kuna wasomi weng ktk kila nyanja???? mtoa mada bado ana mindset zakitumwa
Acha kutetea vilaza mkuu. Kwa hiyo huyo division 4 anaweza fanyaa vizuri mambo ya kiteknolojia ukilinganisha na watu waliosoma mpaka degree level?

Ni kujaribu ku'justify" ujinga tu.
 
Acha kutetea vilaza mkuu. Kwa hiyo huyo division 4 anaweza fanyaa vizuri mambo ya kiteknolojia ukilinganisha na watu waliosoma mpaka degree level?

Ni kujaribu ku'justify" ujinga tu.
Ukute ulifundishwa na walimu waliopata division 4 za O- level lakini unavyojitutumua kuponda!
 
yaani haya unayoyatetea ndiyo unajiona msomi wa ku quote plato????

elimu yetu ni shida tupu watu kukalili majina ya wanafalsafa wanaona wamejua.

narudia tena tangazo la ajira la serikali la kusema tunaajiri form 4 divisheni 4 pointi 28 mpaka 31 limetoka kwa kilaza anayetuharibia jamii. Tutajenga jamii yetu kwa kutengeneza ushindani ambao kila mwanajamii ataona anayejitahidi kusoma kwa bidii au kufanya kazi kwa bidii ndiye anayefanikiwa.

Lakini waliokalili sijui kuna makundi ya plato, kwamba plato alisema wanaopata sifuri ndiyo wenye akili hivyo akitaka kuajiri nafasi za umma anaita wenye sifuri hao siyo wasomi bali wamekalili tu
wewe ego kweli ni kiazi grade 1 na unafananana jina lako EGO

watu wameajiriwa kutokana na level zao za kielemu kama hiyo wizara ina anjiri watu wa division basi hao ndio wanaitajika kwenye hiyo kazi, endapo wangeitaji wstu wenye division 1,2, na 3 basi wangetangaza ajira kw hao wenye division hizo.

wewe hujui kwanini hiyo wizara ina hitaji watu wa division 4 unakuja na mawivu yako na husda kwanini eti kwanini wanaajiri division 4

cha kikuelesha ni kwamba hizo ajira zinawafit watu wa division 4 ya 28 ndio maana yakuitwa, kama zikitokea ajira za kuwafit nyie wa division 1 na nyie mtaitwa kwa wakati wenu

you are so EGO! mr ego
 
Sekta kama magereza, uhamiaji, polisi na jeshi walitakiwa waajiriwe watu wenye elimu kuanzia form 6, diploma, degree na kuendelea.
Lengo la kuwajiri waliofeli ni kuendelea kutumika kisiasa leo hii jeshi la polisi limekuwa la kisiasa.
Matumizi ya silaha na nguvu hayahitaji diploma wala divisheni one.
Kimsingi majeshini hakuhitaji maarifa ya vitabuni.

Kule utafundishwa mahalifa ya kupigana, kushambulia na kujihami.

Ndio maana utakuta makundi ya waasi pamoja na kuwa yanaundwa na watu waliokosa shule ambao ni kizazi cha watoto wa mitaani na hata umri wao unakutabmpaka miaka 7 tu lakini wanakuwa na uwezo mkubwa sana wa kupigana na kuyatoa kamasi majeshi rasmi ya serikali.

Kwa kifupi majeshini hakuhitaji mbwembwe za div one sijui degree ama masters.

Huku wanatakiwa std 7 maana hawa ndio wenye moyo na morali wa kupigania kile walichoelekezwa na wakubwa wao, hao wenye mavyeti na madigree wanafuata maslahi tu na vita ikianza wanaogopa kufa.

Kwa upande wangu naona wasomi ndio wameharibu majeshi maana wako kimaslahi zaidi kuliko utendaji.
 
F = Fail
A,B,C,D = Pass
Mr J alisoma mchepuo wa sayansi O'level na alipata matikeo kam ifuatavyo.

Math =F
Eng. =F
Phy =D
Chem =D
Bio. =D
Geo =D
Hist. =D
Kisw. =D
Civ. =D
Bible. =F
Hiyo ni sawa na division 4 point 28.

Vip huyo amefeli pia....
Mr J anasifa za kusoma hadi PHD.

Yani huyu kapataje English F?
 
Siyo kweli katika sekta ambayo inahitaji wasomi na wanasayansi ni jeshi, polisi, magereza na uhamiaji.
Kila siku technolojia mpya inaibuka, huyu aliyefeli anaweza kupewa kazi ya ujasusi? Huyu aliyefeli anaweza kutengeneza website au virus au software yoyote kulinda taarifa zisiharibiwe na virus?
Wasomi wanahitajika sana, sasa hivi siyo km miaka ile ya 1945 ya vita ya pili kutegemea bunduki.
Sasa hivi mtu 1 au 5 wanaweza kuingamiza nchi na mkafa wote. Watu wanaingia laboratory wanatengeneza virus kisha watuma kwenye nchi yako kisha wanatengeneza na dawa. Unakufa huku unamtajirisha adui
Zama za nguvu zishapitwa na wakati sasa hivi watu wanatumia akili nyingi nguvu kidogo
Ndio wasomi wanahitajika ila wachache sana.
Matumizi ya nguvu jeshini huwezi kuyapitisha wakati hata sikumoja.

Utimamu wa mwilinndio nguzo ya jeshi. Pamoja na masayansi na matekinolojia bado majeshi makubwa duniani yanaajiri kwa wingi vijana kuanzia 18yrs na kuwapakia kwenye madege kwa ajili ya kwenda kupigana kwenye majabali na majangwa ya mashariki ya kati kwenye mazingira magumu sana.

Labda tuseme Jeshini kwa sasa wanahitajika vijana mafundi na wanasayansi wachache lia darasa la saba wanatakiwa jwa wingi zaidi maana hawa ndio wenye kazi ya kukesha nje na kulala macho wakati wenye digree walalala usingizi fofofo wakilindwa na hao std 7.

So wasomi si mhimili wa jeshi bali hawa std7 ambao ndio junior officers.

Wasomi wanataka waingie jeshini ili waendeshe maisha mazuri ila hawako tayari kukaa vikosi vya maporini kulala macho.
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Hujui kitu we Mbuni, jeshi linahitaji wataohudunu kwenye vyeo vidogo kwa mda mrefu sasa ukimuweka bachelor holder unadhan ni kwa mda gani atahudumu kama Private?
 
Kwa bongo yetu wasomi wengi uingia jeshini kimaslai tu na kama ajira zingekuwepo za kutosha kwa kila taaluma wala usiongeona watu wa degree wanajazana huko jeshini, jeshi linataka watu watakaojitolea kufa na kupona na sio kupata mishahara na vyeo vikubwa mkuu nawasilisha.
Umeeleweka sana mkuu. Wasomi sio wafia nchi bali ni wapigadili tu jeshini hamna kitu mle sema tu mambo yameshakuwa magumu siku hizi.

Tangu mwanzo majeshi yalikiwa ni kazi za watoto wa familia maskini na watu wa mkoa wa mara.

Wakati ajira hazijawa shida na jeshi kuboreshwa kimaslahi na kimuundo watoto wa masikini tu ndio walikuwa na option pekee ya jeshi.
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Kuna vyuo uchwara wanatangaza redioni/ runinga nafasi za masomo, uuguzi n.k. wanaweka ufaulu wa chini kabisa kama kigezo cha kujiunga nao. Unajiuliza ni mkunga au muuguzi wa aina gani atakayetoka hapo akutibu?
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom