Wana JF wenzangu,
Naomba ifahamike kuwa kipato changu ni cha kawaida sana ila nina nia ya kutembela hifadhi ya taifa ya Mikumi mwezi Juni ili kufurahia rasimali zetu.
Plan yangu ni kutumia siku moja hifadhini.
Naomba kufahamu yafuatayo;-
1. Je naweza pata malazi aidha ndani au nje ya hifadhi kwa bajeti ya chini ya elfu 40 kwa siku?
2. Je, naweza fika Mikumi nikapata gari la kukodi kunizungusha hifadhini badala ya kwenda kulipia kwa package kwenye makapuni ya tours kama wafanyavyo watalii toka nje ya nchi? Kama ndio, naweza pata gari kwa bei gani?
NB: Nimewahi tembelea Tarangire. Nilienda kwa basi tu, nikashukia eneo la kibaoni. Nikakuta baadhi ya land cruiser zimepaki, wenyeji wakaniambia baadhi wanafanya deiwaka, hawana wateja. Nikaongea na dereva mmoja tukakubaliana 160,000 kwa siku.
Kwanza akanishauri ninunue lunch box then akanipeleka hifadhini nikalipia. Bahati nzuri nilikuta hostel/ lodge zinazomilikiwa na hifadhi zina nafasi. Nikalipia kabisa (20K au 25K kama sijasahau). Tulizunguka sana hifadhini. Around saa 9 akanipeleka Matete picnic nile lunch yangu (kuna mabenchi na vyoo safi). Baadae akanipeleka huko hostel/lodge nikalala, asubuhi akanifata kunitoa hifadhini.
Lodge nilikuta nzuri tu. Self contained, kitanda kizuri, free WiFi, tv.
Kwa kifupi nilitalii kwa gharama ya kawaida sana.
Naomba nijuzwe kuhusu Mikumi.
Naomba ifahamike kuwa kipato changu ni cha kawaida sana ila nina nia ya kutembela hifadhi ya taifa ya Mikumi mwezi Juni ili kufurahia rasimali zetu.
Plan yangu ni kutumia siku moja hifadhini.
Naomba kufahamu yafuatayo;-
1. Je naweza pata malazi aidha ndani au nje ya hifadhi kwa bajeti ya chini ya elfu 40 kwa siku?
2. Je, naweza fika Mikumi nikapata gari la kukodi kunizungusha hifadhini badala ya kwenda kulipia kwa package kwenye makapuni ya tours kama wafanyavyo watalii toka nje ya nchi? Kama ndio, naweza pata gari kwa bei gani?
NB: Nimewahi tembelea Tarangire. Nilienda kwa basi tu, nikashukia eneo la kibaoni. Nikakuta baadhi ya land cruiser zimepaki, wenyeji wakaniambia baadhi wanafanya deiwaka, hawana wateja. Nikaongea na dereva mmoja tukakubaliana 160,000 kwa siku.
Kwanza akanishauri ninunue lunch box then akanipeleka hifadhini nikalipia. Bahati nzuri nilikuta hostel/ lodge zinazomilikiwa na hifadhi zina nafasi. Nikalipia kabisa (20K au 25K kama sijasahau). Tulizunguka sana hifadhini. Around saa 9 akanipeleka Matete picnic nile lunch yangu (kuna mabenchi na vyoo safi). Baadae akanipeleka huko hostel/lodge nikalala, asubuhi akanifata kunitoa hifadhini.
Lodge nilikuta nzuri tu. Self contained, kitanda kizuri, free WiFi, tv.
Kwa kifupi nilitalii kwa gharama ya kawaida sana.
Naomba nijuzwe kuhusu Mikumi.