MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Sababu ambazo zitamfanya JK asikubali kofia za uenyekiti na uraisi zitenganishwe:
1. Atakua raisi wa kwanza kuvuliwa kofia hilo. Kwake yeye ataichukulia kama kuonekana dhaifu.
2. Itampunguzia nguvu na itapunguza hata nguvu zake kama raisi kwani kwa Tanzania chama ni serikali na serikali ni chama.
3. Adui wa kisiasa anaweza akaukwaa uenyekiti kitu ambacho kitamuweka kwenye hali ngumu.
4. Mgombea wa uraisi kupitia chama anatokea kwenye vikao na mkutano wa chama. Asipo kuwa mwenyekiti nguvu za kumteua mrithi au kuinfluence matokeo zitapungua.
Kwa nini itakua busara JK kukubali mabadiliko haya:
1. Chadema ilishaondoa dhana kuwa mwenyekiti wa uraisi lazima awe mgombea uraisi. Hii itaondoa dhana kwamba raisi lazima awe mwenyekiti.
2. Itampunguzia mzigo. Anaongoza serikali wakati ambapo kuna matatizo mengi mno. Labda kushughulikia matatizo ya nchi na ya chama kwa wakati mmoja kunampunguzia uwezo wa kuwa tumikia kikamilifu Watanzania. Si rahisi kutumikia mabosi wawili (Wananchi kupitia uraisi na wanachama kupitia CCM).
3. Itampunguzia lawama. Mwenyekiti akiwa mtu mwingine basi na huyo mwenyeliti atabeba baadhi ya lawama tofauti na sasa ambapo inambidi JK abebe lawama zote.
4. Japo in the short term anaweza kuona kama ni aibu kwake kuwa raisi aliye ruhusu kofia hizo zitenganishwe in the long run atakuja kuheshimika kwa uamuzi huo.
Je CCM ifuate njia gani kutenga kofia hizi pasipo migawanyiko zaidi?....
1. Wanaweza wakakubaliana kuwa atakapo staafu JK basi makofia hayo yata tenganishwa. Hivyo itamaanisha JK atabeba makofia hayo mawili mpaka atakapo maliza yeye na hii inaweza ikawa rahisi zaidi kwake kumezwa kuliko yeye kuvuliwa moja kwa moja.
2. CCM itumie busara na kupendekeza watu kwenye nafasi ya uenyekiti ambao wana heshimika na kuto kuwa na makundi yani a unifier rather than a divider.
3. Katiba ya chama ielezee kabisa nini zita kuwa kazi za mwenyekiti wa chama na kuhakikisha haziingiliani na za raisi iwapo raisi atakuwa wa CCM. Yani isije ikawa swala la power struggle kati ya mwenyekiti na raisi.
4. Ratiba wa uchaguzi wa chama ubadilishwe ili mwenyekiti achaguliwe mwaka mmoja kabla ya uchaguzi wa uraisi. Hii inamaanisha kama mgombea wa CCM atashinda uchaguzi tayari kutakua na mwenyekiti ambae bado ana miaka minne kumaliza muda wake.
Haya ni maoni yangu tu ila uamuzi ni wa chama. Mimi nadhani si vibaya makofia haya kutenganishwa kwani baadhi ya nchi kama Marekani raisi hana cheo rasmi ndani ya chama. Ila hata CCM ikibaki na mfumo huu huu si vibaya. Cha muhimu ni kuhakikisha kuwa uamuzi ni kwa manufaa ya chama na wananchi badala ya watu wachache wenye uchu wa madaraka. Ninacho muomba tu raisi na mwenyekiti wa CCM ni atafakari na kujiuliza kwa nini swala hili limekua hoja sasa na si wakati mwingine wowote ule?
1. Atakua raisi wa kwanza kuvuliwa kofia hilo. Kwake yeye ataichukulia kama kuonekana dhaifu.
2. Itampunguzia nguvu na itapunguza hata nguvu zake kama raisi kwani kwa Tanzania chama ni serikali na serikali ni chama.
3. Adui wa kisiasa anaweza akaukwaa uenyekiti kitu ambacho kitamuweka kwenye hali ngumu.
4. Mgombea wa uraisi kupitia chama anatokea kwenye vikao na mkutano wa chama. Asipo kuwa mwenyekiti nguvu za kumteua mrithi au kuinfluence matokeo zitapungua.
Kwa nini itakua busara JK kukubali mabadiliko haya:
1. Chadema ilishaondoa dhana kuwa mwenyekiti wa uraisi lazima awe mgombea uraisi. Hii itaondoa dhana kwamba raisi lazima awe mwenyekiti.
2. Itampunguzia mzigo. Anaongoza serikali wakati ambapo kuna matatizo mengi mno. Labda kushughulikia matatizo ya nchi na ya chama kwa wakati mmoja kunampunguzia uwezo wa kuwa tumikia kikamilifu Watanzania. Si rahisi kutumikia mabosi wawili (Wananchi kupitia uraisi na wanachama kupitia CCM).
3. Itampunguzia lawama. Mwenyekiti akiwa mtu mwingine basi na huyo mwenyeliti atabeba baadhi ya lawama tofauti na sasa ambapo inambidi JK abebe lawama zote.
4. Japo in the short term anaweza kuona kama ni aibu kwake kuwa raisi aliye ruhusu kofia hizo zitenganishwe in the long run atakuja kuheshimika kwa uamuzi huo.
Je CCM ifuate njia gani kutenga kofia hizi pasipo migawanyiko zaidi?....
1. Wanaweza wakakubaliana kuwa atakapo staafu JK basi makofia hayo yata tenganishwa. Hivyo itamaanisha JK atabeba makofia hayo mawili mpaka atakapo maliza yeye na hii inaweza ikawa rahisi zaidi kwake kumezwa kuliko yeye kuvuliwa moja kwa moja.
2. CCM itumie busara na kupendekeza watu kwenye nafasi ya uenyekiti ambao wana heshimika na kuto kuwa na makundi yani a unifier rather than a divider.
3. Katiba ya chama ielezee kabisa nini zita kuwa kazi za mwenyekiti wa chama na kuhakikisha haziingiliani na za raisi iwapo raisi atakuwa wa CCM. Yani isije ikawa swala la power struggle kati ya mwenyekiti na raisi.
4. Ratiba wa uchaguzi wa chama ubadilishwe ili mwenyekiti achaguliwe mwaka mmoja kabla ya uchaguzi wa uraisi. Hii inamaanisha kama mgombea wa CCM atashinda uchaguzi tayari kutakua na mwenyekiti ambae bado ana miaka minne kumaliza muda wake.
Haya ni maoni yangu tu ila uamuzi ni wa chama. Mimi nadhani si vibaya makofia haya kutenganishwa kwani baadhi ya nchi kama Marekani raisi hana cheo rasmi ndani ya chama. Ila hata CCM ikibaki na mfumo huu huu si vibaya. Cha muhimu ni kuhakikisha kuwa uamuzi ni kwa manufaa ya chama na wananchi badala ya watu wachache wenye uchu wa madaraka. Ninacho muomba tu raisi na mwenyekiti wa CCM ni atafakari na kujiuliza kwa nini swala hili limekua hoja sasa na si wakati mwingine wowote ule?