Kuteswa kwa Kibanda: Kubenea aliumbua Jukwaa la Wahariri (TEF)

Status
Not open for further replies.
Adui wa Watanzania ni unafki. Miezi michache iliyopita Absalom Kibanda aliitwa mnafki na Baadhi ya Memba JF humu JF kisa tu kaamua kujiunga kwa muajiri wakidai si mwenye msimamo leo wanajifanya eti kafanyiwa mbaya kwa sababu ya msimamo usioyumba Mjifunze kuacha kulaumu watu na kufanya Political analysis bila ya kuwa na utaalamu!

leo umetoa hoja ina nguvu bila kuuma uma maneno
 
Adui wa Watanzania ni unafki. Miezi michache iliyopita Absalom Kibanda aliitwa mnafki na Baadhi ya Memba JF humu JF kisa tu kaamua kujiunga kwa muajiri wakidai si mwenye msimamo leo wanajifanya eti kafanyiwa mbaya kwa sababu ya msimamo usioyumba Mjifunze kuacha kulaumu watu na kufanya Political analysis bila ya kuwa na utaalamu!

Kuhamia kwa muajili mpya hakumaanishi kuisha kwa uhasama na uadui kwa watu aliotofautiana nao kimkakati na kimsimamo kwa miaka mingi....Wapo waliomchukia na kumsaka!na pengine ndo walitumia nguvu kumshawishi ahamie huko ili wajifiche ktk kivuli cha kusema yupo ktk chombo ambacho mmiliki ni rafiki wa dola!Majitu yenye roho za kimafia yana mbinu sana
 
Si ndio hawa walio mwalika NCHIMBI apokee maandamano ya wandishi wa habari wakilaani kifo cha Mwangosi? Sasa naanza kujua kwa nini kunaudhaifu mkubwa kwenye kuripoti habari.
 
U-DC na Vibahasha Uchwara ndivyo vitakavyowaponza Waandishi wa Nchi hii , Hata hapa Jf kuna wanafiki wengi sana , mara nyingi sisi tunaoanzisha au kuchangia kwenye Thread yoyote inayomhusu Saed au Mwanahalisi tumeishia kutukanwa pamoja na Kejeli Kedekede, Bali sasa ukweli wa Kubenea umejidhihirisha kuwa Anayeonja Asali Mwisho wake huchonga Mzinga ! Siku utakuja kusikia kwamba INVISIBLE katobolewa macho , hapo sasa ndiyo mtaanza oooh ! Liwalo na Liwe !
 
Hakupuuza, wala haukuwa "msimamo wa ajabu." Kuandika ushahidi wa maovu yanayodhaminiwa na Usalama wa Taifa na kukataa kuomba msamaha ni uzalendo, sio "msimamo wa ajabu!" Please!

Mkuu nionavyo hujamwelewa Bushfire kama sijakosea msimamo wa ajabu aliouzungumzia ni TEF si wa Kubenea"
 
Si ndio hawa walio mwalika NCHIMBI apokee maandamano ya wandishi wa habari wakilaani kifo cha Mwangosi? Sasa naanza kujua kwa nini kunaudhaifu mkubwa kwenye kuripoti habari.

Umeona eeenh" ndio hawa hawa waliochachamaliwa na Mzee wa Kwembe kati"
 
waaandishi wengi wa habari tanzania wapo kwenye mifuko ya wanasiasa-mafisadi na huu ni msingi wa tatizo maana wale ambao wameamua kuwa serious na kazi ya uandishi wa habari na kuandika kile kinachotakiwa kuandikwa wanapigwa vita na kuonekana wachochezi,wenye chuki na wanaolenga kuwaaribia watu-wanasiasa mafisadi na serikali!

kuna media house-tanzania zipo kwa ajili ya political interest tu,kulinda maslahi na kupigania maslahi ya wanasiasa ambao wanajijua kwamba si wasafi na wanakashfa nyingi za ufisadi!

