Kuteswa kwa Kibanda: Kubenea aliumbua Jukwaa la Wahariri (TEF)

Status
Not open for further replies.
Gazeti la Mwanahalisi lilikuwa linamilikiwa na Saed Kubenea lilifungiwa miezi kadhaa iliyopita kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi iosipokuwa tu “uchochezi” – kufuatana na barua aliyoandikiwa na idara ya Maelezo.

Barua haikueleza ni “uchochezi” upi isipokuwa tu inaaminika kutokana na habari gazeti lilikuwa likiandika kuhusiana na kutekwa na kuteswa Ulimboka.

Mwanahalisi lilianza kufanikiwa kupata undani wa wa kutekwa na kuteswa kwa mwanaharakati huyo kwani kidole kilianza kuonyesha Ikulu kwa maana afisa mmoja wa usalama (TISS) ndiye mhusika mkuu.

Baada ya kufungiwa Jujwaa la Wahariri (TEF) lilimuona Kubenea ni “mkosaji” kwa kuandika habari zile na lilimtaka akubali kosa kwa kuandika habari ambazo wengi wa wajumbe wa TEF katika kikao kimoja waliona ni za “majungu” na wengine hata kudiriki kusema Kubenea alikuwa anakwenda kinyume cha maadili ya uandishi.

TEF ilimtaka Kubenea ashirikiane na Jukwaa hilo ili kumuombea kwa serikali gazeti lifunguliwe mradi tu kwanza akubali hilo “kosa” lake.

Kubenea aliipuuza TEF kutokana na msimamo wake huo wa ajabu na alikuwa anasusia vikao vyake.

Sasa hili la Kibanda limetokea ni kama lile lile la Dr Ulimboka ikizingatiwa ile “pattern” ya tukio. Sasa sijui TEF watawapinga wote wale watakaokuwa wanaandika habari kwa undani za kuteswa kwa Kibanda kama habari hizo zinaonyeshea kidole wahusika ambayo inaaminika ni wale wale waliomfanyia unyama Ulimboka?

Kwa maneno mengine ni kwamba iwapo wahariri watagundua “ukweli” kuhusu kuteswa kwa Kibanda watatakiwa kufunga midomo yao?

Kwa mtazamo wangu naona Kubenea amewaumbua sana TEF.

Nawasilisha

Umejidhirisha kuwa Great thinker
Kubenea aliandika ukweli mtu kwenye ile Makala lakini serikali imemfungia kwa ukweli wake
 
To be honest Tanzania waandishi wengi ni MAKANJANJA...!! Only few and dedicated one like kubenea prevail...!! Hata kibanda mwenyewe pia alimkosoa kubenea sasa yamemkuta...!! Anyways Get well soon bro hii ndo bongo..
 
To be honest Tanzania waandishi wengi ni MAKANJANJA...!! Only few and dedicated one's like kubenea prevail...!! Hata kibanda mwenyewe pia alimkosoa kubenea sasa yamemkuta...!! Anyways Get well soon bro hii ndo bongo..
 
Kwani sababu ya kufungiwa mwanahalisi ni ipi?Nilidhani ni incitement of Mutiny, ambayo hata kimataifa ni kosa kubwa kwa mhariri na mwandishi wa habari.

Pole mkuu, naona ndo unakurupuka kutoka usingizini, JF haina kulemba utaisoma plate number kwani maelezo ya Mwanahalisi na Kubenea tumesha yaandika mara kibao we ulikuwa wapi?
 
Unategemea Juma Pinto na Gazeti lake akae upande upi?vipi ulitaka wapinge wakati SACCOS ya TEF mtaji wake wa kuanzia walipewa na Ikulu,siku chache baada ya Mwana Halisi kufungiwa?Devide et Empire......Wagawanye na Uwatawale!
Akhsante ndugu,kwani mie ilinishtua sana kuona wamekubali kununuliwa kwa vipande vya dhahabu kwa bei ya jumla "kusaidiwa fedha kwa saccos yao"nikajua ni mwendelezo wa kukubali kugawanywa na kuwaona wachokonozi wanajitakia matatizo wenyewe hivyo hamna habari ya kuwatetea wenzao watakaoadhibiwa na utawala wala maovu ya IKULU na SERIKALI hatutayaona kwenye magazeti NA TANGU SIKU HIYO NIKAWEKA MGOMO WA KUNUNUA GAZETI LOLOTE LA TANZANIA ZAIDI YA RAIA MWEMA (pamoja na kuwa ninayasoma hata kwa kudandia)NA MSIMAMO WANGU UKO PALEPALE "ILI MRADI SAID KUBENEA YU HAI SINTODHUBUTU HADI ARUDI ULINGONI.
 
Nimesoma huu uzi zaidi ya mara kumi lakini sijaona sehemu yeyote Kubenea alipoliumbuwa jukwaa la wahariri.

R.I.P Mwanahalisi.
 
Tatizo kubwa la waandishi wengi wa habari hapa nchini ni NJAA,siku zote (hata kama una njaa kiasi gani)ukitaka kufanikiwa epuka kwa namna yoyote ile kufanya kazi kwa NJAA mwisho wako utakua mbaya tu.
Saeed Kubenea ni mwandishi wa habari ninayeamini siku zote aliifanya kazi yake kwa maslahi ya Taifa siyo kwa kuendekeza NJAA.
Kuna mwandishi mmoja alikua anafanya kazi TBC,alijikita kwenye hbari za kiuchunguzi akingiza NJAA kilichomkuta hadi leo simsikii,sijui kafia wapi.
 
