Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,793
- 12,238
Uimara na kuendelea kudumu kwa CCM kunatokana na nguvu za dola, nje ya hapo CCM ni chama dhaifu sana. Ndani ya CCM kuna wanachama waganga njaa wengi sana ambao maisha yao nje ya chama hayawezekani. Hivyo ili wanachama hawa waishi maisha ya heshima watafanya kila hila ili mwenyekiti wao awe Rais wa nchi.
Vurugu na mauaji ambayo hutokea wakati wa uchaguzi mkuu husimamiwa na hawa waganga njaa ndani ya CCM. Watu hawa kwa sasa wana wasiwasi mkubwa kuelekea kumsimika Rais Samia kuwa mwenyekiti mpya wa chama. Watafanya kila hila na hata kuua wapo tayari endapo vuguvugu hili la kutenganisha kofia litaendelea kupamba moto.
Kwa hiyo tahadhari ichukuliwe kwa ye yote atakayeweka wazi hoja hii vinginevyo ajiandae kuhama nchi endapo hoja yake itazimishwa si kwa kura bali kwa nguvu za dola. Bahati mbaya sana miongoni mwa waganga njaa ni viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wote ni wanachama wa CCM.
Vurugu na mauaji ambayo hutokea wakati wa uchaguzi mkuu husimamiwa na hawa waganga njaa ndani ya CCM. Watu hawa kwa sasa wana wasiwasi mkubwa kuelekea kumsimika Rais Samia kuwa mwenyekiti mpya wa chama. Watafanya kila hila na hata kuua wapo tayari endapo vuguvugu hili la kutenganisha kofia litaendelea kupamba moto.
Kwa hiyo tahadhari ichukuliwe kwa ye yote atakayeweka wazi hoja hii vinginevyo ajiandae kuhama nchi endapo hoja yake itazimishwa si kwa kura bali kwa nguvu za dola. Bahati mbaya sana miongoni mwa waganga njaa ni viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao wote ni wanachama wa CCM.