Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Kabla ya mauaji Rwanda viongozi wa kisiasa na vyombo vya dola waliminya watu Kama tunavyoshuhudia hapa nchini Sasa. Leo Mhe. Rais ametembelea Makaburi yaliyosababishwa na watu wachache walioona wao ndio waliozaliwa kutawala.
Mwenyenzi Mungu anakusudi kumpa safari siku chache baada ya dola kumweka Mbowe Ndani. Amepata safari hii kwa lengo la kujifunza madhara ya siasa chafu, kujifunza madhara yakutengeneza kundi la watawala na watawaliwa.
Nimeona uteuzi wake nadhani alilenga kuendeleza koo zile zile za akina zelothe, Robert, Katarahia, Nnauye na wa kariba hii. Hii ni nchi, watu wanaona na wanavumiliana. Matembezi yako Kwenye Makaburi yakufanye unaporejea nchini uliutubie Taifa, utoe dira upya ya wapi unataka tuelekee maana tumepoteana.
Ukiwa Rais utengenezewi jina zuri unatengeneza jina zuri, Waziri anaweza akatengenezewa jina na Rais lakini Rais Hana wakumtengenezea jina. Njoo nchini ukiwa unatafakari ufupi wa maisha yetu hapa Duniani, turejeshea amani.
Mwenyenzi Mungu anakusudi kumpa safari siku chache baada ya dola kumweka Mbowe Ndani. Amepata safari hii kwa lengo la kujifunza madhara ya siasa chafu, kujifunza madhara yakutengeneza kundi la watawala na watawaliwa.
Nimeona uteuzi wake nadhani alilenga kuendeleza koo zile zile za akina zelothe, Robert, Katarahia, Nnauye na wa kariba hii. Hii ni nchi, watu wanaona na wanavumiliana. Matembezi yako Kwenye Makaburi yakufanye unaporejea nchini uliutubie Taifa, utoe dira upya ya wapi unataka tuelekee maana tumepoteana.
Ukiwa Rais utengenezewi jina zuri unatengeneza jina zuri, Waziri anaweza akatengenezewa jina na Rais lakini Rais Hana wakumtengenezea jina. Njoo nchini ukiwa unatafakari ufupi wa maisha yetu hapa Duniani, turejeshea amani.