Tunashukuru uchaguzi umeisha salama bila vita au fujo kubwa. Kwa kuwa ni wazi kuwa uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa na mizengo hata kupelekea CHADEMA na wanachama, mashabiki na wananchi kwa ujumla wao kuamini hawakutendewa haki. Hivyo ili CCM iwezekuongoza na wala sio kutawala kama walivyozoea watafute namna gani watawashirikisha kwenye uongozi. Nadhani wangepewa spika wa bunge nchi ingelikua na amani zaidi. CCM wafanye mbinu zote kuhakikisha spika ni Dr. Slaa. Kama kigezo ni lazima awe mbunge ateuliwe na raisi kati ya kete zake kumi. Hii itakuwa imepunguza majeraha ya CHADEMA na CCM kuweza kuongoza nchi kwa amani na heshima kwa wananchi wote