Nimesoma huu uzi zaidi ya mara kumi lakini sijaona sehemu yeyote Kubenea alipoliumbuwa jukwaa la wahariri.

R.I.P Mwanahalisi.

Mkuu kama hujaona sisi hilo halituhusu, ni tatizo la U-kilaza wa familia na ukoo wenu; Ni dhahiri hii ni laana, Baba, Mama, na watoto wote vilaza hakuna wa kumshauri mwingine.
 
Mkuu kama hujaona sisi hilo halituhusu, ni tatizo la U-kilaza wa familia na ukoo wenu; Ni dhahiri hii ni laana, Baba, Mama, na watoto wote vilaza hakuna wa kumshauri mwingine.

Matusi ya nini sasa...
 
Tatizo kubwa la waandishi wengi wa habari hapa nchini ni NJAA,siku zote (hata kama una njaa kiasi gani)ukitaka kufanikiwa epuka kwa namna yoyote ile kufanya kazi kwa NJAA mwisho wako utakua mbaya tu.
Saeed Kubenea ni mwandishi wa habari ninayeamini siku zote aliifanya kazi yake kwa maslahi ya Taifa siyo kwa kuendekeza NJAA.
Kuna mwandishi mmoja alikua anafanya kazi TBC,alijikita kwenye hbari za kiuchunguzi akingiza NJAA kilichomkuta hadi leo simsikii,sijui kafia wapi.

Mkuu hilo liko wazi, huwezi kula fedha za mafisadi kisha ukawageuka na wewe ukaendelea kuwa salama. Kumbuka kauli ya Mizengwe iliyopinda " Mafisadi wana nguvu sana inabidi twende nao pole pole".
 
Kubenea huwezi kulazimisha kuwa ulikuwa unamtetea Ulimboka mbona alikukana, wewe ulikuwa unatumia matatizo aliyopata Ulimboka kupata pesa kuuza gazeti lako tu.
 
Kubenea huwezi kulazimisha kuwa ulikuwa unamtetea Ulimboka mbona alikukana, wewe ulikuwa unatumia matatizo aliyopata Ulimboka kupata pesa kuuza gazeti lako tu.

Thibitisha kwamba Dr Uli alimkana Kubenea.
Acha porojo za kwa mtoro wewe.
 
Kubenea huwezi kulazimisha kuwa ulikuwa unamtetea Ulimboka mbona alikukana, wewe ulikuwa unatumia matatizo aliyopata Ulimboka kupata pesa kuuza gazeti lako tu.

Kuna uK na uKenge.
 
Kubenea huwezi kulazimisha kuwa ulikuwa unamtetea Ulimboka mbona alikukana, wewe ulikuwa unatumia matatizo aliyopata Ulimboka kupata pesa kuuza gazeti lako tu.

Hapo ndipo unapokosea; Jiulize swali moja tu endapo Saed Kubenea aliandika habari za ki-uchochezi kwanini serikali ya muishiwa dhaifu ameshindwa kumfungulia kesi mahakamani hadi leo hii, wakakimbilia kulifungia gazeti lake, je Mwanahalisi lilikuwa na kosa gani?
 
Gazeti la Mwanahalisi lilikuwa linamilikiwa na Saed Kubenea lilifungiwa miezi kadhaa iliyopita kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi iosipokuwa tu “uchochezi” – kufuatana na barua aliyoandikiwa na idara ya Maelezo.

Barua haikueleza ni “uchochezi” upi isipokuwa tu inaaminika kutokana na habari gazeti lilikuwa likiandika kuhusiana na kutekwa na kuteswa Ulimboka.

Mwanahalisi lilianza kufanikiwa kupata undani wa wa kutekwa na kuteswa kwa mwanaharakati huyo kwani kidole kilianza kuonyesha Ikulu kwa maana afisa mmoja wa usalama (TISS) ndiye mhusika mkuu.

Baada ya kufungiwa Jujwaa la Wahariri (TEF) lilimuona Kubenea ni “mkosaji” kwa kuandika habari zile na lilimtaka akubali kosa kwa kuandika habari ambazo wengi wa wajumbe wa TEF katika kikao kimoja waliona ni za “majungu” na wengine hata kudiriki kusema Kubenea alikuwa anakwenda kinyume cha maadili ya uandishi.

TEF ilimtaka Kubenea ashirikiane na Jukwaa hilo ili kumuombea kwa serikali gazeti lifunguliwe mradi tu kwanza akubali hilo “kosa” lake.

Kubenea aliipuuza TEF kutokana na msimamo wake huo wa ajabu na alikuwa anasusia vikao vyake.

Sasa hili la Kibanda limetokea ni kama lile lile la Dr Ulimboka ikizingatiwa ile “pattern” ya tukio. Sasa sijui TEF watawapinga wote wale watakaokuwa wanaandika habari kwa undani za kuteswa kwa Kibanda kama habari hizo zinaonyeshea kidole wahusika ambayo inaaminika ni wale wale waliomfanyia unyama Ulimboka?

Kwa maneno mengine ni kwamba iwapo wahariri watagundua “ukweli” kuhusu kuteswa kwa Kibanda watatakiwa kufunga midomo yao?

Kwa mtazamo wangu naona Kubenea amewaumbua sana TEF.

Nawasilisha
Hiki ndio kipindi nalimisi sana Mwanahalisi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom