Kutana na ‘Jeshi la Machinga’ lisilo na silaha linavyoitetemesha Serikali hadi inajificha uvunguni

Hakika machinga na kina mama wauza mboga mboga na matunda kwenye mabeseni na pembezoni mwa barabara wameishika sharubu serikali

Siku hizi hata hawasubiri jioni, miji mingine saa tano mchana unakuta barabara hazipitiki, parking zimezibwa, watembea kwa miguu ndo hawana hata pa kukanyga

Ole wake mgambo awaguse! Mkurugenzi hana kazi!

DC wa Morogoro yeye ameamua kukopa kwa ajili ya kuwajengea mabanda, halafu Cha ajabu mabanda yamejengwa palipoandaliwa Kama parking ya soko kuu la Chief kingalu.

Yaani ndani ya soko maduka na vioski viko empty halafu DC anakopa pesa kuwajengea mabanda nje ya soko. Kwani wangepewa vibanda humo ndani hawawezi fanya kazi!? Soko limejengwa likaliwe na mijusi na popo au nini!!
Ukipanga ndani ya soko unalipa tozo.

Nje ya soko Kuna kibanda machinga kapewa bure na halipi tozo.

Huyu kijana alikua very intelligent alipokua cdm. I am wondering what went wrong.
 
Usi wa overrate kihivyo. Hao ni asset ya wanasiasa. Wanaogopa kuvurunda kura zitapita kushoto.

Ila ukiweka siasa pembeni serikal inaweza kuwa move chap na hakuna atakae bisha

Serekali isiyo na uhalali wa umma haina uwezo wa kuwafanya chochote wamachinga. Wanajua kabisa wakiwagusa wanachinga huku hawajaingia madarakani kwa kura halali, ni kujisogeza kwenye shimo la kupoteza madaraka.
 
Kwa taarifa hao machinga ni cdm mwanzo mwisho. Hata Magufuli kuwaruhusu kufanya biashara popote ilikuwa ni kuwapora cdm washabiki. Kwa sasa serikali haina cha kuwafanya, maana inajua ni rahisi kutumiwa na Cdm kwani serikali hii ya majizi ya kura inajua haina uhalali wa umma.
Mkuu wamachinga wanawachukia sana chadema!

Si uliona yule belgiji kipindi kile cha kampeni akajifanya kujipitisha kununua mitumba kule soko sijui la wapi watu wakawa wanamuangalia.

Baadae tena akajifanya kwenda kununua nyanya kariakoo watu wakampuuza tena
 
Wana Jf,

Ukisikia kila mkoa una majeshi ya serikali, lakini jeshi butu lisilo na siraha wala chombo chochote hatarishi, jeshi la machinga lilijijengea nguvu za kutisha kiasi kwamba linaogopeka sana.

Jeshi hili nimeShuhudia pale kaliakoo wakiondoa magari yanayoegeshwa kwa ajiri ya parking system watumishi wakitishiwa na wateja wa maduka wakiondoa garibaldi nao. Ukikaidi kuondoa basi kama tairi haitatatobolewa basi utakuta hakuna upepo.

Jeshi la machinga limethubutu kuifanya mwendokasi akifika maeneo yao atembee mwendo wa kinyoga sana huku akiwakwepa kwa umahili. Tanesco wanashangaa nguo kupangwa kwenye transforma

Tanroads hasa ndio kabisa nguzo za kuongozea taa zinazibwa.

Hivi hawa wanaodaiwa ndio wapiga kura hivi ndio walipa kodiak wakubwa kiasi hicho cha kupendelewa?
Wewe Ndugu nadhani hujaelewa vizuri concept ya machinga ...usiwachukulie poa wamachinga ...na usidhani ni hao tu wanaotandaza bidhaa mitaani...machinga ni pamoja na mamilioni ya wasio na ajira na hasa mitaani...ni pamoja na bodaboda, bajaji Mama ntilie au Mama lishe, watu wa kipato Cha chini....ni kundi kubwa Sana..wanafunzi pia wamo...kundi hili kwa Sasa linaungwa mkono na hata na baadhi ya wasomi...wamachinga wenyewe wamo pia wenye digrii au. Diplona...vyuo vinamwaga vijana Kila mwaka na hawana ajira na baadhi wanaishia kuendesha bodaboda, bajaji kuuza vocha na vibanda vya tigo pesa na mpesa..hili ni kundi hatari...na likitokea. La kutokea kundi hili halina Cha kupoteza isipokuwa minyororo yao ya mateso ya maisha. Eti halina silaha???!! Subirini ghasia zitokee ndipo ujue silaha zake ..
 
Kwa taarifa hao machinga ni cdm mwanzo mwisho. Hata Magufuli kuwaruhusu kufanya biashara popote ilikuwa ni kuwapora cdm washabiki. Kwa sasa serikali haina cha kuwafanya, maana inajua ni rahisi kutumiwa na Cdm kwani serikali hii ya majizi ya kura inajua haina uhalali wa umma.
Ilikuwa zamani enzi za kina Slaa wakati ule wana nyanyaswa na selikali ya JK kina Lema wakawa wanatumia mwanya huo kuwafanyisha maandamano.

Nakumbuka hadi bungeni kina Lema wakawa wanafoka kwamba hao watu waruhusiwe kufanya biashara popote hii ni nchi yao

Yani bavicha hii ya sasa hakuna wa kuniambia kitu.
 
Ilikuwa zamani enzi za kina Slaa wakati ule wana nyanyaswa na selikali ya JK kina Lema wakawa wanatumia mwanya huo kuwafanyisha maandamano.

Nakumbuka hadi bungeni kina Lema wakawa wanafoka kwamba hao watu waruhusiwe kufanya biashara popote hii ni nchi yao

Yani bavicha hii ya sasa hakuna wa kuniambia kitu.
Ilikuwa zamani wakati sasa hivi ccm ndio wanafanya wizi wa kura wakimachomacho baada ya kujua hawana ushawishi tena!?
 
Ajiri hutoona machinga
Wasomi wengi ndio machinga waliokoswa ajira
Ogopa walivyo wachungu umemkalisha shuleni umemnyima ajira leo ajiajiri umuletee nyoko hapo lazima mtauana..
Serikali ijitathimini sana hili ni bomu wakiligusa vibaya tutapoteana
 
Usi wa overrate kihivyo. Hao ni asset ya wanasiasa. Wanaogopa kuvurunda kura zitapita kushoto.

Ila ukiweka siasa pembeni serikali inaweza kuwa move chap na hakuna atakae bisha
Machinga ni MTAJI wa WANASIASA na WAFANYABIASHARA WAKUBWA.

1- Wanasiasa wanataka KURA na UTULIVU.

2- Wafanyabiashara wakubwa wanahitaji WAUZAJI wa BIDHAA zao.
 
Ukipanga ndani ya soko unalipa tozo.

Nje ya soko Kuna kibanda machinga kapewa bure na halipi tozo.

Huyu kijana alikua very intelligent alipokua cdm. I am wondering what went wrong.
Kaambukizwa ujinga
 
Usi wa overrate kihivyo. Hao ni asset ya wanasiasa. Wanaogopa kuvurunda kura zitapita kushoto.

Ila ukiweka siasa pembeni serikali inaweza kuwa move chap na hakuna atakae bisha
Basi Makala ndio kaingia kati sijui ataweza
 
Wamewaibia kura ngapi mwaka jana?
Mwaka jana hawakuiba, bali Magufuli kwa ulevi wake wa kiburi cha madaraka, aliagiza wagombea wa ccm ikiwemo yeye watangazwe washindi kwa shuruti
 
Machinga ni wale wanatembeza bidhaa ambazo zinatumika in an instant kama vile soft drinks, bites , handkerchief, miwani, saa, earphones.
Lakini sasa unakuta mtu anauza vyombo, mashuka, nguo, viatu, matunda ya kwenda kumenya nyumbani, mama ntilie, mafundi simu/ pc n.k na ameweka kibanda cha kudumu kwenye eneo la barabara dah! Sababu ya ushenzi wa siasa.
Umachinga unapaswa kuwa kama ule wa Bakhresa kuwanunulia watu wake vibaiskeli vya kuuza ice cream na vibegi vyenye coolbox vya kuuza 'ukwaju', hii ya mabanda barabarani na kwenye mitaro ni uchafu!!!
 
Sisi machinga tumeshatoa rai, tuguse tunuke
Nenda posta kesho ukaone, wenyewe tu wanabomoa mabanda yao kwa hiari yao tu, huko kunuka kinuke vipi?mikwara tu, na kituo kinachofuata ni kariakoo hapo sasa ndio mnapaita makao makuu ya kambi ya jeshi!!!ni siasa tu, mwenyewe tu unajikata, zamu hii hawatumii nguvu ili mje kutaka huruma kutoka kwa rais!!!wewe unakuta city centre , wakina mama wanapasua kuni za kuchomea mihogo, wengine wanashindilia majiko ya pumba!!!ila mwendazakeeee!!!
SASA NIA, UWEZO UPO, LAZIMA MPISHE TU, na kama nguvu kiasi ikibidi kutumika kwa watu kama nyie itatumika tu, ile ya RUNGU ZA UGOKO.
 
Back
Top Bottom