EMM_411
Member
- Mar 24, 2011
- 27
- 7
Nina jirani yangu ambaye nyumba zetu zinatazamana tunaishi pamoja maeneo ya Bunju, leo jioni nilimtuma mwanangu akamfungulie ndama ambaye alikua amefungwa nyuma ya uzio wa nyumba yetu. kwa bahati mbaya hakumkuta ndama, ndama huyu alikuwa amekimbilia kwa jirani yangu. Mtoto wangu akaenda kumfuatilia ndama huyo na kumkuta yupo kwa jirani yangu akila majani (sio akiiba), wakati kijana akiendelea kumtoa ndama kwa jirani yangu huyu, jirani aliwasili na gari lake na kumkuta kijana wangu akiwa kwake huku akiwa na ndama yule. Jirani alimuhoji kijana wangu kwanini ndama alikuwa kwake, kijana alijaribu kumuelewesha jirani yangu huyu mwenye jabza bila maelewano, ndipo alipomwambia samahani ndama alifungua, jirani kwa jazba akamwambia kijana wangu "NITAKUPIGA RISASI,NIMEKATAZA NG'OMBE KUJA KWANGU" hakuishia hapo bali alitoa Bastola yake na kumwelekezea kijana wangu huku akimwambia "NITAKUUA" Sasa mimi nilikuwa naomba kuuliza kisheria, Je jirani yangu ana haki ya kumtishia mwanangu Bunduki? Je ni hatua zipi za kisheria napaswa kumchukulia jirani yangu huyu?
Nawasilisha!
Nawasilisha!