Kutelekeza majina yetu ya asili na kung'ang'ania yale ya kigeni ni utumwa wa kifikra

African Believer

JF-Expert Member
Jul 30, 2015
436
425
Natumai wanajamvi wenzangu mu wazima,

Lengo la uzi wangu linakwenda sambamba na kichwa cha habari hapo juu.

Sababu kubwa iliyonihimiza kuandika ni kutoweka kwa kasi kwa ladha ya majina yenye asili ya Kiafrika na punde tu hatutasikia tena majina kama vile;
Nwangomale
Mushi, Massawe
Tibyampansha
Mwalukuta
Ambakisye,
Loibanguti
Anyosinsye
Ludelengeja
Mapunda
Makanyanga
Ng'ondwa
Mwakaringa
Mushumbusi
Nchimbi, Amanyisye, Ndomoji, Mwakibuja, Chasimba na mengine mengi yenye kupendeza na yanayoleta positive energy za kweli kabisa pindi yanapotamkwa.

Kwa miaka mingi sasa tangu ujio wa wageni katika maeneo yetu ya Afrika Mashariki hususani Tanzania watu wengi wamekua wakitelekeza majina yao ya kiasili na kukumbatia yale ya kigeni hata kama matamko yake yana maana sawa na majina yetu.

Mtu ataona ni sawa kumwita mtoto wake wa kimakonde jina kwa lugha ya kiaramu (Aramaic) ilhali neno mbadala la kimakonde likiwepo, mtu anamwita mtoto SEIF= UPANGA ila hawezi kumwita mwanae upanga.

Kwa kipindi cha nyuma kasi ya uitaji wa majina hayo ilikuwa si kubwa sana lakini katika zama hizi za kukua kwa sayansi na teknolojia imeongezeka mara dufu.

Mtu hamwiti mwanae jina ni mpaka akagoogle. Utawasikia mastaa wetu kama kina Nasibu Abdul ( akijiita diamond Platnamz) na wanae Tiffany na Prince Nillan, utamsikia Ray Kigosi akimwita kijana wake Jaden na hii ni mifano michache tu. Ninachoweza kusema huu ni utumwa wa kifikra (mind colonization) wa kuhisi kila cha wenzetu ni bora kuliko chetu.
 
sasa mtoto mdogo anaenyonya unaanzaje kumwita Mwakibinga..
Tuanzie hapo, Afu maana ya Mwakibinga ni nini? Binafsi sir name ni muhimu ya kumbukumbu ya origin yangu ila jina la kwanza la mtoto tusipangiane. Uzuri wa jina la mtu lina impact kubwa ktk maisha.
 
Tuanzie hapo, Afu maana ya Mwakibinga ni nini? Binafsi sir name ni muhimu ya kumbukumbu ya origin yangu ila jina la kwanza la mtoto tusipangiane. Uzuri wa jina la mtu lina impact kubwa ktk maisha.
swadakta mkuu...hayo majina yabakie kuwa origin tu...tuwaite watoto wetu majina mazuri yenye impact katika maisha yao...:D:D
 
Majina yetu ni magumu sana, unaskia mtu anaitwa mchambawima, mwakibolwa, tulia mwakifyogo
 
Embu acheni mambo ya kijinga, majina mengine nuksi tu, unakuta mtu anaitwa shida, siwazuri, mateso, siwema, siwatu bora wamakonde wao wameamua utakuta ntu anaitwa Train, knife na mengineyo
 
Tuanzie hapo, Afu maana ya Mwakibinga ni nini? Binafsi sir name ni muhimu ya kumbukumbu ya origin yangu ila jina la kwanza la mtoto tusipangiane. Uzuri wa jina la mtu lina impact kubwa ktk maisha.
Yana impact gani na hiyo impact inakujaje, tuelezane hapa
 
Embu acheni mambo ya kijinga, majina mengine nuksi tu, unakuta mtu anaitwa shida, siwazuri, mateso, siwema, siwatu bora wamakonde wao wameamua utakuta ntu anaitwa Train, knife na mengineyo
Yale yale ya Bitoz Nyangema kutaka aitwe 2PAC
 
Siwez mpa mwanangu majina ya Kiafrika.
Mikael
Gabriel
Raphael
Ndio majina watakayopewa
 
Yana impact gani na hiyo impact inakujaje, tuelezane hapa
mkuu correlation ipo...unakuta familia ime strugle kinyama kupata mtoto na pindi akipatikana utaskia anaitwa Tabu, Bahati..so haya majina ukiyaangalia utaona hiyo impact, kwamba wewe ni kumbukizi ya waloyoyapitia wazazi wako. Sasa hii si michongo zama hizi mkuu
 
Siwez mpa mwanangu majina ya Kiafrika.
Mikael
Gabriel
Raphael
Ndio majina watakayopewa
Hata wakoloni walipofika Afrika waliwaambia Waafrika kuwa majina yao ni ya kishenzi. Hivyo waliwapa majina uliyoyataja kama ishara ya ustaarabu jambo ambalo sio kweli.

Majina ni aina ya maneno ya utambulisho wa mtu, kitu, mahali au hali na hayana maana yoyote wala kazi nyingine zaidi ya kumtambulisha.
 
Naweza mwita jina la asili lakini lisiwe na maana mbaya, ninachoangalia ni maana ya jina basi
Malaika. Hili jina utadhani watu huwa hawalion ni machache sana ila sasa utaskia Nyamboga sijui nyanjige! Dah .. stak kwa kweli
 
Ni matumaini yangu mleta maada anavaa magome ya miti.... maana yeye ana allergy na vitu vya wazungu.... Ila sijui kwanini anaingia jamii forums.... wakati anatumia internet ya wazungu
 
Back
Top Bottom