kwa mfano new habari corporation wanaofuatiliwa historia ya vyombo vya habari wanajua ilikotoka na ilipo sasa kwa maana ya umiliki wa kampuni hii na malengo ya wamiliki wa sasa vilevile yanajulikana pia kwa wanaofuatilia mustakabali wa vyombo vya habari tanzania.

waandishi makini wa habari na vyombo makini vya habari vinajulikana na serikali imekuwa inaviandama kila uchao,waandishi makini na wanaozingatia maadili ya taaluma wanajulikana na serikali inawachukia na kuwaandama kwa kila aina ya kashfa,kesi zisizo na mantiki,kuwatenga,kuwawinda kila waendapo na kujaribu kuwadhuru mwili na hata kuwaua!


wakati sasa umefika kwa tasnia ya habari tanzania kuungana na kuwa na kauli moja,kuzingatia maadili ya taaluma ya habari,kuhakikisha kuwa sheria ya vyombo vya habari inapatikana na kumlinda mwandishi na kusimamia maadili ya kazi/taaluma,kuwabana na kuwadhibiti waandishi wa habari wala rushwa na ambao ni vibaraka wa mafisadi,kuset standard za watu wanaotakiwa kusimamia/kuongoza vyombo vya habari na sifa za kumiliki vyombo vya habari hali kadhalika!

nawasilisha!
 
kubenea mwenyewe ni mzigo kwa taifa, ina maana hapo anashangilia na kufurahia kibanda kuumizwa.........shame on him
 
Mkuki kwa nguruwe!.
Uzuri ni kuwa Habari Coop. haijafungiwa itumie magazeti yake kuomba msamaha kwa watesaji ili Kibanda asifuatwe huko Sauzi.
 
sijawahi kumkubali kubenea hata siku moja maana, kuna wakati alitumika sana kumchafua zitto, akajakuhamia kwa membe akamchafua sana, akatoka hapo akahamia kwa kwa lowassa, akamwandika saaaana.... huyu jamaa huwa anabadilika kutoka na ufadhili anaopata wala haandiki ukweli kama ambavyo jamii inamtizama. take time to make your brain busy to think all these events
 
`Halafu huwa nashangaa gazeti la ulimwengu la Raia Mwema linavyokwenda siku hizi. Limeshindwa kabisa kutake advantage ya kufungiwa Mwanahalisi ambalo yote mawili yalikuwa yanatoka siku moja - J'tano.

Naona wahariri wake nao wameshatekwa na serikali. Siku hizi limesheheni matangazo ya serikali na taasisi nyingine kibao (kama vile Daily News), hivyo unatarajia liikosoe serikali kama vile Mwanahalisi? No way!

Gazeti la akina Balile (Jamhuri) nale laonekana kutota kwani yeye na mwenzake Manyerere ni wachumia tumbo kutoka kwa wanasiasa wa magambaz -- hakuna lolote pale.

Kweli nali-miss Mwanahalisi!
 
Mbinu aliyotumia Kubenea kupata zile habari za watesaji wa Dr. Ulimboka ilikuwa ni ya hali ya juu na ya kitaalam mno kiasi kwamba waandishi wengi na hata Serikali yenyewe iliona kama habari za kuumba ama za kufikirika zaidi ya kubeba ukweli. Kwa wanahabari naona pamoja na kuwa na jukwaa lao lakini kiundani wanaonekana kufanyakazi yao kwa kuweka ubinafsi na kutekeleza maagizo ya wale waliowaajiri badala ya kufanya kazi kwa umoja na kuheshimu maadili ya kazi yao zaidi. Kimsingi waandishi wa habari wanatakiwa wawe na ujasiri wa kuzama kwenye maeneo hatarishi ili waweze kupata habari nzito/nyeti na za uhakika badala ya kusubiri kutoka vyanzo ambavyo si vya uhakika.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom