Kutenganisha uenyekiti na urais

Mwalimu alipokabidhi nchi kwa Mwinyi, aliendelea kuwa mwenyekiti wa chama hadi mwanzoni mwa miaka ya 90. Jambo hili likitokea halitakuwa jipya...! Kuongoza chama kinachounda serikali kuna manufaa yake. Kwanza unakuwa na nguvu kubwa dhidi ya serikali, kwa maana ya kusimamia ilani ya uchaguzi. Jambo hili litakuwa na ugumu kupita ingawa likitafsiriwa kihalisia linaweza kupita. Nia ya makundi yanayovutana kuhusiana na swala hili ndiyo hasa tatizo kubwa. Upande mmoja kunawanaotaka kurithisha wenzao kwa maslahi yao..!, upande wa pili ni wale wanaoona kuwa wanaonewa. Kuliweka jambo hili sawa hadi lipite ni kazi kubwa kama ilivyo kazi kubwa kulipinga lisipite. Upande utakaoshinda ndio utakaoshinda pia katika mpambano wa kusimamisha mgombea urais wa CCM. Ukishinda upande ulioko nje ya utawala, makubwa zaidi yatafuata. Hatutashangaa kuona yaliyotokea ANC. Nafikiri ni swala la wakati tu, muda ukifika majibu yatatojitokeza yenyewe bila kutafutwa.
 
Mkuu Gurtu

Nakushukuru kwa maoni yako. Ndiyo swala la kofia mbili la mwenyekiti na raisi siyo la kikatiba. Ndiyo wanaCCM wana haki ya kumuondoa au kumbakisha mwenyekiti kwa mujibu wa katiba na kanuni za chama. Ila kumbuka "change is constant". Huwezi kufanya vitu vile vile kila siku. Kuna ubaya gani wanachama kutafakari na kuamua kuwa ili kuwa na utendaji mzuri zaidi tutenganishe makofia haya? Haimaanishi yakitenganishwa itakuwa kwa JK tu.

Politics revolve. Mnaangalia nini kina fanya kazi na nini hakifanyi kazi. Saa nyingine kitu kinafanya kazi ila mnabudi mbinu za kuongeza ufanisi zaidi. Sasa kung'an'gania tu status quo ina hasara yake kwa dunia inazunguuka, siku zina sogea na mambo yana badilika. Kwa maana watu wote wangekua wanafikiria wewe unavyo fikiria basi hadi leo tungekua na chama kimoja tu na kiongozi mmoja anae kaa mpaka atakapo kufa. Hata Nyerere mwenyewe aliona umuhimu wa kuachia ngazi japo kikatiba angeweza kukaa mpaka mwisho wa uhai wake.

Kwa hiyo nakuchallenge mkuu try to thing outside the box. Mabadiliko siyo lazima yafanyike ila siyo vibaya kutafakari kama unacho fanya ni sahihi. Ndiyo maana kuna coming up with a plan, evaluating a plan then choosing to continue or discontinue the plan. Sasa ukizoea kupita njia moja tu ina maana utaipita hata ukijua mbeleni kuna shimo.

Ni hayo tu mkuu.
MwanaFalsafa1 nakuelewa na ninaimani mimi na wewe hatupo mbali.
Mabadiliko ndiyo yanayoleta maendeleo, hivyo ni muhimu yakawepo. Pia ninaelewa kuwa kuna baadhi ya mambo yanaweza yaka sahihi leo lakini kesho yakawa siyo sahihi. Jambo ambalo linanitatiza ni kuwa kufanya jambo ambalo linapaswa kuongozwa na katiba ni kuhujumu katiba. Kama madai ya wanaCCM ni kutaka kufanya mabadiliko inafaa wakabadilishe katiba. Vile vile mabadiliko ya katiba yafanywe kwa utaratibu uliowekwa.
 
MwanaFalsafa1 nakuelewa na ninaimani mimi na wewe hatupo mbali.
Mabadiliko ndiyo yanayoleta maendeleo, hivyo ni muhimu yakawepo. Pia ninaelewa kuwa kuna baadhi ya mambo yanaweza yaka sahihi leo lakini kesho yakawa siyo sahihi. Jambo ambalo linanitatiza ni kuwa kufanya jambo ambalo linapaswa kuongozwa na katiba ni kuhujumu katiba. Kama madai ya wanaCCM ni kutaka kufanya mabadiliko inafaa wakabadilishe katiba. Vile vile mabadiliko ya katiba yafanywe kwa utaratibu uliowekwa.

Lakini mkuu hakuna haja ya CCM kubadilisha katiba kwa vile swala la raisi kuwa mwenyekiti pia siyo la kikatiba bali mazoea kama zilivyo kuwa kelele za kupishana Watanganyika na Wazanzibar kwenye uraisi. Kwa maana hiyo kutenganisha kofia hizo mbili hakuta vunja katiba wala kanuni yoyote ya CCM. Nadhi kwenye siku za usoni hili swala la uenyekiti litaingizwa kwenye kanuni rasmi za chama iwe kuziunganisha au kuzitenganisha.
 
Nitafurahi sana siku hii topic ikiacha kuongelewa humu, maana ni sawa na kujadili maji ya mto yarudi rivazi. CCM wenye maamuzi kwa sasa ni Mkapa, Mwinyi, Msekwa na Kikwete. Hawawezi kwa namna yeyote kuruhusu raisi anyang'anywe uenyekiti, sahauni. So, tujadilini tu mambo mengine...
 
Back
Top Bottom