Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,780
Wengi wetu tumeshakumbana na hili tatizo aidha sisi wenyewe ama kupitia ndugu jamaa au hata rafiki, ni tatizo la kiufahamu ambalo husababishwa na matatizo mengine mwilini kama mfumo wa upumuaji kutokuwa sawa, shida kwenye mfumo wa kusukuma damu, madawa msongo wa mawazo uchovu fikra za kufikirika nk
Kiroho pia ina tafsiri yake kwamba hata unapokuwa umelala na hujitambui ufahamu wako huwa active na kufanya mengine yote bila wewe mwenyewe kwenye nafsi ya utashi ukishindwa kutambua lolote.
Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa hata wale wanga na wachawi wanaochukua watu usiku hutumia formula ya ufahamu kuchukua watu kwenda kuwafanyisha kazi kisha kuwarudisha bila wao kujitambua
Dalili za tatizo hili kwa baadhi huanza utotoni ambalo wala mtoto hana stress nk, na utakuta mtoto anaongea pekeyake bila kutoa sauti anakunjua sura ama kukunja na wakati mwingine kushtuka,(hapa mambo ya kishirikina pia huhusika sana)
Hali hii hutokea masaa takibran matatu baada ya kulala ama kwenye usingizi mzito usiku wa manane na huweza kudumu kuanzia sekunde 30 mpaka nususaa.
Tatizo hili hutofautiana ukubwa, wengine huamka tu kitandani na kuzunguka ndani ya chumba na kurudi kulala! Ila wengine huamka na kama ni mwanafunzi huvaa uniform kabisa na kutoka mpaka nje hata wafanyakazi pia!
Akiwa katika hali hiyo huweza kutembea mpaka hatua kadhaa kisha kurejea ndani na kulala tena huku mwenyewe kwenye hali ya utashi akiwa hajui lolote
Nimekutana na kesi za namna hiyo na watu wakitibiwa kwa kitunguu saumu ama ndimu(hii ni tiba mbadala)kwakuwa kwa hospitali hizi za kizungu hili halina tiba bali hupotea lenyewe au kwa njia ya kutibu chanzo, hasa kama limesababishwa na viashiria vya wazi kama madawa msukumo wa damu stress nk
Kiafrika haishauriwi kabisa kumshtua mtu anayetembea usingizini kwakuwa kile kitendo si utashi wake bali ni command ya ufahamu ambalo haukuwalisiana na nafsi ya utashi (kutenda kwa uamuzi)kinachotakiwa ni kumshika mkono na kumrudisha kitandani taratibu na mara nyingi ufahamu hutii....!
Si wote wanaoamka asubuhi wakiwa wachovu au wamechafuka miguu nk ni matendo ya kishirikina, wengine ni hili tatizo la kutembea usingizini.